Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 25.12
Bible en Swahili de l’est


Paul devant le gouverneur Festus

1 Hata Festo alipokwisha kuingia katika uliwali, baada ya siku tatu akapanda kwenda Yerusalemu kutoka Kaisaria.
Actes 23.34 Actes 21.15 Actes 25.5 Actes 18.22 Actes 8.40
2 Kuhani Mkuu na wakuu wa Wayahudi wakampasha habari za Paulo, wakamsihi,
Actes 25.15 Actes 24.1 Romains 3.12-3.19 Job 31.31 Proverbes 4.16
3 na kumwomba fadhili juu yake, kwamba atoe amri aletwe Yerusalemu, wapate kumwotea na kumwua njiani.
Psaumes 140.1-140.5 1 Samuel 23.19-23.21 Actes 26.9-26.11 Jean 16.3 Actes 9.2
4 Lakini Festo akajibu ya kwamba Paulo analindwa Kaisaria; naye mwenyewe yu tayari kwenda huko karibu.
Actes 24.23
5 Akasema, Wale walio na mamlaka kwenu na watelemke pamoja nami wakamshitaki, ikiwa liko neno baya katika mtu huyu.
Actes 25.18-25.19 Actes 23.30 Actes 18.14 Actes 24.8 Psaumes 7.3-7.5
6 Alipokwisha kukaa kwao siku nane au kumi si zaidi, akatelemkia Kaisaria; hata siku ya pili akaketi katika kiti cha hukumu akaamuru Paulo aletwe.
Actes 25.17 Actes 25.10 Matthieu 27.19 2 Corinthiens 5.10 Actes 18.12-18.17
7 Alipokuja, wale Wayahudi walioshuka kutoka Yerusalemu wakasimama karibu yake wakaleta mashitaka mengi mazito juu yake, wasiyoweza kuyayakinisha.
Actes 24.13 Actes 24.5-24.6 Luc 23.10 Luc 23.2 Marc 15.3-15.4
8 Paulo akasema akijitetea, Mimi sikukosa neno juu ya sheria ya Wayahudi, wala juu ya hekalu, wala juu ya Kaisari.
Actes 28.17 Actes 24.12 Jérémie 37.18 Daniel 6.22 Actes 25.10
9 Lakini Festo akitaka kujipendekeza kwa Wayahudi akamjibu Paulo, akisema, Je! Wataka kwenda Yerusalemu, ukahukumiwe huko mbele yangu kwa ajili ya mambo hayo?
Actes 24.27 Actes 25.20 Actes 12.3 Marc 15.15 Actes 25.3
10 Paulo akasema, Mimi ninasimama hapa mbele ya kiti cha hukumu cha Kaisari, ndipo panipasapo kuhukumiwa; sikuwakosa Wayahudi neno, kama wewe ujuavyo sana.
2 Corinthiens 4.2 Actes 22.25-22.28 Actes 23.29 Actes 26.31 Actes 25.25
11 Basi ikiwa ni mkosa au nimetenda neno la kustahili kufa, sikatai kufa; bali, kama si kweli neno hili wanalonishitaki, hapana awezaye kunitia mikononi mwao. Nataka rufani kwa Kaisari.
Actes 28.19 Actes 26.32 Actes 25.25 Job 31.38-31.40 Actes 18.14
12 Basi Festo alipokwisha kusema na watu wa baraza, akajibu, Umetaka rufani kwa Kaisari! Basi, utakwenda kwa Kaisari.
Actes 26.32-27.1 Actes 25.21 Psaumes 76.10 Philippiens 1.20 Philippiens 1.12-1.14
13 Siku kadha wa kadha zilipokwisha kupita, Agripa mfalme na Bernike wakafika Kaisaria, wakimwamkia Festo.
1 Samuel 25.14 2 Samuel 8.10 Actes 26.27-26.28 Actes 8.40 1 Samuel 13.10
14 Na walipokuwa wakikaa huko siku nyingi, Festo akamweleza mfalme habari za Paulo, akisema, Yupo hapa mtu mmoja aliyeachwa na Feliki kifungoni;
Actes 24.27
15 ambaye nilipokuwa Yerusalemu wakuu wa makuhani na wazee wa Wayahudi wakaniarifu habari zake, wakinitaka hukumu juu yake.
Luc 23.23 Esther 3.9 Actes 25.1-25.3 Actes 24.1 Luc 18.3-18.5
16 Nikawajibu kwamba si desturi ya Warumi kumtoa mtu awaye yote, kabla mtu yule aliyeshitakiwa hajaonana na washitaki wake uso kwa uso, na kupewa nafasi ya kujitetea katika mashitaka yake.
Actes 25.4-25.5 Actes 23.30 Jean 7.51 Actes 26.1 Proverbes 18.13
17 Basi walipokutanika hapa sikukawia; bali siku ya pili nikaketi katika kiti cha hukumu nikaamuru mtu huyo aletwe.
Actes 25.10 Actes 25.6
18 Na wale waliomshitaki waliposimama hawakuleta neno lo lote baya, kama nilivyodhani,
19 bali walikuwa na maswali mengine mengine juu yake katika dini yao wenyewe, na katika habari ya mtu mmoja Yesu, aliyekuwa amekwisha kufa, ambaye Paulo alikaza kusema kwamba yu hai.
Actes 18.15 Actes 23.29 Actes 26.22-26.23 1 Corinthiens 15.14-15.20 Actes 25.7
20 Nami nikaona shaka jinsi ya kutafuta hakika ya habari hii, nikamwuliza kama anataka kwenda Yerusalemu ahukumiwe huko katika mambo haya.
Actes 25.9
21 Lakini Paulo alipodai kuwekwa ahukumiwe na Kaisari, nikaamuru alindwe hata nitakapompeleka kwa Kaisari.
2 Timothée 4.16 Actes 25.10-25.11 Actes 26.32-27.1 Luc 2.1
22 Agripa akamwambia Festo, Mimi nami nalikuwa nikitaka kumsikia mtu huyu. Akasema, Utamsikia kesho.
Actes 9.15 Luc 21.12 Matthieu 10.18 Esaïe 52.15
23 Hata asubuhi Agripa akaja pamoja na Bernike kwa fahari nyingi, wakaingia mahali pa kusikia maneno, pamoja na maakida wakuu na watu wakuu wa mji; Festo akatoa amri, Paulo akaletwa.
Actes 26.30 Actes 25.13 Actes 12.21 Ezéchiel 32.12 1 Jean 2.16
24 Festo akasema, Mfalme Agripa, na ninyi nyote mliopo hapa pamoja nasi, mnamwona mtu huyu, ambaye jamii yote ya Wayahudi huko Yerusalemu na hapa pia wamenitaka niwasaidie, wakipiga kelele kwamba haimpasi kuishi zaidi.
Actes 25.7 Actes 22.22 Actes 25.2-25.3 Luc 23.21-23.23
25 Lakini mimi naliona kwamba hakutenda neno la kustahili kuuawa, na yeye mwenyewe alipotaka kuhukumiwa na Kaisari, nalikusudia kumpeleka kwake.
Actes 23.29 Luc 23.4 Actes 23.9 Actes 25.11-25.12 Luc 23.14
26 Nami katika habari yake sina neno la hakika la kumwandikia bwana. Kwa hiyo nimemleta hapa mbele yenu, hasa mbele yako wewe, mfalme Agripa, ili akiisha kuulizwa-ulizwa nipate neno la kuandika.
Actes 26.2-26.3
27 Kwa maana naona ni neno lisilo maana kumpeleka mfungwa, bila kuonyesha mashitaka yale aliyoshitakiwa.
Proverbes 18.13 Jean 7.51

Cette Bible est dans le domaine public.