Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 11.18
Bible en Swahili de l’est


1 Basi mitume na ndugu waliokuwako katika Uyahudi wakapata habari ya kwamba watu wa Mataifa nao wamelipokea neno la Mungu.
Galates 1.17-1.22 Esaïe 11.10 Jérémie 16.19 Esaïe 52.10 Sophonie 2.11
2 Na Petro alipopanda kwenda Yerusalemu, wale walio wa tohara wakashindana naye,
Actes 10.45 Actes 15.1 Actes 15.5 Galates 2.12-2.14 Actes 21.20-21.23
3 wakisema, Uliingia kwa watu wasiotahiriwa ukala nao.
Actes 10.28 Luc 15.2 Galates 2.12 Actes 10.23 Actes 10.48
4 Petro akaanza kuwaeleza kwa taratibu, akasema,
Luc 1.3 Josué 22.21-22.31 Proverbes 15.1 Actes 14.27
5 Nalikuwa katika mji wa Yafa, nikiomba, roho yangu ikazimia, nikaona maono; chombo kinashuka, kama nguo kubwa inatelemshwa kutoka mbinguni kwa pembe zake nne, kikanifikilia.
Actes 10.9-10.32 Actes 22.17 Amos 7.4-7.7 Actes 9.10 Jérémie 1.11-1.14
6 Nikakitazama sana, nikifikiri, nikaona wanyama wa nchi wenye miguu minne, na wanyama wa mwituni, nao watambaao, na ndege wa angani.
Actes 3.4 Luc 4.20
7 Nikasikia na sauti ikiniambia, Ondoka, Petro, ukachinje ule.
8 Nikasema, Hasha, Bwana, kwa maana kitu kilicho kichafu au kilicho najisi hakijaingia kabisa kinywani mwangu.
Romains 14.14 Osée 9.3 Esdras 9.11-9.12 Lévitique 11.47 Lévitique 10.10
9 Sauti ikanijibu mara ya pili kutoka mbinguni, Alivyovitakasa Mungu, usivinene wewe najisi.
Actes 15.9 Hébreux 9.13-9.14 Actes 10.34-10.35 Actes 10.15 1 Timothée 4.5
10 Jambo hili likatendeka mara tatu, kisha vitu vyote vikavutwa tena juu mbinguni.
2 Corinthiens 12.8 Nombres 24.10 Jean 21.17 Jean 13.38
11 Na tazama, mara hiyo watu watatu wakasimama mbele ya nyumba tuliyokuwamo, waliotumwa kwangu kutoka Kaisaria.
Exode 4.27 Actes 10.17-10.18 Actes 9.10-9.12 Exode 4.14
12 Roho akaniambia nifuatane nao, nisione tashwishi. Ndugu hawa sita nao wakaenda pamoja nami, tukaingia katika nyumba ya mtu yule;
Actes 8.29 Actes 10.23 Actes 16.6-16.7 Actes 15.9 Actes 10.45
13 akatueleza jinsi alivyomwona malaika aliyesimama nyumbani mwake na kumwambia, Tuma watu kwenda Yafa ukamwite Simoni aitwaye Petro,
Actes 10.30-10.32 Actes 12.11 Actes 9.43 Actes 10.3-10.6 Actes 10.22
14 atakayekuambia maneno ambayo yatakuokoa, wewe na nyumba yako yote.
Actes 16.15 Actes 10.22 Actes 16.31-16.34 Jean 4.53 Marc 16.16
15 Ikawa nilipoanza kunena, Roho Mtakatifu akawashukia kama alivyotushukia sisi mwanzo.
Actes 10.34-10.46 Actes 2.2-2.12 Actes 4.31 Actes 19.6
16 Nikalikumbuka neno lile la Bwana, jinsi alivyosema, Yohana alibatiza kwa maji kweli, bali ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
Actes 1.5 Marc 1.8 Jean 14.26 Proverbes 1.23 Matthieu 3.11
17 Basi ikiwa Mwenyezi Mungu amewapa wao karama ile ile aliyotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani niweze kumpinga Mungu?
Actes 10.47 Matthieu 20.14-20.15 Job 9.12-9.14 Job 40.8-40.9 Romains 9.20-9.26
18 Waliposikia maneno haya wakanyamaza, wakamtukuza Mungu, wakisema, Basi, Mungu amewajalia hata mataifa nao toba liletalo uzima.
2 Corinthiens 7.10 Romains 10.12-10.13 Actes 5.31 Actes 20.21 Actes 21.20

L’Évangile à Antioche de Syrie

19 Basi wale waliotawanyika kwa sababu ya ile dhiki iliyotukia kwa habari ya Stefano, wakasafiri hata Foinike na Kipro na Antiokia, wasilihubiri lile neno ila kwa Wayahudi peke yao.
Actes 15.3 Actes 15.22 Actes 15.35 Actes 21.2 Actes 4.36
20 Lakini baadhi ya hao walikuwa watu wa Kipro na Kirene, nao walipofika Antiokia wakasema na Wayahudi wa Kiyunani, wakihubiri habari njema za Bwana Yesu.
Matthieu 27.32 Actes 13.1 Actes 6.9 Actes 2.10 Actes 5.42-6.1
21 Mkono wa Bwana ukawa pamoja nao, watu wengi wakaamini, wakamwelekea Bwana.
Luc 1.66 Actes 2.47 Actes 9.35 Néhémie 2.18 Esaïe 59.1
22 Habari hizo za watu hao zikafika masikioni mwa kanisa lililokuwako katika Yerusalemu; wakamtuma Barnaba, aende hata Antiokia.
Actes 11.1 Actes 15.22 Actes 15.2 Actes 4.36-4.37 Actes 8.14
23 Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo.
Actes 13.43 Colossiens 1.6 2 Timothée 3.10 Actes 14.22 Actes 14.26
24 Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.
Actes 5.14 Actes 11.21 Actes 6.5 Actes 9.31 Proverbes 13.22
25 Kisha akatoka akaenda Tarso kumtafuta Sauli;
Actes 9.11 Actes 9.30 Actes 21.39 Actes 9.27
26 hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia.
Actes 26.28 1 Pierre 4.16 Actes 11.27 Actes 11.22 Actes 14.27
27 Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia.
Actes 13.1 1 Corinthiens 12.28 Actes 2.17 Actes 15.32 Ephésiens 4.11
28 Na tulipokusanyika akasimama mmoja wao, jina lake Agabo, akaonyesha kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itakuja karibu katika dunia nzima, nayo ikatukia katika siku za Klaudio.
Actes 21.10 Actes 18.2 Luc 3.1 1 Rois 17.1-17.16 Luc 2.1
29 Na wale wanafunzi, kila mtu kwa kadiri ya alivyofanikiwa, wakaazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi.
Actes 11.26 Luc 12.29-12.33 Hébreux 13.5-13.6 2 Corinthiens 8.12-8.14 Esdras 2.69
30 Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.
Actes 12.25 Actes 14.23 1 Timothée 5.17 Actes 16.4 Actes 15.4

Cette Bible est dans le domaine public.