Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 19.32
Bible en Swahili de l’est


1 Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.
Josué 2.1 Josué 6.1-6.27 2 Rois 2.18-2.22 Luc 18.35 1 Rois 16.34
2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.
Luc 18.24-18.27 2 Chroniques 17.5-17.6
3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.
Jean 12.21 Luc 23.8 Luc 9.7-9.9 Luc 12.25
4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.
1 Rois 10.27 Esaïe 9.10 1 Chroniques 27.28 Luc 5.19 Psaumes 78.47
5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako.
Apocalypse 3.20 Jean 14.23 Jean 1.48 Ephésiens 3.17 Jean 4.7-4.10
6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.
Actes 16.34 Esaïe 64.5 Galates 1.15-1.16 Genèse 18.6-18.7 Actes 16.15
7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.
Luc 15.2 Matthieu 9.11 Luc 7.39 Luc 7.34 Luc 18.9-18.14
8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.
2 Samuel 12.6 Exode 22.1-22.4 Jacques 1.10-1.11 Luc 12.33 Lévitique 6.1-6.6
9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.
Galates 3.7 Romains 4.16 Luc 13.16 Romains 4.11-4.12 Jean 4.38-4.42
10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.
Ezéchiel 34.16 1 Timothée 1.13-1.16 Luc 15.4-15.7 Luc 15.32 Matthieu 15.24

Parabole des serviteurs et des récompenses

11 Waliposikia hayo, aliongeza kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu utaonekana mara.
Luc 17.20 Actes 1.6 2 Thessaloniciens 2.1-2.3
12 Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.
Matthieu 25.14-25.30 Luc 24.51 1 Corinthiens 15.25 Philippiens 2.9-2.11 Actes 17.31
13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, Fanyeni biashara hata nitakapokuja.
2 Pierre 1.1 1 Pierre 4.9-4.11 Matthieu 25.14-25.15 Jean 12.26 Jacques 1.1
14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.
Zacharie 11.8 Psaumes 2.1-2.3 Actes 4.27-4.28 Actes 7.51-7.52 Luc 19.27
15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.
Matthieu 18.23-18.35 1 Corinthiens 4.1-4.5 Psaumes 2.4-2.6 Luc 12.48 Matthieu 25.19
16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.
1 Chroniques 29.14-29.16 1 Corinthiens 15.10 Jacques 2.18-2.26 2 Timothée 4.7-4.8 Colossiens 1.28-1.29
17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.
Luc 16.10 Matthieu 25.21 1 Corinthiens 4.5 Apocalypse 2.26-2.29 Genèse 39.4
18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.
Matthieu 13.23 Marc 4.20 2 Corinthiens 8.12
19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.
1 Corinthiens 15.41-15.42 1 Corinthiens 3.8 1 Corinthiens 15.58 Esaïe 3.10 2 Jean 1.8
20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.
Jacques 4.17 Proverbes 26.13-26.16 Matthieu 25.24 Luc 19.13 Luc 6.46
21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.
1 Samuel 12.20 2 Timothée 1.7 Ezéchiel 18.25-18.29 Job 21.14-21.15 Matthieu 25.24-25.25
22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;
2 Samuel 1.16 Matthieu 22.12 Matthieu 25.26-25.27 Matthieu 12.37 Romains 3.19
23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?
Exode 22.25-22.27 Deutéronome 23.19-23.20 Romains 2.4-2.5
24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.
Luc 16.2 Luc 12.20
25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.
2 Samuel 7.19 Esaïe 55.8-55.9 Luc 16.2
26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho.
Matthieu 13.12 Luc 8.18 2 Jean 1.8 Matthieu 25.28-25.29 Marc 4.25
27 Tena, wale adui zangu, wasiotaka niwatawale, waleteni hapa mwachinje mbele yangu.
Nombres 16.30-16.35 Nombres 14.36-14.37 Luc 19.14 Matthieu 22.7 Luc 20.16

Entrée triomphale de Jésus à Jérusalem

28 Na alipokwisha kusema hayo, alitangulia mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
Luc 9.51 Jean 18.11 Luc 12.50 Psaumes 40.6-40.8 1 Pierre 4.1
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, kwenye mlima uitwao wa Mizeituni, alituma wawili katika wale wanafunzi,
Actes 1.12 Zacharie 14.4 Luc 24.50 Luc 19.37 Matthieu 21.1-21.11
30 akisema, Nendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mtakapoingia ndani mtaona mwana-punda, amefungwa, ambaye hajapandwa na mtu ye yote bado, mfungueni mkamlete hapa.
Luc 22.8-22.13 Jean 14.29 1 Samuel 10.2-10.9 Luc 19.32
31 Na kama mtu akiwauliza, Mbona mnamfungua? Semeni hivi, Bwana anamhitaji.
Psaumes 24.1 Actes 10.36 Psaumes 50.10-50.12 Matthieu 21.2-21.3 Marc 11.3-11.6
32 Na wale waliotumwa wakaenda wakaona kama alivyowaambia.
Luc 22.13
33 Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda?
34 Wakasema, Bwana ana haja naye.
Zacharie 9.9 2 Corinthiens 8.9 Jean 10.35 Jean 12.16
35 Wakampeleka kwa Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana-punda, wakampandisha Yesu.
Marc 11.7-11.8 Jean 12.14 Matthieu 21.7 Galates 4.15-4.16 2 Rois 9.13
36 Na alipokuwa akienda walitandaza nguo zao njiani.
2 Rois 9.13 Matthieu 21.8
37 Hata alipokuwa amekaribia matelemko ya mlima wa Mizeituni, kundi zima la wanafunzi wake walianza kufurahi na kumsifu Mungu kwa sauti kuu, kwa ajili ya matendo yote ya uwezo waliyoyaona,
Juges 5.1-5.31 1 Rois 8.55-8.56 Marc 14.26 2 Samuel 6.2-6.6 2 Chroniques 29.28-29.30
38 wakasema, Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana; amani mbinguni, na utukufu huko juu.
Luc 13.35 Psaumes 72.17-72.19 Matthieu 21.9 Marc 11.9-11.10 Zacharie 9.9
39 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, uwakanye wanafunzi wako.
Actes 4.1-4.2 Jean 12.19 Jacques 4.5 Jean 12.10 Actes 4.16-4.18
40 Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, mawe yatapiga kelele.
Habakuk 2.11 Esaïe 55.12 Matthieu 21.15-21.16 Psaumes 98.7-98.9 Psaumes 114.1-114.8
41 Alipofika karibu aliuona mji, akaulilia,
Jean 11.35 Jérémie 13.17 Jérémie 17.16 Luc 13.34-13.35 Psaumes 119.53
42 akisema, Laiti ungalijua, hata wewe katika siku hii, yapasayo amani! Lakini sasa yamefichwa machoni pako.
Deutéronome 32.29 Matthieu 13.14-13.15 Romains 11.7-11.10 Luc 10.5-10.6 Esaïe 29.10-29.14
43 Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote;
Ezéchiel 4.2 Ezéchiel 26.8 Matthieu 22.7 Luc 21.20-21.24 Matthieu 23.37-23.39
44 watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua majira ya kujiliwa kwako.
1 Pierre 2.12 Luc 21.6 Matthieu 24.2 Marc 13.2 Daniel 9.24
45 Akaingia hekaluni, akaanza kuwatoa wale waliokuwa wakifanya biashara,
Matthieu 21.12-21.13 Marc 11.15-11.17 Deutéronome 14.25-14.26 Jean 2.13-2.17
46 akiwaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.
Esaïe 56.7 Jérémie 7.11 Ezéchiel 43.12 Psaumes 93.5 Matthieu 23.13
47 Naye akawa akifundisha kila siku hekaluni. Lakini wakuu wa makuhani, na waandishi, na wakuu wa watu walikuwa wakitafuta njia ya kumwangamiza;
Marc 11.18 Matthieu 26.55 Marc 14.1 Marc 11.27-11.33 Matthieu 21.23
48 wasione la kutenda, kwa kuwa watu wote walikuwa wakiandamana naye, wakimsikiliza.
Luc 20.19-20.20 Jean 7.46-7.49 Néhémie 8.3 Matthieu 22.15-22.16 Luc 22.2-22.4

Cette Bible est dans le domaine public.