Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 7.23
Bible en Swahili de l’est


Le cœur humain

1 Kisha Mafarisayo, na baadhi ya waandishi waliotoka Yerusalemu, wakakusanyika mbele yake,
Marc 3.22 Matthieu 15.1-15.20 Luc 5.17 Luc 11.53-11.54
2 wakaona wengine katika wanafunzi wake wakila vyakula kwa mikono najisi, yaani, isiyonawiwa.
Actes 10.28 Romains 14.14 Matthieu 7.3-7.5 Actes 11.8 Matthieu 23.23-23.25
3 Kwa maana Mafarisayo na Wayahudi wote wasiponawa mikono mpaka kiwiko, hawali, wakishika mapokeo ya wazee wao;
Galates 1.14 Marc 7.13 Colossiens 2.8 Colossiens 2.21-2.23 Marc 7.7-7.10
4 tena wakitoka sokoni, wasipotawadha, hawali; na yako mambo mengine waliyopokea kuyashika, kama kuosha vikombe, na midumu, na vyombo vya shaba.
Matthieu 23.25 Hébreux 9.10 Jacques 4.8 Esaïe 1.16 Jean 2.6
5 Basi wale Mafarisayo na waandishi wakamwuliza, Mbona wanafunzi wako hawaendi kwa kuyafuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?
Matthieu 15.2 Actes 21.21 2 Thessaloniciens 3.11 Marc 7.2-7.3 Actes 21.24
6 Akawaambia, Isaya alitabiri vema juu yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, Watu hawa huniheshimu kwa midomo Ila mioyo yao iko mbali nami;
Esaïe 29.13 Matthieu 15.7-15.9 Ezéchiel 33.31 Tite 1.16 Jacques 2.14-2.17
7 Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu,
Matthieu 6.7 Colossiens 2.22 Matthieu 15.9 Jacques 2.20 Deutéronome 12.32
8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.
Marc 7.3-7.4 Esaïe 1.12
9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.
Marc 7.13 Galates 2.21 Matthieu 15.3-15.6 Marc 7.3 2 Rois 16.10-16.16
10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.
Exode 20.12 Deutéronome 5.16 Exode 21.17 Lévitique 20.9 Marc 10.19
11 Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, Ni Korbani, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi;
Matthieu 23.18 1 Timothée 5.4-5.8 Matthieu 15.5
12 wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye;
13 huku mkilitangua neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyopokeana; tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo.
Marc 7.9 Tite 1.14 Osée 8.12 Matthieu 5.17-5.20 Ezéchiel 18.14
14 Akawaita makutano tena, akawaambia, Nisikieni nyote na kufahamu.
Matthieu 15.10 Psaumes 49.1-49.2 Proverbes 8.5 Psaumes 94.8 1 Rois 22.28
15 Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu.
Matthieu 12.34 Marc 7.18-7.23 Actes 11.8-11.10 Actes 10.28 Lévitique 11.42-11.47
16 Mtu akiwa na masikio ya kusikilia, na asikie.]
17 Hata alipoingia nyumbani, ameuacha mkutano, wanafunzi wake wakamwuliza habari za ule mfano.
Matthieu 15.15 Matthieu 13.36 Marc 9.28 Marc 4.10 Marc 4.34
18 Akawaambia, Hivi hata ninyi hamna akili? Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi;
Matthieu 15.16-15.17 Jérémie 5.4-5.5 1 Corinthiens 3.2 Marc 4.13 Matthieu 16.11
19 kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote.
1 Corinthiens 6.13 Actes 10.15 Luc 11.41 Colossiens 2.16 Matthieu 15.17
20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.
Marc 7.15 Jacques 3.6 Matthieu 12.34-12.37 Hébreux 7.6 Michée 2.1
21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,
Jacques 4.1-4.3 Jérémie 17.9 Galates 5.19-5.21 Romains 8.7-8.8 Actes 8.22
22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.
Matthieu 20.15 1 Pierre 5.5 1 Pierre 2.15 Proverbes 28.22 Proverbes 22.15
23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi.
Marc 7.15 Marc 7.18 Jude 1.8 Tite 1.15 1 Corinthiens 3.17

Jésus et la femme non juive

24 Akaondoka huko, akaenda zake hata mipaka ya Tiro na Sidoni. Akaingia katika nyumba, akataka isijulikane na mtu; lakini hakuweza kusitirika.
Matthieu 15.21-15.28 Matthieu 11.21 Marc 3.7-3.8 Marc 6.31-6.32 Ezéchiel 28.2
25 Ila mara mwanamke, ambaye binti yake yuna pepo mchafu, alisikia habari zake, akaja akamwangukia miguuni pake.
Matthieu 15.22 Marc 5.22-5.23 Apocalypse 22.8-22.9 Actes 10.25-10.26 Marc 9.17-9.23
26 Na yule mwanamke ni Myunani, kabila yake ni Msirofoinike. Akamwomba amtoe pepo katika binti yake.
Matthieu 15.22 Esaïe 49.12 Colossiens 3.11 Galates 3.28
27 Akamwambia, Waache watoto washibe kwanza; maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto, na kuwatupia mbwa.
Matthieu 7.6 Actes 22.21 Matthieu 15.23-15.28 Matthieu 10.5 Ephésiens 2.12
28 Naye akajibu, akamwambia, Naam, Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto.
Psaumes 145.16 Actes 11.17-11.18 Matthieu 5.45 Romains 15.8-15.9 Ephésiens 3.8
29 Akamwambia, Kwa sababu ya neno hilo, enenda zako, pepo amemtoka binti yako.
Esaïe 66.2 Matthieu 8.9-8.13 Matthieu 5.3 Esaïe 57.15-57.16 1 Jean 3.8
30 Akaenda zake nyumbani kwake, akamkuta yule kijana amelazwa kitandani, na yule pepo amekwisha kumtoka.
1 Jean 3.8 Jean 4.50-4.52
31 Akatoka tena katika mipaka ya Tiro, akapita katikati ya Sidoni, akaenda mpaka bahari ya Galilaya, kati ya mipaka ya Dekapoli.
Matthieu 4.25 Marc 5.20 Marc 7.24 Matthieu 15.29-15.31 Matthieu 11.21
32 Wakamletea kiziwi, naye ni mwenye utasi, wakamsihi amwekee mikono.
Luc 11.14 Marc 5.23 Matthieu 9.32-9.33
33 Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi,
Marc 8.23 Jean 9.6-9.7 Marc 5.40 1 Rois 17.19-17.22 2 Rois 4.4-4.6
34 akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka.
Marc 8.12 Marc 6.41 Jean 11.33 Jean 11.41 Jean 17.1
35 Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri.
Esaïe 35.5-35.6 Esaïe 32.3-32.4 Matthieu 11.5 Psaumes 33.9 Marc 2.12
36 Akawaonya wasimwambie mtu; lakini kadiri ya alivyozidi kuwaagiza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari;
Matthieu 8.4 Marc 5.43 Marc 1.44-1.45 Marc 8.26 Marc 3.12
37 wakashangaa mno kupita kiasi, wakinena, Ametenda mambo yote vema; viziwi awafanya wasikie, na bubu waseme.
Genèse 1.31 Actes 3.10-3.13 Marc 1.27 Actes 2.7-2.12 Marc 2.12

Cette Bible est dans le domaine public.