Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 6.30
Bible en Swahili de l’est


Les pratiques religieuses

1 Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni.
Matthieu 23.5 Hébreux 6.10 Galates 6.12 Jean 12.43 Matthieu 23.28-23.30
2 Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.
Matthieu 6.5 Matthieu 6.16 Actes 11.29 Matthieu 7.5 Osée 8.1
3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;
Jean 7.4 Marc 1.44 Matthieu 9.30
4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Jérémie 17.10 Matthieu 6.6 Matthieu 6.18 Psaumes 44.21 Jérémie 23.24
5 Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
Matthieu 6.2 Luc 18.10-18.11 Marc 11.25 Luc 18.1 Luc 14.12-14.14
6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
2 Rois 4.33 Esaïe 26.20 Esaïe 65.24 Psaumes 34.15 Matthieu 6.18
7 Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.
Ecclésiaste 5.2-5.3 Ecclésiaste 5.7 1 Rois 18.26-18.29 Matthieu 26.44 Matthieu 26.39
8 Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.
Matthieu 6.32 Psaumes 38.9 Luc 12.30 Philippiens 4.6 Jean 16.23-16.27
9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,
Ezéchiel 36.23 Luc 11.1-11.4 Malachie 1.11 Matthieu 7.11 Zacharie 14.9
10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.
1 Thessaloniciens 5.18 Matthieu 12.50 Matthieu 3.2 1 Pierre 2.15 Hébreux 10.36
11 Utupe leo riziki yetu.
Proverbes 30.8 Exode 16.16-16.35 Luc 11.3 Matthieu 4.4 1 Timothée 6.8
12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.
Marc 11.25 Ephésiens 4.32 1 Rois 8.39 Psaumes 32.1 Exode 34.7
13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]
1 Corinthiens 10.13 Jean 17.15 Matthieu 26.41 Jérémie 15.21 Matthieu 6.10
14 Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.
Ephésiens 4.32 Marc 11.25 Colossiens 3.13 Matthieu 7.2 Proverbes 21.13
15 Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
Matthieu 18.35
16 Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.
Esaïe 58.3-58.5 Matthieu 6.2 Luc 18.12 Matthieu 6.5 Psaumes 69.10
17 Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;
Ruth 3.3 2 Samuel 12.20 2 Samuel 14.2 Daniel 10.2-10.3 Ecclésiaste 9.8
18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Matthieu 6.4 Matthieu 6.6 2 Corinthiens 10.18 2 Corinthiens 5.9 Colossiens 3.22-3.24

Les biens matériels

19 Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba;
Hébreux 13.5 Jacques 5.1-5.3 1 Timothée 6.8-6.10 1 Jean 2.15-2.16 Luc 12.21
20 bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi;
Luc 12.33 Hébreux 11.26 Matthieu 19.21 1 Timothée 6.19 1 Pierre 1.4
21 kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.
Colossiens 3.1-3.3 Proverbes 4.23 Luc 12.34 Romains 7.5-7.7 2 Corinthiens 4.18
22 Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.
Luc 11.34-11.36 2 Corinthiens 11.3
23 Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo!
1 Corinthiens 1.18-1.20 Matthieu 6.22 Romains 2.17-2.23 Esaïe 5.20-5.21 Jérémie 4.22
24 Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
Luc 16.13 1 Jean 2.15-2.16 Jacques 4.4 1 Timothée 6.9-6.10 Galates 1.10
25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
Matthieu 6.31 Philippiens 4.6 Matthieu 6.34 1 Pierre 5.7 Matthieu 6.27-6.28
26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?
Psaumes 147.9 Job 38.41 Luc 12.24-12.32 Psaumes 104.27-104.28 Matthieu 10.29-10.31
27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?
Ecclésiaste 3.14 Luc 12.25-12.26 Matthieu 5.36 Psaumes 39.5-39.6 1 Corinthiens 12.18
28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti
Matthieu 6.31 Matthieu 6.25 Luc 12.27 Philippiens 4.6 Luc 22.35-22.36
29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.
2 Chroniques 9.20-9.22 2 Chroniques 9.4-9.6 1 Pierre 3.2-3.5 1 Timothée 2.9-2.10 1 Rois 10.4-10.7
30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?
Matthieu 16.8 Matthieu 14.31 Matthieu 8.26 Jacques 1.10-1.11 1 Pierre 1.24
31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?
1 Pierre 5.7 Psaumes 55.22 Luc 12.29 Psaumes 37.3 Matthieu 15.33
32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.
Matthieu 6.8 Luc 12.30 Ephésiens 4.17 Psaumes 17.14 Psaumes 103.13
33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
Matthieu 5.6 Luc 12.31 Jean 6.27 Marc 10.29-10.30 Psaumes 34.9-34.10
34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
Matthieu 6.25 Jean 14.27 Hébreux 13.5-13.6 Lamentations 3.23 Jean 16.33

Cette Bible est dans le domaine public.