Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 20.8
Bible en Swahili de l’est


1 Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.
Cantique 8.11-8.12 Matthieu 13.24 Matthieu 13.31 Matthieu 9.37-9.38 Matthieu 13.47
2 Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.
1 Rois 18.12 Deutéronome 5.27-5.30 1 Samuel 3.21 1 Rois 3.6-3.11 Apocalypse 6.6
3 Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;
1 Timothée 5.13 Actes 17.17-17.21 Matthieu 11.16-11.17 Actes 2.15 Ezéchiel 16.49
4 na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
1 Corinthiens 6.11 Tite 3.8 Matthieu 9.9 Romains 6.16-6.22 1 Pierre 1.13
5 Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.
Actes 3.1 Actes 10.9 Hébreux 11.24-11.26 Genèse 12.1-12.4 Luc 23.44-23.46
6 Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Jean 9.4 Ezéchiel 16.49 Hébreux 6.12 Proverbes 19.15 Actes 17.21
7 Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
Jean 9.4 Romains 16.25 Actes 4.16 Ephésiens 6.8 Actes 17.30-17.31
8 Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia msimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza.
Deutéronome 24.15 Lévitique 19.13 Luc 10.7 Matthieu 13.39-13.40 Matthieu 25.31
9 Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari.
Matthieu 20.2 Ephésiens 2.8-2.10 1 Timothée 1.14-1.16 Ephésiens 1.6-1.8 Romains 4.3-4.6
10 Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.
11 Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unikia mwenye nyumba,
Luc 5.30 Luc 19.7 Jude 1.16 Luc 15.2 Actes 22.21-22.22
12 wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa.
Luc 12.55 Jacques 1.11 Romains 9.30-9.32 Ephésiens 3.6 Zacharie 7.3-7.5
13 Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari?
Matthieu 26.50 Matthieu 22.12 Job 34.17-34.18 Job 35.2 Romains 9.14-9.15
14 Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.
Matthieu 6.2 Luc 15.31 2 Rois 10.16 Matthieu 6.16 Luc 16.25
15 Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema?
Deutéronome 15.9 Matthieu 6.23 Marc 7.22 Romains 9.15-9.24 Proverbes 23.6
16 Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.
Matthieu 19.30 Luc 14.24 Marc 10.31 Matthieu 7.13 Jacques 1.23-1.25

Demande de la mère de Jacques et de Jean

17 Hata Yesu alipokuwa akipanda kwenda Yerusalemu, aliwachukua wale wanafunzi kumi na wawili faraghani; na njiani akawaambia,
Marc 10.32-10.34 Genèse 18.17 Jean 15.15 Jean 12.12 Luc 18.31-18.34
18 Angalieni, tunapanda kwenda Yerusalemu; na Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi; nao watamhukumu afe;
Matthieu 16.21 Matthieu 27.1 Matthieu 26.66 Matthieu 26.2 Psaumes 2.1-2.3
19 kisha watampeleka kwa Mataifa wapate kumdhihaki, na kumpiga mijeledi, na kumsulibisha; na siku ya tatu atafufuka.
Matthieu 16.21 Marc 15.16-15.20 Actes 2.23 Matthieu 27.27-27.31 Luc 23.1-23.5
20 Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.
Matthieu 4.21 Matthieu 8.2 Matthieu 27.56 Marc 10.35-10.45 Marc 15.40
21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.
Matthieu 19.28 Marc 10.36-10.37 Matthieu 18.1 Esther 5.3 Psaumes 110.1
22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
Matthieu 26.42 Jean 18.11 Luc 22.42 Jacques 4.3 Esaïe 51.22
23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.
Apocalypse 1.9 Actes 12.2 Matthieu 25.34 1 Corinthiens 2.9 2 Timothée 2.11-2.12
24 Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili.
1 Pierre 5.5 1 Corinthiens 13.4 Luc 22.23-22.25 Jacques 4.5-4.6 Marc 10.41
25 Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
Luc 22.25-22.27 Matthieu 20.25-20.28 Jean 13.12-13.17 Matthieu 18.3-18.4 Daniel 3.2-3.7
26 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu;
Marc 10.43 Marc 9.35 Marc 10.45 1 Pierre 5.3 1 Pierre 4.11
27 na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu;
Marc 9.33-9.35 Luc 22.26 Romains 1.14 2 Corinthiens 4.5 2 Corinthiens 11.23-11.27
28 kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.
Luc 22.27 Hébreux 9.28 1 Pierre 1.18-1.19 Tite 2.14 1 Timothée 2.6

Guérison de deux aveugles

29 Hata walipokuwa wakitoka Yeriko mkutano mkubwa wakamfuata.
Marc 10.46-10.52 Luc 18.35-18.43 Matthieu 9.27-9.31
30 Na tazama, vipofu wawili wameketi kando ya njia, nao waliposikia ya kwamba Yesu anapita, walipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Bwana, mwana wa Daudi!
Matthieu 22.42 Matthieu 21.9 Luc 4.18 Esaïe 35.5-35.6 Psaumes 146.8
31 Mkutano wakawakaripia, wanyamaze. Lakini wao wakazidi kupaza sauti, wakisema, Uturehemu, Bwana, mwana wa Daudi!
Matthieu 19.13 Matthieu 15.23 Luc 11.8-11.10 Matthieu 7.7-7.8 Colossiens 4.2
32 Yesu akasimama, akawaita, akasema, Mnataka niwafanyie nini?
Ezéchiel 36.37 Philippiens 4.6 Matthieu 20.21 Actes 10.29
33 Wakamwambia, Bwana, twataka macho yetu yafumbuliwe.
Ephésiens 1.17-1.19 Psaumes 119.18
34 Yesu akawahurumia, akawagusa macho yao; mara wakapata kuona, wakamfuata.
Matthieu 14.14 Luc 22.51 Actes 26.18 Matthieu 15.32 Psaumes 119.71

Cette Bible est dans le domaine public.