Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 12.35
Bible en Swahili de l’est


Jésus et le sabbat

1 Wakati ule Yesu alipita katika mashamba siku ya sabato; wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kuvunja masuke, wakala.
Deutéronome 23.25 Marc 2.23-2.28 Luc 6.1-6.5
2 Na Mafarisayo walipoona, walimwambia, Tazama! Wanafunzi wako wanafanya neno ambalo si halali kulifanya siku ya sabato.
Matthieu 12.10 Luc 14.3 Exode 20.9-20.11 Exode 31.15-31.17 Esaïe 58.13
3 Akawaambia, Hamkusoma alivyotenda Daudi, alipokuwa na njaa, yeye na wenziwe?
1 Samuel 21.3-21.6 Luc 6.3 Marc 2.25-2.26 Marc 12.26 Matthieu 21.16
4 jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, akaila mikate ile ya wonyesho, ambayo si halali kwake kuila wala kwa wale wenziwe, ila kwa makuhani peke yao?
Exode 25.30 Lévitique 24.5-24.9 Lévitique 8.31 Exode 29.32-29.33
5 Wala hamkusoma katika torati, kwamba siku ya sabato makuhani hekaluni huinajisi sabato wasipate hatia?
Nombres 28.9-28.10 Jean 7.22-7.23 Ezéchiel 24.21
6 Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.
Matthieu 12.41-12.42 2 Chroniques 6.18 Malachie 3.1 1 Pierre 2.4-2.5 Colossiens 2.9
7 Lakini kama mngalijua maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka, msingaliwalaumu wasio na hatia.
Matthieu 9.13 Osée 6.6 Michée 6.6-6.8 Psaumes 94.21 Jacques 5.6
8 Kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.
Marc 2.28 Matthieu 9.6 Luc 6.5 1 Corinthiens 16.2 1 Corinthiens 9.21
9 Akaondoka huko, akaingia katika sinagogi lao.
Luc 6.6-6.11 Marc 3.1-3.6
10 Na tazama, yumo mtu mwenye mkono umepooza; wakamwuliza, wakisema, Ni halali kuponya watu siku ya sabato? Wapate kumshitaki.
Luc 13.14 Jean 9.16 Matthieu 12.2 Jean 8.6 Zacharie 11.17
11 Akawaambia, Ni mtu yupi miongoni mwenu mwenye kondoo mmoja, na yule kondoo ametumbukia shimoni siku ya sabato, asiyemshika akamwopoa?
Luc 14.5 Deutéronome 22.4 Exode 23.4-23.5 Luc 13.15-13.17
12 Je! Mtu ni bora kuliko kondoo mara ngapi? Basi ni halali kutenda mema siku ya sabato.
Matthieu 6.26 Luc 12.24 Marc 3.4 Matthieu 10.31 Luc 6.9
13 Kisha akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako; akaunyosha, ukapona, ukawa mzima kama wa pili.
Actes 3.7-3.8 Luc 13.13

Jésus, le serviteur de l’Éternel contesté

14 Lakini wale Mafarisayo wakatoka wakafanya shauri juu yake jinsi ya kumwangamiza.
Jean 11.53 Jean 10.39 Marc 3.6 Jean 5.18 Luc 6.11
15 Naye Yesu hali akiyafahamu hayo akaondoka huko; na watu wengi wakamfuata; akawaponya wote,
Matthieu 19.2 Matthieu 10.23 Marc 3.7-3.12 Luc 6.12 1 Pierre 2.21
16 akawakataza wasimdhihirishe;
Matthieu 17.9 Matthieu 8.4 Matthieu 9.30 Luc 5.14-5.15 Marc 7.36
17 ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema,
Esaïe 42.1-42.4 Esaïe 42.9 Jean 19.28 Esaïe 44.26 Jean 12.38
18 Tazama, mtumishi wangu niliyemteua; Mpendwa wangu, moyo wangu uliyependezwa naye; Nitatia roho yangu juu yake, Naye atawatangazia Mataifa hukumu.
Luc 4.18 Jean 3.34 Esaïe 42.1 Esaïe 49.5-49.6 Esaïe 32.15-32.16
19 Hatateta wala hatapaza sauti yake; Wala mtu hatasikia sauti yake njiani.
Jean 18.36-18.38 2 Timothée 2.24-2.25 Luc 17.20 2 Corinthiens 10.1 Zacharie 9.9
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, Wala utambi utokao moshi hatauzima, Hata ailetapo hukumu ikashinda.
Esaïe 42.3-42.4 Luc 4.18 Esaïe 61.1-61.3 Psaumes 147.3 Hébreux 12.12-12.13
21 Na jina lake Mataifa watalitumainia.
Esaïe 11.10 Ephésiens 1.12-1.13 Esaïe 42.4 Colossiens 1.27 Romains 15.12-15.13
22 Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.
Esaïe 35.5-35.6 Esaïe 29.18 Actes 26.18 Marc 7.35-7.37 Matthieu 9.32-9.34
23 Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi?
Matthieu 9.27 Matthieu 22.42-22.43 Matthieu 21.9 Jean 7.40-7.42 Jean 4.29
24 Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo.
Matthieu 9.34 Marc 3.22 Luc 11.15
25 Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.
Matthieu 9.4 Jérémie 17.10 Galates 5.15 Hébreux 4.13 Psaumes 139.2
26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?
Colossiens 1.13 1 Jean 5.19 2 Corinthiens 4.4 Jean 12.31 Apocalypse 12.9
27 Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu.
Luc 11.19 Marc 9.38-9.39 Luc 9.49-9.50 Actes 19.13-19.16 Matthieu 12.41-12.42
28 Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia.
Luc 11.20 Matthieu 21.31 Colossiens 1.13 Matthieu 12.18 Matthieu 21.43
29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake.
Marc 3.27 Esaïe 53.12 Esaïe 49.24 Apocalypse 20.7-20.9 1 Jean 4.4
30 Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.
Luc 11.23 Marc 9.40 Luc 9.50 1 Jean 2.19 2 Corinthiens 6.15-6.16
31 Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa.
Luc 12.10 Marc 3.28-3.30 Hébreux 10.26 Hébreux 6.4 1 Jean 5.16
32 Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.
Marc 3.29 Matthieu 11.19 Ephésiens 1.21 Hébreux 6.4-6.6 1 Timothée 1.13
33 Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri; au ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana.
Luc 6.43-6.44 Matthieu 7.16-7.20 Amos 5.15 Jacques 4.8 Ezéchiel 18.31
34 Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake.
Luc 6.45 Matthieu 15.18 Ephésiens 4.29 Jacques 3.5-3.8 1 Samuel 24.13
35 Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.
Colossiens 4.6 Proverbes 10.20-10.21 Matthieu 13.52 Colossiens 3.16 Proverbes 25.11-25.12
36 Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
Ecclésiaste 12.14 Jude 1.14-1.15 Apocalypse 20.12 Romains 2.16
37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.
Proverbes 13.3 Jacques 2.21-2.25
38 Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.
1 Corinthiens 1.22 Jean 2.18 Marc 8.11-8.12 Luc 11.16 Jean 4.48
39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.
Matthieu 16.4 Luc 11.29-11.32 Marc 8.38 Esaïe 57.3 Jacques 4.4
40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.
Jonas 1.17 Matthieu 16.21 Matthieu 17.23 Matthieu 8.20 Matthieu 27.63-27.64
41 Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona.
Matthieu 12.42 Hébreux 11.7 Matthieu 12.6 Romains 2.27 Esaïe 54.17
42 Malkia wa kusini atasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, naye atawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu yeye alikuja kutoka pande za mwisho za dunia ili asikie hekima ya Sulemani, na hapa yupo aliye mkuu kuliko Sulemani.
Hébreux 1.2-1.4 2 Chroniques 9.1-9.12 1 Rois 10.1-10.13 Matthieu 12.41 Jean 1.18
43 Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.
Psaumes 63.1 Esaïe 41.18 Esaïe 35.6-35.7 Ezéchiel 47.8-47.12 1 Pierre 5.8
44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.
Apocalypse 13.3-13.4 1 Jean 4.4 Osée 7.6 Apocalypse 13.8-13.9 Jean 13.2
45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.
Hébreux 6.4-6.8 Marc 5.9 Luc 11.26 Hébreux 10.26-10.31 Hébreux 10.39
46 Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye.
Actes 1.14 Galates 1.19 Jean 2.12 Matthieu 13.55 Marc 6.3
47 Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.
48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani?
Deutéronome 33.9 2 Corinthiens 5.16 Matthieu 10.37 Marc 3.32-3.33 Luc 2.49
49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!
Jean 20.17-20.20 Jean 17.8-17.9 Matthieu 28.7 Marc 3.34 Jean 17.20
50 Kwa maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu.
Jean 15.14 Marc 3.35 Hébreux 2.11-2.17 1 Timothée 5.2 1 Jean 2.17

Cette Bible est dans le domaine public.