Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 24.3
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Balaamu alipoona ya kuwa ilimpendeza Bwana kuwabariki Israeli, hakwenda, kama hapo kwanza, ili kutafuta uchawi, bali alielekeza uso wake jangwani.
Nombres 23.23 Nombres 23.15 Nombres 23.3 Nombres 23.20 1 Samuel 26.25
2 Balaamu akainua macho yake akawaona Israeli wamekaa kabila kabila; roho ya Mungu ikamjia.
1 Samuel 19.20 2 Chroniques 15.1 1 Samuel 10.10 1 Samuel 19.23 Matthieu 10.8
3 Akatunga mithali yake, akasema, Balaamu mwana wa Beori asema, Yule mtu aliyefumbwa macho asema;
Nombres 23.7 Nombres 24.16 Nombres 23.18 Nombres 24.4 Nombres 22.31
4 Asema, yeye asikiaye maneno ya Mungu, Yeye aonaye maono ya Mwenyezi, Akianguka kifudifudi, amefumbuliwa macho;
Apocalypse 1.17 Nombres 12.6 Ezéchiel 1.28 Apocalypse 1.10 2 Corinthiens 12.1-12.4
5 Mahema yako ni mazuri namna gani, Ee Yakobo, Maskani zako, Ee Israeli!
6 Mfano wa bonde zimetandwa, Mfano wa bustani kando ya mto, Mfano wa mishubiri aliyoipanda Bwana, Mfano wa mierezi kando ya maji.
Psaumes 1.3 Psaumes 104.16 Esaïe 58.11 Genèse 13.10 Ezéchiel 47.12
7 Maji yatafurika katika ndoo zake, Na mbegu zake zitakuwa katika maji mengi. Na mfalme wake ataadhimishwa kuliko Agagi, Na ufalme wake utatukuzwa.
2 Samuel 5.12 1 Chroniques 14.2 Apocalypse 17.1 Jérémie 51.13 Psaumes 145.11-145.13
8 Mungu amemleta kutoka Misri, Ana nguvu mfano wa nguvu za nyati; Atawameza mataifa walio adui zake, Ataivunja mifupa yao vipande vipande. Atawachoma kwa mishale yake.
Psaumes 45.5 Nombres 23.22 Nombres 23.24 Psaumes 2.9 Jérémie 50.17
9 Aliinama, akalala mfano wa simba, Na kama simba mke; ni nani atakayemstusha? Na abarikiwe kila akubarikiye, Na alaaniwe kila akulaaniye.
Genèse 49.9 Nombres 23.24 Genèse 12.3 Genèse 27.29 Matthieu 25.45
10 Hasira ya Balaki ikawaka juu ya Balaamu akayapiga makofi; Balaki akamwambia Balaamu, Nalikuita ili unilaanie adui zangu, na tazama, umewabariki kabisa mara tatu hizi.
Nombres 23.11 Ezéchiel 21.14 Ezéchiel 22.13 Ezéchiel 21.17 Néhémie 13.2
11 Basi sasa kimbilia mahali pako; naliazimu kukuheshimu sana; lakini, tazama, Bwana amekuzuilia heshima.
Nombres 22.17 Nombres 22.37 Actes 8.20 Hébreux 11.24-11.26 1 Pierre 5.2-5.3
12 Balaamu akamwambia Balaki, Je! Sikuwaambia wajumbe wako ulionipelekea, nikisema,
Nombres 22.18 Nombres 22.38
13 Kama Balaki angenipa nyumba yake imejaa fedha na dhahabu, siwezi kupita mpaka wa neno la Bwana, kutenda neno jema, wala neno baya, kwa nia yangu mwenyewe; Bwana atakalolinena ndilo nitakalolinena mimi.
Nombres 22.20 Nombres 22.18 Nombres 16.28
14 Basi sasa, tazama, ninakwenda kwa watu wangu; haya, nitakuarifu mambo ambayo watu hawa watakayowatenda watu wako siku za mwisho.
Genèse 49.1 Michée 6.5 Daniel 2.28 Apocalypse 2.14 Jérémie 48.47
15 Akatunga mithali yake akasema, Balaamu mwana wa Beori asema, Yule mtu aliyefumbwa macho asema,
Nombres 23.7 Nombres 24.3-24.4 Nombres 23.18 Job 27.1 Matthieu 13.35
16 Asema, yeye asikiaye maneno ya Mungu, Na kuyajua maarifa yake Aliye Juu. Yeye aonaye maono ya Mwenyezi, Akianguka kifudifudi, amefumbuliwa macho,
Nombres 24.4 1 Corinthiens 13.2 2 Samuel 23.1-23.2 1 Corinthiens 8.1
17 Namwona, lakini si sasa; Namtazama, lakini si karibu; Nyota itatokea katika Yakobo Na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli; Nayo itazipiga-piga pembe za Moabu, Na kuwavunja-vunja wana wote wa ghasia.
Genèse 49.10 Apocalypse 22.16 Apocalypse 1.7 Zacharie 10.4 Esaïe 9.7
18 Na Edomu itakuwa milki Seiri pia itakuwa milki, waliokuwa adui zake; Israeli watakapotenda kwa ushujaa.
Amos 9.12 2 Samuel 8.14 Genèse 27.29 Genèse 32.3 Psaumes 60.8-60.12
19 Mwenye kutawala atakuja toka Yakobo, Atawaangamiza watakaobaki mjini.
Michée 5.2 Genèse 49.10 Luc 19.27 Psaumes 72.10-72.11 Apocalypse 19.16
20 Kisha akamwangalia Amaleki, akatunga mithali yake, akasema, Amaleki alikuwa ni wa kwanza wa mataifa; Lakini mwisho wake atafikilia uharibifu.
Exode 17.14 Esther 9.14 1 Chroniques 4.43 Exode 17.16 Esther 3.1
21 Kisha akamwangalia Mkeni, akatunga mithali yake, akasema, Makao yako yana nguvu, Na kitundu chako kimewekwa katika jabali.
Genèse 15.19 Juges 1.16 Job 29.18
22 Pamoja na haya Wakeni wataangamizwa, Hata Ashuru atakapokuchukua mateka.
Esdras 4.2 Osée 14.3 Psaumes 83.8 Genèse 10.22 Genèse 10.11
23 Akatunga mithali yake akasema, Ole wao! Ni nani atakayepona, Mungu atakapofanya haya?
Malachie 3.2 Nombres 23.23 2 Rois 5.1
24 Lakini merikebu zitakuja kutoka pwani kwa Kitimu, Nazo zitamtaabisha Ashuru, na Eberi zitamtaabisha, Yeye naye atafikilia uharibifu.
Genèse 10.4 Nombres 24.20 Daniel 11.30 Daniel 7.19-7.20 Daniel 11.45
25 Basi Balaamu akainuka, akaondoka na kurudi mahali pake; Balaki naye akaenda zake.
Nombres 31.8 Josué 13.22 Nombres 24.11

Cette Bible est dans le domaine public.