Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 15.28
Bible en Swahili de l’est


L’état d’impureté de l’homme et de la femme

1 Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
Lévitique 13.1 Lévitique 11.1 Psaumes 25.14 Hébreux 1.1 Amos 3.7
2 Haya, semeni na wana wa Israeli, mkawaambie, Mtu ye yote atakapokuwa na kisonono kimtokacho mwilini mwake, atakuwa najisi kwa ajili ya kisonono chake.
2 Samuel 3.29 Lévitique 22.4 Nombres 5.2 Matthieu 9.20 Luc 8.43
3 Na unajisi wake katika kisonono chake ni huu; kama mwili wake unachuruzika kisonono chake, au kama kisonono chake kimezuiwa mwilini mwake, ni unajisi wake.
Lévitique 12.3 Ezéchiel 16.26 Ezéchiel 23.20
4 Kitanda cho chote akilaliacho mwenye kisonono kitakuwa najisi; na kitu cho chote ambacho akiketia kitakuwa najisi.
1 Corinthiens 15.33 Tite 1.15 Ephésiens 5.11
5 Mtu ye yote atakayekigusa kitanda chake huyo, atazifua nguo zake, na kuoga mwili wake majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
Lévitique 11.25 Lévitique 17.15 Lévitique 16.26 Hébreux 9.14 Nombres 19.22
6 Na mtu atakayeketi katika kitu cho chote alichokiketia mwenye kisonono, atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
Jacques 4.8 Esaïe 1.16
7 Na mtu atakayegusa mwili wake mwenye kisonono atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
8 Tena kama mwenye kisonono akimtemea mate mtu aliye safi; ndipo atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa yu najisi hata jioni.
Jude 1.4 Tite 1.9-1.10 1 Timothée 4.1-4.3 Esaïe 1.16 2 Pierre 2.1-2.3
9 Na tandiko lo lote atakalolipanda mwenye kisonono litakuwa najisi.
Genèse 31.34
10 Mtu awaye yote atakayegusa kitu cho chote kilichokuwa chini yake huyo atakuwa najisi hata jioni; na mtu atakayevichukua vitu vile atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
Lévitique 15.8 Jacques 4.8 Psaumes 26.6 Lévitique 15.5
11 Na mtu ye yote atakayeguswa na mwenye kisonono, asipokuwa amenawa mikono yake majini, atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
12 Na chombo cha udongo ambacho amekigusa mwenye kisonono, kitavunjwa-vunjwa; na kila chombo cha mti kitaoshwa majini.
Lévitique 6.28 Lévitique 11.32-11.33 Philippiens 3.21 Proverbes 3.21 Proverbes 1.23
13 Na huyo aliye na kisonono atakapotakaswa na kisonono chake, atajihesabia siku saba kwa kutakaswa kwake, naye atazifua nguo zake; naye ataoga mwili wake katika maji ya mtoni, naye atakuwa safi.
Lévitique 14.8 Lévitique 8.33 Lévitique 15.28 Lévitique 15.5 Jacques 4.8
14 Na siku ya nane atajipatia hua wawili, au makinda mawili ya njiwa, naye atakwenda mbele za Bwana mlangoni pa hema ya kukutania, naye atampa kuhani hao ndege;
Lévitique 12.8 Lévitique 1.14 Nombres 6.10 Lévitique 15.29-15.30 Hébreux 7.26
15 na kuhani atawasongeza, mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa; naye kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya kisonono chake.
Lévitique 4.26 Lévitique 14.30-14.31 Lévitique 12.7 Nombres 25.13 Nombres 15.25
16 Na mtu ye yote akitokwa na shahawa yake, ndipo ataoga mwili wake wote majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
Lévitique 22.4 Deutéronome 23.10-23.11 Lévitique 15.5 1 Jean 1.7 2 Corinthiens 7.1
17 Na kila nguo, na kila ngozi, ambayo ina shahawa, itafuliwa kwa maji, nayo itakuwa najisi hata jioni.
18 Huyo mwanamke naye ambaye mtu mume amelala naye kwa shahawa, wote wawili wataoga majini, nao watakuwa najisi hata jioni.
2 Timothée 2.22 1 Thessaloniciens 4.3-4.5 Psaumes 51.5 1 Pierre 2.11 1 Samuel 21.4-21.5
19 Mwanamke ye yote, kama anatokwa na kitu, na kitu chake alichokuwa nacho mwilini mwake ni damu, ataketi katika kutengwa kwake muda wa siku saba; na mtu ye yote atakayemgusa atakuwa najisi hata jioni.
Lévitique 12.2 Matthieu 15.19 Ezéchiel 36.17 Marc 5.25 Lamentations 1.8-1.9
20 Na kitu cho chote akilaliacho katika kutengwa kwake kitakuwa najisi; na kila kitu ambacho akiketia kitakuwa najisi.
Lévitique 15.4-15.9 Proverbes 22.27 1 Corinthiens 15.33 Proverbes 5.3-5.13 Proverbes 9.13-9.18
21 Mtu ye yote atakayekigusa kitanda chake huyo mwanamke atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
Hébreux 9.26 2 Corinthiens 7.1 Apocalypse 7.14 Esaïe 22.14 Lévitique 15.5-15.6
22 Mtu ye yote atakayekigusa cho chote ambacho huyo mwanamke amekiketia atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
23 Kwamba ni katika kitanda, au cho chote alichokikalia huyo mwanamke, atakapokigusa kitu hicho, atakuwa najisi hata jioni.
24 Na mtu ye yote atakayelala na mwanamke na unajisi ukawa juu yake, atakuwa najisi muda wa siku saba; na kila kitanda alichokilalia kitakuwa najisi.
Lévitique 20.18 Lévitique 18.19 Ezéchiel 18.6 1 Pierre 2.11 Ezéchiel 22.10
25 Na mwanamke kama akitokwa na damu yake siku nyingi, nayo si katika majira ya kutengwa kwake, au kama anatoka damu kuzidi majira ya kutengwa kwake; siku hizo zote za kutoka damu ya unajisi wake, atakuwa kama alivyokuwa katika siku za kutengwa kwake; yeye yu najisi.
Marc 5.25 Matthieu 9.20 Luc 8.43 Marc 7.20-7.23 Lévitique 15.19-15.24
26 Kila kitanda akilaliacho katika siku zote za kutoka damu kitakuwa kama kitanda cha kutengwa kwake; na kila kitu atakachokilalia kitakuwa najisi, kama unajisi wa kutengwa kwake.
27 Na mtu ye yote atakayevigusa vitu vile atakuwa najisi, naye atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
Hébreux 10.22 Zacharie 13.1 Lévitique 15.21 Lévitique 15.13 Hébreux 9.14
28 Lakini huyo mwanamke kwamba ametakaswa na kule kutoka damu kwake, ndipo atakapojihesabia siku saba, na baadaye atakuwa safi.
Lévitique 15.13-15.15 Matthieu 1.21 1 Corinthiens 6.11 Galates 3.13 Ephésiens 1.6-1.7
29 Siku ya nane atajipatia hua wawili, au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani, mlangoni pa hema ya kukutania.
30 Kuhani atamsongeza mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, kwa ajili ya kutoka damu ya unajisi kwake.
31 Ni hivi mtakavyowatenga wana wa Israeli na unajisi wao; ili wasife katika unajisi wao, hapo watakapoitia unajisi maskani yangu iliyo katikati yao.
Nombres 5.3 Ezéchiel 5.11 Nombres 19.13 Nombres 19.20 Ezéchiel 23.38
32 Hii ndiyo sheria ya mwenye kisonono, na ya mtu ambaye shahawa yake yamtoka, akawa na unajisi kwa hiyo;
Lévitique 11.46 Nombres 5.29 Lévitique 13.59 Lévitique 14.54-15.18 Lévitique 14.2
33 na ya mwanamke ambaye yu katika kutengwa kwake, na ya mtu ambaye ana kisonono, kama ni mtu mume, kama ni mtu mke, na ya huyo alalaye na mwanamke mwenye unajisi.
Lévitique 15.24-15.25 Lévitique 20.18 Lévitique 15.19

Cette Bible est dans le domaine public.