Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 43.24
Bible en Swahili de l’est


La gloire de l’Éternel dans le temple

1 Kisha akanileta mpaka langoni, yaani, lango lile lielekealo upande wa mashariki;
Ezéchiel 42.15 Ezéchiel 44.1 Ezéchiel 40.6 Ezéchiel 46.1 Ezéchiel 10.19
2 na tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulitokea kwa njia ya mashariki; na sauti yake ilikuwa kama mshindo wa maji mengi, nayo nchi iling’aa kwa utukufu wake.
Ezéchiel 10.18-10.19 Apocalypse 18.1 Ezéchiel 11.23 Apocalypse 1.15 Esaïe 6.3
3 Na maono niliyoyaona yalikuwa kama maono niliyoyaona nilipokuja kuuharibu mji; nayo maono niliyoyaona yalikuwa kama maono niliyoyaona karibu na mto wa Kebari; nikaanguka kifudifudi.
Ezéchiel 9.1 Ezéchiel 9.5 Ezéchiel 3.23 Ezéchiel 1.3-1.28 Ezéchiel 32.18
4 Na huo utukufu wa Bwana ukaingia ndani ya nyumba, kwa njia ya lango lile lielekealo upande wa mashariki.
Ezéchiel 44.2 Ezéchiel 43.2 Ezéchiel 10.18-10.19
5 Kisha Roho ikaniinua, ikanichukua mpaka ua wa ndani; na tazama, utukufu wa Bwana uliijaza nyumba.
Ezéchiel 8.3 Ezéchiel 11.24 2 Corinthiens 12.2-12.4 Ezéchiel 44.4 1 Rois 8.10-8.11
6 Nikasikia sauti ya mmoja asemaye nami, itokayo katika nyumba hiyo; na mtu akasimama karibu nami.
Ezéchiel 40.3 Lévitique 1.1 Esaïe 66.6 Apocalypse 16.1
7 Akaniambia, Mwanadamu, hapa ni mahali pa kiti changu cha enzi, na mahali pa nyayo za miguu yangu, nitakapokaa kati ya wana wa Israeli milele; na nyumba ya Israeli hawatalinajisi jina langu takatifu tena, wao, wala wafalme wao, kwa mambo yao ya kikahaba, na kwa mizoga ya wafalme wao, katika mahali pao pa juu;
Lévitique 26.30 Ezéchiel 43.9 Psaumes 47.8 Ezéchiel 1.26 Psaumes 99.1
8 kwa kuweka kizingiti chao karibu na kizingiti changu; na mwimo wao karibu na mwimo wangu; tena palikuwa na ukuta tu kati ya mimi na wao; nao wamelinajisi jina langu takatifu kwa machukizo yao waliyoyatenda; basi, kwa sababu hiyo, nimewakomesha katika hasira yangu.
Ezéchiel 5.11 Ezéchiel 8.3-8.16 2 Rois 21.4-21.7 Ezéchiel 23.39 2 Chroniques 33.7
9 Basi sasa wayaondoe mambo yao ya kikahaba, na mizoga ya wafalme wao, yawe mbali nami, nami nitakaa kati yao milele.
Ezéchiel 43.7 Ezéchiel 18.30-18.31 Ezéchiel 37.26-37.28 Colossiens 3.5-3.9 Ezéchiel 37.23
10 Na wewe, mwanadamu, waonyeshe wana wa Israeli nyumba hii, ili wayatahayarikie maovu yao; na waipime hesabu yake.
Ezéchiel 40.4 Ezéchiel 16.61 Ezéchiel 43.11 Ezéchiel 16.63 1 Chroniques 28.19
11 Na ikiwa wameyatahayarikia yote waliyoyatenda, waonyeshe umbo la nyumba, na namna yake, na matokeo yake, na maingilio yake, na maumbo yake yote, na maagizo yake yote, na kawaida zake zote, na sheria zake zote, ukayaandike machoni pao; ili walishike umbo lake lote, na maagizo yake, na kuyatenda.
Ezéchiel 11.20 Ezéchiel 36.27 Ezéchiel 44.5-44.6 Ezéchiel 12.3 Ezéchiel 40.1-40.42
12 Hii ndiyo sheria ya nyumba; juu ya kilele cha mlima, mpaka wake wote pande zote patakuwa patakatifu sana. Tazama, hii ndiyo sheria ya nyumba.
Ezéchiel 40.2 Ezéchiel 42.20 Apocalypse 21.27 Psaumes 93.5 Zacharie 14.20-14.21

L’autel des sacrifices et les offrandes

13 Na vipimo vya madhabahu kwa dhiraa ni hivi; (dhiraa ni dhiraa na shubiri); tako lake ni dhiraa moja, na upana wake dhiraa moja; na pambizo yake karibu na ncha yake pande zote, shubiri moja; na hili litakuwa tako la madhabahu.
Exode 27.1-27.8 Ezéchiel 40.5 Ezéchiel 41.8 2 Chroniques 4.1
14 Tena toka chini, juu ya nchi, hata daraja ya chini, dhiraa mbili, na upana wake dhiraa moja; tena toka daraja ndogo hata daraja kubwa, dhiraa nne, na upana wake dhiraa moja.
15 Na madhabahu ya juu itakuwa dhiraa nne; na toka madhabahu pawashwapo moto na kwenda juu zitakuwa pembe nne.
Exode 27.2 Lévitique 9.9 Psaumes 118.27 1 Rois 2.28 Esaïe 29.1-29.2
16 Na pale pawashwapo moto, urefu wake dhiraa kumi na mbili, na upana wake kumi na mbili, mraba pande zake nne.
Exode 27.1 Esdras 3.3 Exode 38.1-38.2 2 Chroniques 4.1
17 Na daraja, urefu wake dhiraa kumi na nne, na upana wake dhiraa kumi na nne, pande zake nne; na pambizo yake nusu dhiraa; na tako lake dhiraa moja, kote kote, na madaraja yake yataelekea upande wa mashariki.
Exode 20.26 Ezéchiel 40.6 Néhémie 9.4 1 Rois 6.8 Ezéchiel 8.16
18 Kisha akaniambia, Mwanadamu, Bwana MUNGU asema hivi; Hizi ndizo sheria za madhabahu katika siku ile watakapoifanya, ili watoe sadaka za kuteketezwa juu yake, na kunyunyiza damu juu yake.
Exode 40.29 Lévitique 1.5-1.17 Lévitique 16.19 Hébreux 9.13 Ezéchiel 2.1
19 Utawapa makuhani Walawi, walio wa uzao wa Sadoki, walio karibu nami, ili kunihudumu, asema Bwana MUNGU, ng’ombe mume mchanga awe sadaka ya dhambi.
Ezéchiel 40.46 Ezéchiel 44.15 Nombres 16.40 Ezéchiel 45.18-45.19 Hébreux 7.27
20 Nawe utatwaa baadhi ya damu yake, na kuitia juu ya pembe zake nne, na juu ya ncha nne za daraja, na juu ya pambizo yake pande zote; ndivyo utakavyoitakasa, na kuifanyia upatanisho.
Lévitique 16.19 Lévitique 8.15 Lévitique 9.9 Ezéchiel 43.22 Exode 29.12
21 Tena utamtwaa ng’ombe wa sadaka ya dhambi, naye utamteketeza mahali palipoamriwa pa nyumba ile, nje ya mahali patakatifu.
Exode 29.14 Lévitique 4.12 Hébreux 13.11-13.12 Lévitique 8.17
22 Na siku ya pili utamtoa beberu mkamilifu awe sadaka ya dhambi; nao wataisafisha madhabahu, kama walivyoisafisha kwa ng’ombe huyo.
Ezéchiel 43.20 Ezéchiel 43.25-43.26 Esaïe 53.10 Exode 29.15-29.18 1 Pierre 1.19
23 Utakapokwisha kuitakasa, utatoa ng’ombe mume mchanga mkamilifu, na kondoo mume wa kundini mkamilifu.
Exode 29.1
24 Nawe utawaleta karibu mbele za Bwana, na makuhani watamwaga chumvi juu yao, nao watawatoa wawe sadaka za kuteketezwa kwa Bwana.
Lévitique 2.13 Marc 9.49-9.50 Nombres 18.19 Colossiens 4.6 2 Chroniques 13.5
25 Kwa muda wa siku saba utaweka tayari mbuzi kila siku awe sadaka ya dhambi; pia wataweka tayari ng’ombe mume mchanga, na kondoo mume wa kundini, wakamilifu.
Lévitique 8.33 Exode 29.35-29.37 Lévitique 8.35
26 Kwa muda wa siku saba wataifanyia madhabahu upatanisho, na kuitakasa; ndivyo watakavyoiweka wakfu.
Exode 32.29 Lévitique 8.34 Exode 29.24
27 Nao watakapozitimiza siku hizo, itakuwa, siku ya nane na baadaye, makuhani watatoa sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu, na sadaka zenu za amani nami nitawakubali ninyi, asema Bwana MUNGU.
Lévitique 9.1 Colossiens 1.20-1.21 Romains 12.1 Philippiens 2.17 1 Pierre 2.5

Cette Bible est dans le domaine public.