Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 16.1
Bible en Swahili de l’est


Jérusalem comparée à une prostituée

1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Mwanadamu, uujulishe Yerusalemu machukizo yake,
Ezéchiel 22.2 Ezéchiel 20.4 Esaïe 58.1 Osée 8.1 Ezéchiel 8.9-8.17
3 useme, Bwana MUNGU auambia Yerusalemu hivi; Asili yako na kuzaliwa kwako kwatoka katika nchi ya Mkanaani; Mwamori alikuwa baba yako, na mama yako alikuwa Mhiti.
Ezéchiel 16.45 Ezéchiel 21.30 Genèse 15.16 Ephésiens 2.3 Deutéronome 7.1
4 Na katika habari za kuzaliwa kwako, siku ile uliyozaliwa, kitovu chako hakikukatwa, wala hukuoshwa kwa maji usafishwe; hukutiwa chumvi hata kidogo, wala hukutiwa katika nguo kabisa.
Osée 2.3 Deutéronome 15.15 Lamentations 2.22 Ezéchiel 20.13 Josué 24.2
5 Hapana jicho lililokuhurumia, ili kukutendea lo lote la mambo hayo kwa kukuhurumia; lakini ulitupwa nje uwandani, kwa kuwa nafsi yako ilichukiwa, katika siku ile uliyozaliwa.
Exode 1.22 Ezéchiel 2.6 Lamentations 2.19 Jérémie 22.19 Deutéronome 32.10
6 Nami nilipopita karibu nawe, nikakuona ukigaagaa katika damu yako, nalikuambia, Ujapokuwa katika damu yako, uwe hai; naam, nalikuambia, Ujapokuwa katika damu yako, uwe hai.
Jean 5.25 Tite 3.3-3.7 Ephésiens 2.4-2.5 Actes 7.34 Hébreux 10.29
7 Nalikufanya kuwa maelfu-elfu, kama mimea ya mashamba, ukaongezeka, na kuzidi kuwa mkubwa, ukapata kuwa na uzuri mno; matiti yako yakaumbwa, nywele zako zikawa zimeota; lakini ulikuwa uchi, huna nguo.
Exode 1.7 Deutéronome 1.10 Ezéchiel 16.22 Job 1.21 Cantique 4.5
8 Basi, nilipopita karibu nawe, nikakutazama; tazama, wakati wako ulikuwa wakati wa upendo; nikatandika upindo wa vazi langu juu yako, nikakufunika uchi wako; naam, nalikuapia, nikafanya agano nawe, asema Bwana MUNGU, ukawa wangu.
Ruth 3.9 Exode 19.4-19.8 Esaïe 43.4 Jérémie 2.2-2.3 Romains 5.8
9 Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nalikuosha kabisa damu yako, nikakupaka mafuta;
Ruth 3.3 Psaumes 23.5 1 Corinthiens 10.2 Hébreux 9.10-9.14 Esaïe 4.4
10 nikakuvika nguo ya taraza, nikakupa viatu vya ngozi ya pomboo, nikakufunga nguo ya kitani safi kiunoni mwako, nikakufunika kwa hariri.
Ezéchiel 16.18 Ezéchiel 16.13 Exode 26.36 Ezéchiel 27.16 Esaïe 61.10
11 Nikakupamba kwa mapambo pia, nikatia vikuku mikononi mwako, na mkufu shingoni mwako.
Genèse 24.22 Genèse 24.47 Esaïe 3.19 Genèse 41.42 Ezéchiel 23.42
12 Nikatia hazama puani mwako, na pete masikioni mwako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
Esaïe 28.5 Jérémie 13.18 Esaïe 3.21
13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha; na mavazi yako yalikuwa ya kitani safi, na hariri, na kazi ya taraza; ulikula unga mzuri, na asali, na mafuta; nawe ulikuwa mzuri mno, ukafanikiwa hata kufikilia hali ya kifalme.
Deutéronome 32.13-32.14 1 Rois 4.21 Psaumes 50.2 Psaumes 45.13-45.14 Psaumes 48.2
14 Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kwa sababu ya uzuri wako; kwa maana ulikuwa mkamilifu, kwa sababu ya utukufu wangu niliokutia, asema Bwana MUNGU.
Lamentations 2.15 1 Rois 10.24 2 Chroniques 2.11-2.12 2 Chroniques 9.23 Deutéronome 4.6-4.8
15 Lakini uliutumainia uzuri wako, ukafanya mambo ya kikahaba kwa sababu ya sifa zako, ukamwaga mambo yako ya kikahaba juu ya kila mtu aliyepita; ulikuwa wake.
Esaïe 57.8 Ezéchiel 16.25 Jérémie 2.20 Jérémie 7.4 Ezéchiel 23.3
16 Ukatwaa baadhi ya mavazi yako, ukajifanyia mahali palipoinuka, palipopambwa kwa rangi mbalimbali, ukafanya mambo ya kikahaba juu yake; mambo kama hayo hayatakuja wala hayatakuwako.
2 Rois 23.7 2 Chroniques 28.24 Osée 2.8 Ezéchiel 7.20
17 Pia ulivitwaa vyombo vyako vya uzuri, vya dhahabu yangu na vya fedha yangu, nilivyokupa, ukajifanyia sanamu za wanaume, ukafanya mambo ya kikahaba pamoja nazo;
Esaïe 44.19-44.20 Ezéchiel 16.11 Osée 2.13 Ezéchiel 23.14-23.21 Esaïe 57.7-57.8
18 ukatwaa nguo zako za kazi ya taraza, ukawafunika, ukaweka mafuta yangu na uvumba wangu mbele yao.
19 Mkate wangu niliokupa, unga mzuri, na mafuta, na asali, nilivyokulisha, ukaviweka mbele yao viwe harufu ya kupendeza; na ndivyo vilivyokuwa; asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 16.13 Genèse 8.21 Osée 2.8-2.13 Deutéronome 32.14-32.17
20 Pamoja na hayo uliwatwaa wana wako na binti zako, ulionizalia, ukawatoa sadaka kwao ili waliwe. Je! Mambo yako ya kikahaba ni kitu kidogo tu,
Ezéchiel 23.37 Jérémie 7.31 Exode 13.2 Ezéchiel 20.31 Psaumes 106.37-106.38
21 hata ukawaua watoto wangu, na kuwatoa kwa kuwapitisha motoni kwa hao?
2 Rois 17.17 Deutéronome 18.10 Lévitique 20.1-20.5 Psaumes 106.37 2 Rois 21.6
22 Na katika machukizo yako yote, na mambo yako ya kikahaba, hukuzikumbuka siku za ujana wako, ulipokuwa uchi, huna nguo, ukawa ukigaagaa katika damu yako.
Jérémie 2.2 Ezéchiel 16.43 Osée 11.1 Ezéchiel 16.3-16.7 Osée 2.3
23 Tena, imekuwa baada ya uovu wako wote, (ole wako! ole wako! Asema Bwana MUNGU,)
Apocalypse 8.13 Ezéchiel 13.18 Apocalypse 12.12 Sophonie 3.1 Ezéchiel 2.10
24 ulijijengea mahali palipoinuka, ukajifanyia mahali palipoinuka katika kila njia kuu.
Esaïe 57.7 Ezéchiel 16.39 Ezéchiel 16.31 Psaumes 78.58 Ezéchiel 20.28-20.29
25 Umejenga mahali pako palipoinuka penye kichwa cha kila njia, ukaufanya uzuri wako kuwa chukizo, ukatanua miguu yako kwa kila mtu aliyepita karibu, ukaongeza mambo yako ya kikahaba.
Jérémie 3.2 Ezéchiel 16.31 Apocalypse 17.12-17.13 Apocalypse 17.1-17.5 Ezéchiel 16.15
26 Tena umezini na Wamisri, jirani zako, wakuu wa mwili; ukaongeza mambo yako ya kikahaba, ili kunikasirisha.
Ezéchiel 23.19-23.21 Ezéchiel 20.7-20.8 Ezéchiel 8.17 Ezéchiel 8.14 Ezéchiel 23.8
27 Basi, tazama, kwa ajili ya hayo nimenyosha mkono wangu juu yako, nami nimelipunguza posho lako, na kukutoa kwa mapenzi yao wanaokuchukia, binti za Wafilisti, walioyaonea haya mambo yako ya uasherati.
Esaïe 9.12 Ezéchiel 16.57 Ezéchiel 16.37 Esaïe 3.1 Ezéchiel 14.9
28 Pia umefanya mambo ya kikahaba pamoja na Waashuri, kwa sababu ulikuwa huwezi kushibishwa; naam, umefanya mambo ya kikahaba pamoja nao, wala hujashiba bado.
2 Rois 16.7 Osée 10.6 Jérémie 2.36 Jérémie 2.18 2 Rois 16.10-16.18
29 Pamoja na hayo umeongeza mambo yako ya kikahaba katika nchi ya Kanaani, mpaka Ukaldayo, wala hujashibishwa kwa hayo.
2 Rois 21.9 Ezéchiel 23.14-23.21 Juges 2.12-2.19 Ezéchiel 13.14-13.23
30 Jinsi moyo wako ulivyokuwa dhaifu, asema Bwana MUNGU, ikiwa unafanya mambo hayo yote, kazi ya mwanamke mzinzi,
Jérémie 3.3 Esaïe 3.9 Proverbes 9.13 Esaïe 1.3 Jérémie 4.22
31 apendaye kutawala watu; kwa kuwa wajijengea mahali pako pakuu penye kichwa cha kila njia, na kufanya mahali pako palipoinuka katika kila njia kuu; lakini hukuwa kama kahaba, kwa maana ulidharau kupokea ujira.
Ezéchiel 16.33-16.34 Esaïe 52.3 Ezéchiel 16.39 Osée 12.11 Ezéchiel 16.24-16.25
32 Mke wa mtu, aziniye! Akaribishaye wageni badala ya mumewe!
Ezéchiel 16.8 Ezéchiel 23.37 Jérémie 2.25 Osée 3.1 2 Corinthiens 11.2-11.3
33 Watu huwapa makahaba wote zawadi, bali wewe unawapa wapenzi wako wote zawadi zako, na kuwapa rushwa ili waje kwako pande zote, kwa ajili ya mambo yako ya kikahaba.
Osée 8.9-8.10 Esaïe 57.9 Joël 3.3 Michée 1.7 Esaïe 30.3
34 Tena, katika mambo yako ya kikahaba, wewe na wanawake wengine ni mbalimbali, kwa kuwa hapana akufuataye katika mambo yako ya kikahaba; tena kwa kuwa unatoa ujira, wala hupewi ujira; basi, njia yako na njia yao ni mbalimbali.
35 Kwa sababu hiyo, Ewe kahaba, lisikie neno la Bwana;
Ezéchiel 20.47 1 Rois 22.19 Jérémie 3.6-3.8 Jean 4.18 Esaïe 1.21
36 Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu uchafu wako umemwagwa, na uchi wako umefunuliwa, kwa njia ya uzinzi wako pamoja na wapenzi wako; na kwa sababu ya vinyago vyote vya machukizo yako; na kwa sababu ya damu ya watoto wako, uliyowapa;
Ezéchiel 23.10 Genèse 3.10-3.11 Apocalypse 3.18 Psaumes 139.11-139.12 Jérémie 2.34
37 basi, tazama, nitawakusanya wapenzi wako wote ambao umejifurahisha pamoja nao, nao wote uliowapenda, pamoja na watu wote uliowachukia; naam, nitawakusanya juu yako pande zote, na kuwafunulia uchi wako, wapate kuuona uchi wako wote.
Osée 2.10 Jérémie 13.22 Osée 2.3 Ezéchiel 23.9-23.10 Apocalypse 17.16
38 Nami nitakuhukumu, kama wahukumiwavyo wake walioolewa wazinio, na kumwaga damu, nami nitakupatiliza damu ya ghadhabu na wivu.
Lévitique 20.10 Sophonie 1.17 Jérémie 18.21 Genèse 9.6 Ezéchiel 16.20-16.21
39 Tena nitakutia katika mikono yao, nao watapaangusha mahali pako pakuu, na kupabomoa mahali pako palipoinuka, nao watakuvua nguo zako, na kutwaa vyombo vyako vya uzuri, nao watakuacha uchi, huna nguo.
Osée 2.3 Ezéchiel 23.26 Ezéchiel 16.24-16.25 Ezéchiel 7.22-7.24 Ezéchiel 16.10-16.20
40 Tena wataleta mkutano wa watu juu yako, nao watakupiga kwa mawe, na kukuchoma kwa panga zao.
Ezéchiel 23.47 Habakuk 1.6-1.10 Jean 8.5-8.7 Jérémie 25.9 Ezéchiel 23.10
41 Nao watazipiga moto nyumba zako, na kutekeleza hukumu juu yako mbele ya wanawake wengi, nami nitakulazimisha kuacha mambo ya kikahaba, wala hutatoa ujira tena.
Ezéchiel 23.48 Ezéchiel 23.27 Jérémie 52.13 Jérémie 39.8 2 Rois 25.9
42 Hivyo ndivyo nitakavyoshibisha ghadhabu yangu juu yako, na wivu wangu utanitoka, nami nitatulia wala sitaona hasira tena.
Ezéchiel 5.13 Ezéchiel 39.29 Esaïe 40.1-40.2 Zacharie 6.8 Esaïe 54.9-54.10
43 Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako, bali umenikasirisha kwa mambo hayo yote; basi, tazama, mimi nami nitaleta njia yako juu ya kichwa chako, asema Bwana MUNGU; wala hutafanya uasherati zaidi ya machukizo yako yote.
Ezéchiel 16.22 Psaumes 78.42 Ezéchiel 11.21 Ezéchiel 22.31 Ezéchiel 6.9
44 Tazama, kila mtu atumiaye mithali atatumia mithali hii kinyume chako, akisema, Kama mama ya mtu alivyo, ndivyo alivyo binti yake.
Ezéchiel 18.2-18.3 1 Samuel 24.13 Esdras 9.1 Ezéchiel 16.3 2 Rois 17.15
45 Wewe u binti ya mama yako, amchukiaye mume wake na watoto wake; nawe u umbu la maumbu yako, waliowachukia waume zao na watoto wao; mama yako alikuwa Mhiti, na baba yako Mwamori.
Esaïe 1.4 Zacharie 11.8 Ezéchiel 23.37-23.39 Romains 1.30-1.31 Ezéchiel 16.15
46 Na umbu lako mkubwa ni Samaria, akaaye mkono wako wa kushoto, yeye na binti zake; na umbu lako mdogo, akaaye mkono wako wa kuume, ni Sodoma na binti zake.
Ezéchiel 23.4 Ezéchiel 16.48-16.49 Ezéchiel 16.61 Genèse 13.10-13.13 Ezéchiel 16.53-16.56
47 Lakini hukuenda katika njia zao, wala hukutenda sawasawa na machukizo yao; lakini kana kwamba hilo ni jambo dogo sana, ulikuwa umeharibika kuliko wao katika njia zako zote.
2 Rois 21.9 Ezéchiel 16.51 Ezéchiel 16.48 Ezéchiel 5.6-5.7 1 Rois 16.31
48 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, Sodoma, umbu lako, yeye na binti zake, hawakutenda kama wewe ulivyotenda, wewe na binti zako.
Matthieu 10.15 Marc 6.11 Actes 7.52 Matthieu 11.23-11.24 Luc 10.12
49 Tazama, uovu wa umbu lako, Sodoma, ulikuwa huu; kiburi, na kushiba chakula, na kufanikiwa, hayo yalikuwa ndani yake na binti zake; tena hakuutia nguvu mkono wa maskini na mhitaji.
Psaumes 138.6 Genèse 13.10 Ezéchiel 18.16 Daniel 4.30 Amos 5.11-5.12
50 Nao walijivuna, wakafanya machukizo mbele zangu; kwa sababu hiyo naliwaondoa hapo nilipoyaona.
Genèse 19.5 Genèse 18.20 Genèse 19.24 Genèse 13.13 2 Pierre 2.6
51 Samaria naye hakutenda nusu ya dhambi zako; bali wewe umeyaongeza machukizo yako zaidi ya hao, nawe umewapa haki maumbu yako kwa machukizo yako yote uliyoyatenda.
Jérémie 3.8-3.11 Romains 3.9-3.20 Luc 12.47-12.48 Matthieu 12.41-12.42
52 Wewe nawe, ichukue aibu yako mwenyewe, kwa kuwa umetoa hukumu juu ya maumbu yako; kwa dhambi zako ulizozitenda, zilizochukiza kuliko hao, wao wana haki kuliko wewe; naam, ufedheheke wewe nawe, ukaichukue aibu yako, kwa kuwa umewapa haki maumbu yako.
Matthieu 7.1-7.5 Ezéchiel 16.54 Osée 10.6 Genèse 38.26 Jérémie 23.40
53 Nami nitawarudisha watu wao waliofungwa; wafungwa wa Sodoma na binti zake, na wafungwa wa Samaria na binti zake na wafungwa wako waliofungwa kati yao;
Esaïe 19.24-19.25 Ezéchiel 29.14 Ezéchiel 39.25 Jérémie 49.39 Psaumes 126.1
54 upate kuichukua aibu yako mwenyewe, na kutahayari, kwa sababu ya mambo yote uliyoyatenda, kwa kuwa umekuwa faraja kwao.
Jérémie 2.26 Ezéchiel 14.22-14.23 Ezéchiel 16.52 Ezéchiel 36.31-36.32 Ezéchiel 16.63
55 Na maumbu yako, Sodoma na binti zake, watairudia hali yao ya kwanza, na Samaria na binti zake watairudia hali yao ya kwanza, na wewe na binti zako mtairudia hali yenu ya kwanza.
Malachie 3.4 Ezéchiel 36.11 Ezéchiel 16.53
56 Kwa maana umbu lako, Sodoma, hakutajwa kwa kinywa chako katika siku ya kiburi chako;
Luc 15.28-15.30 Esaïe 65.5 Luc 18.11 Sophonie 3.11
57 kabla uovu wako haujafunuliwa bado, kama vile wakati ule walipokutukana binti za Shamu, na wale wote waliomzunguka, binti za Wafilisti wanaokudharau pande zote.
2 Rois 16.5-16.7 Ezéchiel 16.36-16.37 Esaïe 7.1 2 Chroniques 28.5-28.6 2 Chroniques 28.18-28.23
58 Umeuchukua uasherati wako, na machukizo yako, asema Bwana.
Ezéchiel 23.49 Genèse 4.13 Lamentations 5.7
59 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Nitakutenda vile vile kama ulivyotenda, uliyekidharau kiapo kwa kulivunja agano.
Esaïe 24.5 Ezéchiel 17.19 Deutéronome 29.25 Exode 24.1-24.8 Ezéchiel 7.4
60 Walakini nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe, katika siku za ujana wako, nami nitaweka imara agano la milele pamoja nawe.
Jérémie 50.5 Lévitique 26.42 Jérémie 32.38-32.41 Hébreux 12.24 Ezéchiel 16.8
61 Hapo ndipo utakapozikumbuka njia zako, na kutahayarika, hapo utakapowakaribisha maumbu yako, walio wakubwa wako na wadogo wako; nami nitakupa hao wawe binti zako, lakini si kwa agano lako.
Hébreux 8.13 Galates 4.26-4.31 Esaïe 66.7-66.12 Romains 11.11 Ezéchiel 20.43
62 Nami nitaweka imara agano langu nawe; nawe utajua ya kuwa mimi ndimi Bwana;
Jérémie 24.7 Ezéchiel 6.7 Ezéchiel 39.22 Ezéchiel 20.43-20.44 Joël 3.17
63 upate kukumbuka, na kufadhaika, usifumbue kinywa chako tena, kwa sababu ya aibu yako; hapo nitakapokusamehe yote uliyoyatenda, asema Bwana MUNGU.
Romains 3.19 Daniel 9.7-9.8 Psaumes 39.9 Ezéchiel 36.31-36.32 Romains 3.27

Cette Bible est dans le domaine public.