Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 40.23
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa, baada ya mambo hayo, mnyweshaji wa mfalme wa Misri, na mwokaji wake, wakamkosa bwana wao, mfalme wa Misri.
Genèse 40.13 Esther 6.1 Néhémie 1.11-2.2 Genèse 39.20-39.23
2 Farao akawaghadhibikia maakida wake wawili, mkuu wa wanyweshaji na mkuu wa waokaji.
Proverbes 16.14 Proverbes 27.4 1 Chroniques 27.27 Actes 12.20 Proverbes 19.12
3 Akawatia katika lindo nyumbani mwa mkuu wa askari, humo gerezani, mahali alipofungwa Yusufu.
Genèse 39.20 Genèse 39.23
4 Mkuu wa askari akamwekea Yusufu watu hao, naye akawahudumu, nao wakakaa siku kadha wa kadha katika kifungo.
Genèse 39.21-39.23 Psaumes 37.5 Genèse 39.1 Genèse 37.36
5 Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani.
Genèse 41.11 Genèse 12.1-12.7 Job 33.15-33.17 Nombres 12.6 Daniel 4.5
6 Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika.
Genèse 41.8 Genèse 40.8 Daniel 2.1-2.3 Daniel 8.27 Daniel 7.28
7 Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo?
Néhémie 2.2 1 Samuel 1.8 Juges 18.24 2 Samuel 13.4 Luc 24.17
8 Wakamwambia, Tumeota ndoto wala hapana awezaye kuifasiri. Yusufu akawaambia, Kufasiri si kazi ya Mungu? Tafadhalini mniambie.
Genèse 41.15-41.16 Daniel 2.28 Daniel 2.47 Psaumes 25.14 Daniel 5.11-5.15
9 Mnyweshaji mkuu akamhadithia Yusufu ndoto yake; akamwambia, Katika ndoto yangu nimeota, uko mzabibu mbele yangu.
Juges 7.13-7.15 Daniel 4.8 Genèse 37.5-37.10 Daniel 4.10-4.18 Daniel 2.31
10 Na katika mzabibu mlikuwa na matawi matatu, nao ulikuwa kana unamea, unachanua maua, vishada vyake vikatoa zabibu zilizoiva.
11 Na kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, nikampa Farao kikombe mkononi mwake.
Néhémie 1.11-2.1 Genèse 40.21 2 Chroniques 9.4 1 Rois 10.5 Proverbes 3.10
12 Yusufu akamwambia, Tafsiri yake ndiyo hii. Matawi matatu ni siku tatu.
Juges 7.14 Genèse 41.12 Genèse 40.18 Genèse 41.25-41.26 1 Corinthiens 10.4
13 Baada ya siku tatu Farao atakiinua kichwa chako, atakurudisha katika kazi yako; nawe utampa Farao kikombe mkononi mwake, kama desturi ya kwanza, ulipokuwa mnyweshaji wake.
Psaumes 3.3 Jérémie 52.31 2 Rois 25.27 Genèse 40.19-40.22 Genèse 7.4
14 Ila unikumbuke mimi, utakapopata mema, ukanifanyie fadhili, nakuomba, ukanitaje kwa Farao, na kunitoa katika nyumba hii.
Josué 2.12 Luc 23.42 1 Rois 2.7 1 Samuel 20.14-20.15 1 Corinthiens 7.21
15 Kwa sababu hakika naliibiwa kutoka nchi ya Waebrania, wala hapa sikutenda neno lo lote hata wanitie gerezani.
Genèse 39.20 Jean 15.25 1 Timothée 1.10 Genèse 37.26-37.28 Daniel 6.22
16 Mkuu wa waokaji alipoona ya kwamba hiyo tafsiri ni ya mema, akamwambia Yusufu, Mimi kadhalika nilikuwa katika ndoto yangu, na tazama, ziko nyungo tatu za mikate myeupe juu ya kichwa changu.
Genèse 40.1-40.2
17 Na katika ungo wa juu, mlikuwa na kila namna ya chakula kwa Farao, kazi za mwokaji; ndege wakavila katika ungo juu ya kichwa changu.
Genèse 49.20
18 Yusufu akajibu, akasema, Tafsiri yake ndiyo hii Nyungo tatu ni siku tatu.
Genèse 40.12 1 Corinthiens 11.24 1 Corinthiens 10.4 Genèse 41.26
19 Baada ya siku tatu Farao atakiinua na kukuondolea kichwa chako, na kukutundika juu ya mti, na ndege watakula nyama yako.
Genèse 40.22 Deutéronome 21.22-21.23 Genèse 41.13 Galates 3.13 1 Samuel 17.46
20 Ikawa siku ya tatu, siku ya kuzaliwa kwake Farao, akawafanyia karamu watumwa wake wote; akakiinua kichwa cha mkuu wa wanyweshaji, na cha mkuu wa waokaji, miongoni mwa watumwa wake.
Genèse 40.19 Genèse 40.13 Matthieu 14.6 Marc 6.21 2 Rois 25.27
21 Akamrudisha mkuu wa wanyweshaji katika kazi yake ya kunywesha, naye akampa Farao kikombe mkononi mwake.
Genèse 40.13 Néhémie 2.1
22 Bali akamtundika mkuu wa waokaji, kama Yusufu alivyowafasiria.
Genèse 40.19 Daniel 2.30 Daniel 5.12 Daniel 2.19-2.23 Genèse 40.8
23 Lakini huyo mkuu wa wanyweshaji hakumkumbuka Yusufu, alimsahau.
Job 19.14 Psaumes 31.12 Psaumes 105.19 Amos 6.6 Ecclésiaste 9.15-9.16

Cette Bible est dans le domaine public.