Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 18.31
Bible en Swahili de l’est


Confirmation de la naissance d’Isaac

1 Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari.
Genèse 14.13 Genèse 13.18 Genèse 48.3 Genèse 26.2 Genèse 12.7
2 Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi,
Hébreux 13.2 Genèse 18.22 Genèse 19.1 Juges 13.3 Genèse 18.16
3 akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako.
Genèse 32.5
4 Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu.
Genèse 19.2 Genèse 43.24 Genèse 24.32 Luc 7.44 Jean 13.5-13.15
5 Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema.
Juges 13.15 Juges 6.18 Genèse 19.8 Psaumes 104.15 Genèse 33.10
6 Basi Ibrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate.
Luc 10.38-10.40 Galates 5.13 Romains 12.13 1 Pierre 4.9 Actes 16.15
7 Ibrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng’ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa.
Luc 15.23 Juges 13.15-13.16 Malachie 1.14 Genèse 19.3 Amos 6.4
8 Akatwaa siagi na maziwa, na ndama aliyoiandaa, akawaandikia mbele yao, akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala.
Genèse 19.3 Néhémie 12.44 Jean 12.2 Deutéronome 32.14 Luc 24.30
9 Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani.
Genèse 24.67 Genèse 4.9 Tite 2.5 Genèse 31.33
10 Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake.
Genèse 21.2 Genèse 17.21 Genèse 17.19 Genèse 18.13-18.14 Romains 9.8-9.9
11 Basi Ibrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake.
Genèse 17.17 Hébreux 11.11-11.12 Romains 4.18-4.21 Luc 1.18 Hébreux 11.19
12 Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee?
Genèse 17.17 1 Pierre 3.6 Luc 1.18-1.20 Hébreux 11.11-11.12 Ephésiens 5.33
13 Bwana akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee?
Jean 2.25
14 Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Bwana? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.
Jérémie 32.17 Matthieu 19.26 Luc 1.37 Jérémie 32.27 Marc 10.27
15 Akakana Sara, akisema, Sikucheka, maana aliogopa. Naye akasema, Sivyo, umecheka.
Psaumes 44.21 Job 2.10 Jean 2.25 Jean 18.25-18.27 Romains 3.19

Intercession d’Abraham en faveur de Sodome

16 Kisha watu hao wakaondoka huko wakaelekeza nyuso zao Sodoma. Ibrahimu akaenda pamoja nao awasindikize.
Actes 15.3 Actes 20.38 Actes 21.5 3 Jean 1.6 Romains 15.24
17 Bwana akanena, Je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo,
Amos 3.7 Psaumes 25.14 Genèse 19.24 Jean 15.15 2 Chroniques 20.7
18 akiwa Ibrahimu atakuwa taifa kuu, hodari, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa?
Galates 3.8 Genèse 26.4 Ephésiens 1.3 Genèse 22.17-22.18 Genèse 12.2-12.3
19 Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na nyumba yake baada yake waishike njia ya Bwana, wafanye haki na hukumu, ili kwamba Bwana naye akamtimizie Ibrahimu ahadi zake.
Deutéronome 4.9-4.10 Deutéronome 6.6-6.7 Proverbes 22.6 Ephésiens 6.4 Josué 24.15
20 Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
Genèse 19.13 Jacques 5.4 Esaïe 3.9 Genèse 4.10 Jérémie 14.7
21 basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
Genèse 11.5 Exode 3.8 Exode 33.5 Genèse 11.7 Josué 22.22
22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana.
Genèse 19.1 Jérémie 18.20 Psaumes 106.23 Genèse 18.1-18.2 Actes 7.55
23 Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu?
Nombres 16.22 2 Samuel 24.17 Genèse 20.4 Psaumes 11.4-11.7 Hébreux 10.22
24 Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo?
Jérémie 5.1 Esaïe 1.9 Genèse 18.32 Actes 27.24 Matthieu 7.13-7.14
25 Hasha usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha; Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?
Job 8.20 Deutéronome 32.4 Esaïe 3.10-3.11 Job 8.3 Psaumes 94.2
26 Bwana akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha mahali pote kwa ajili yao.
Jérémie 5.1 Esaïe 65.8 Ezéchiel 22.30 Matthieu 24.22 Esaïe 10.22
27 Ibrahimu akajibu, akasema, Basi, nimeshika kusema na Bwana, nami ni mavumbi na majivu tu.
Esaïe 6.5 Genèse 3.19 Genèse 2.7 Luc 18.1 Job 42.6-42.8
28 Huenda wakapunguka watano katika wale hamsini wenye haki, je! Utaharibu mji wote kwa kupungua watano? Akasema, Sitauharibu, nikiona humo arobaini na watano.
Genèse 18.26 1 Rois 20.32-20.33 Nombres 14.17-14.19 Job 23.3-23.4 Genèse 18.29
29 Akazidi tena kusema naye, akinena, Huenda wakaonekana humo arobaini? Akasema, Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini.
Ephésiens 6.18 Hébreux 4.16
30 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema, Huenda wakaonekana huko thelathini? Akasema, Sitafanya, nikiona humo thelathini.
Psaumes 10.17 Hébreux 12.28-12.29 Esaïe 6.5 Psaumes 9.12 Esther 4.11-4.16
31 Akasema, Tazama, nimeshika kusema na Bwana, huenda wakaonekana huko ishirini? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini.
Matthieu 7.7 Luc 11.8 Hébreux 4.16 Matthieu 7.11 Luc 18.1
32 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema mara hii tu, Huenda wakaonekana huko kumi? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao kumi.
Juges 6.39 Jacques 5.15-5.17 Exode 34.9-34.10 Esaïe 42.6-42.7 Genèse 18.30
33 Basi Bwana alipokwisha kuzungumza na Ibrahimu, akaenda zake; Ibrahimu naye akarudi mahali pake.
Genèse 18.16 Genèse 18.22 Genèse 32.26 Genèse 31.55

Cette Bible est dans le domaine public.