Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 13.7
Bible en Swahili de l’est


Instructions diverses et salutations

1 Upendano wa ndugu na udumu.
1 Pierre 1.22 2 Pierre 1.7 1 Pierre 3.8 1 Pierre 2.17 1 Jean 4.20-5.1
2 Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua.
Matthieu 25.35 Romains 12.13 1 Pierre 4.9 Genèse 18.1-19.3 Romains 16.23
3 Wakumbukeni hao waliofungwa kana kwamba mmefungwa pamoja nao; na hao wanaodhulumiwa, kwa vile ninyi nanyi mlivyo katika mwili.
Hébreux 10.34 Matthieu 25.36 1 Corinthiens 12.26 Colossiens 4.18 Romains 12.15
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.
1 Corinthiens 6.9 Galates 5.19 Proverbes 5.15-5.23 Galates 5.21 1 Corinthiens 7.2-7.16
5 Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.
Josué 1.5 Deutéronome 31.8 Deutéronome 31.6 1 Samuel 12.22 1 Chroniques 28.20
6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
Psaumes 118.6-118.9 Esaïe 41.10 Psaumes 27.1-27.3 Romains 8.31 Psaumes 56.4
7 Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.
Hébreux 6.12 Hébreux 13.17 Actes 14.23 Hébreux 13.24 Cantique 1.8
8 Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele.
Malachie 3.6 Jacques 1.17 Hébreux 1.12 Apocalypse 1.8 Jean 8.56-8.58
9 Msichukuliwe na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni; maana ni vizuri moyo ufanywe imara kwa neema, wala si kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida.
Ephésiens 4.14 Romains 14.6 Ephésiens 5.6 2 Corinthiens 1.21 Actes 20.30
10 Tuna madhabahu ambayo wale waihudumiao ile hema hawana ruhusa kula vitu vyake.
1 Corinthiens 9.13 1 Corinthiens 10.20 1 Corinthiens 5.7-5.8 Nombres 7.5 1 Corinthiens 10.17-10.18
11 Maana wanyama wale ambao damu yao huletwa ndani ya patakatifu na kuhani mkuu kwa ajili ya dhambi, viwiliwili vyao huteketezwa nje ya kambi.
Exode 29.14 Lévitique 16.27 Nombres 19.3 Lévitique 9.11 Lévitique 4.5-4.7
12 Kwa ajili hii Yesu naye, ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa nje ya lango.
Ephésiens 5.26 Hébreux 2.11 Marc 15.20-15.24 Actes 7.58 Lévitique 24.23
13 Basi na tutoke tumwendee nje ya kambi, tukichukua shutumu lake.
Hébreux 11.26 1 Corinthiens 4.10-4.13 1 Pierre 4.14-4.16 Actes 5.41 Matthieu 5.11
14 Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.
Hébreux 12.22 Philippiens 3.20 Michée 2.10 2 Pierre 3.13-3.14 Hébreux 11.12-11.16
15 Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.
Osée 14.2 Lévitique 7.12 1 Pierre 2.5 Psaumes 107.21-107.22 Psaumes 136.1-136.26
16 Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.
Philippiens 4.18 Romains 12.13 Ephésiens 4.28 Galates 6.10 Michée 6.7-6.8
17 Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.
Actes 20.28 Hébreux 13.7 1 Pierre 5.2-5.3 1 Timothée 5.17 1 Thessaloniciens 5.12-5.13
18 Tuombeeni; maana tunaamini kwamba tuna dhamiri njema, tukitaka kuwa na mwenendo mwema katika mambo yote.
1 Thessaloniciens 5.25 1 Timothée 1.5 Actes 24.16 Actes 23.1 2 Thessaloniciens 3.1
19 Nami nawasihi zaidi sana kufanya hayo ili nirudishwe kwenu upesi.
Philémon 1.22 Romains 15.31-15.32 Romains 1.10-1.12
20 Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu,
Romains 15.33 Jean 10.11 Zacharie 9.11 Ezéchiel 37.26 Actes 2.24
21 awafanye ninyi kuwa wakamilifu katika kila tendo jema, mpate kuyafanya mapenzi yake, naye akifanya ndani yetu lipendezalo mbele zake, kwa Yesu Kristo; utukufu una yeye milele na milele. Amina.
2 Thessaloniciens 2.17 Philippiens 2.13 Philippiens 1.11 Psaumes 72.18-72.19 1 Pierre 2.5
22 Lakini nawasihi, ndugu, mchukuliane na neno hili lenye maonyo maana nimewaandikia kwa maneno machache.
1 Pierre 5.12 Hébreux 3.1 2 Corinthiens 10.1 Hébreux 10.19-10.39 Hébreux 12.25-12.28
23 Jueni ya kuwa ndugu yetu Timotheo amekwisha kufunguliwa; ambaye, akija upesi, nitaonana nanyi pamoja naye.
1 Thessaloniciens 3.2 Philémon 1.1 Philémon 1.22 2 Timothée 1.8 Romains 15.25
24 Wasalimuni wote wenye kuwaongoza, na watakatifu wote; hao walio wa Italia wanawasalimu.
Hébreux 13.17 Hébreux 13.7 Actes 18.2 Philippiens 1.1 Colossiens 1.2
25 Neema na iwe nanyi nyote.
Colossiens 4.18 Romains 16.20 Ephésiens 6.24 Apocalypse 22.21 Tite 3.15

Cette Bible est dans le domaine public.