Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 4.10
Bible en Swahili de l’est


1 Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.
1 Pierre 4.10 Romains 16.25 Tite 1.7 Ephésiens 6.19 1 Timothée 3.9
2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.
Matthieu 25.21 Luc 12.42 Colossiens 4.17 2 Corinthiens 2.17 Nombres 12.7
3 Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu.
Jean 7.24 1 Samuel 16.7 1 Corinthiens 3.13 1 Corinthiens 2.15
4 Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana.
Psaumes 143.2 1 Jean 3.20-3.21 Psaumes 130.3 2 Corinthiens 1.12 Psaumes 19.12
5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.
2 Corinthiens 10.18 2 Corinthiens 5.10 1 Corinthiens 3.13 Romains 2.16 Romains 2.1

Orgueil et humilité

6 Basi ndugu, mambo hayo nimeyafanya kuwa mfano wa mimi na Apolo kwa ajili yenu, ili kwamba kwa mfano wetu mpate kujifunza kutokupita yale yaliyoandikwa; ili mmoja wenu asijivune kwa ajili ya huyu, kinyume cha mwenziwe.
1 Corinthiens 13.4 1 Corinthiens 1.12 2 Corinthiens 11.4 1 Corinthiens 8.1 1 Corinthiens 4.18-4.19
7 Maana ni nani anayekupambanua na mwingine? Nawe una nini usichokipokea? Lakini iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea?
Jean 3.27 Romains 12.6 1 Pierre 4.10 Jacques 1.17 1 Chroniques 29.11-29.16
8 Mmekwisha kushiba, mmekwisha kupata utajiri, mmemiliki pasipo sisi. Naam, laiti mngemiliki, ili sisi nasi tumiliki pamoja nanyi!
Apocalypse 5.10 Romains 12.15-12.16 1 Corinthiens 1.5 Galates 6.3 Psaumes 122.5-122.9
9 Maana nadhani ya kuwa Mungu ametutoa sisi mitume mwisho, kama watu waliohukumiwa wauawe; kwa sababu tumekuwa tamasha kwa dunia; kwa malaika na wanadamu.
Hébreux 10.33 Romains 8.36 Apocalypse 7.11-7.14 Philippiens 1.29-1.30 Psaumes 44.22
10 Sisi tu wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye akili katika Kristo; sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu; ninyi mna utukufu, lakini sisi hatupati heshima.
1 Corinthiens 2.3 Actes 26.24 Actes 17.18 2 Corinthiens 13.9 1 Corinthiens 3.18
11 Hata saa hii ya sasa, tuna njaa na kiu, tu uchi, twapigwa ngumi, tena hatuna makao;
Romains 8.35 2 Corinthiens 11.23-11.27 Philippiens 4.12 Matthieu 8.20 2 Corinthiens 4.8
12 kisha twataabika tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa twabariki, tukiudhiwa twastahimili;
1 Pierre 3.9 Actes 18.3 Romains 12.20 Matthieu 5.11 Luc 6.28
13 tukisingiziwa twasihi; tumefanywa kama takataka za dunia, na tama ya vitu vyote hata sasa.
Lamentations 3.45 Actes 22.22
14 Siyaandiki hayo ili kuwatahayarisha; bali kuwaonya kama watoto niwapendao.
1 Thessaloniciens 2.11 1 Corinthiens 4.15 Ezéchiel 3.21 1 Corinthiens 6.5 2 Corinthiens 7.3
15 Kwa kuwa ijapokuwa mna waalimu kumi elfu katika Kristo, walakini hamna baba wengi. Maana mimi ndimi niliyewazaa katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili.
Galates 4.19 1 Corinthiens 3.10 Romains 15.20 Philémon 1.10-1.12 1 Corinthiens 9.14
16 Basi, nawasihi mnifuate mimi.
2 Thessaloniciens 3.9 1 Corinthiens 11.1 Philippiens 3.17 1 Thessaloniciens 1.6 Hébreux 13.7
17 Kwa sababu hii nimemtuma Timotheo kwenu, aliye mwanangu mpendwa, mwaminifu katika Bwana, atakayewakumbusha njia zangu zilizo katika Kristo, kama vile nifundishavyo kila mahali katika kila kanisa.
1 Corinthiens 7.17 1 Timothée 1.2 1 Corinthiens 16.10 1 Corinthiens 14.33 2 Timothée 1.2
18 Basi wengine wamejivuna kana kwamba siji kwenu.
1 Corinthiens 4.6-4.8 1 Corinthiens 5.2 1 Corinthiens 4.21
19 Lakini nitakuja kwenu upesi, nikijaliwa, nami nitafahamu, si neno lao tu waliojivuna, bali nguvu zao.
Actes 19.21 Actes 18.21 1 Corinthiens 4.18 Actes 20.2 2 Corinthiens 1.23
20 Maana ufalme wa Mungu hauwi katika neno, bali katika nguvu.
2 Corinthiens 10.4-10.5 1 Corinthiens 2.4 1 Thessaloniciens 1.5 Romains 14.17 Romains 1.16
21 Mnataka vipi? Nije kwenu na fimbo, au nije katika upendo na roho ya upole?
2 Corinthiens 13.2 2 Corinthiens 13.10 1 Thessaloniciens 2.7 2 Corinthiens 1.23 2 Corinthiens 12.20-12.21

Cette Bible est dans le domaine public.