Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 12.4
Bible en Swahili de l’est


Les dons spirituels et leur diversité

1 Basi, ndugu zangu, kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu.
1 Corinthiens 14.37 1 Corinthiens 12.4-12.11 1 Corinthiens 14.1-14.18 Ephésiens 4.11 1 Thessaloniciens 4.13
2 Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa, mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa.
1 Thessaloniciens 1.9 Psaumes 115.5 1 Pierre 4.3 Ephésiens 2.11-2.12 Habakuk 2.18-2.19
3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
1 Jean 4.2-4.3 Jean 13.13 1 Corinthiens 8.6 Romains 9.3 Jean 15.26
4 Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.
1 Corinthiens 12.28 Hébreux 2.4 Romains 12.4-12.6 Ephésiens 4.4-4.6 1 Pierre 4.10
5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.
Matthieu 23.10 Romains 12.6-12.8 Philippiens 2.11 1 Corinthiens 12.28-12.29 Ephésiens 4.11-4.12
6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
Colossiens 3.11 1 Corinthiens 15.28 Jean 5.17 Ephésiens 4.6 1 Corinthiens 12.11
7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
1 Corinthiens 14.19 Romains 12.6-12.8 1 Pierre 4.10-4.11 1 Corinthiens 14.12 Ephésiens 4.7-4.12
8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule;
2 Corinthiens 8.7 1 Corinthiens 2.6-2.10 1 Corinthiens 1.5 1 Corinthiens 1.30 Ephésiens 1.17-1.18
9 mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja;
2 Corinthiens 4.13 1 Corinthiens 12.30 1 Corinthiens 13.2 1 Corinthiens 12.28 Matthieu 17.19-17.20
10 na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;
Marc 16.17 1 Jean 4.1 1 Corinthiens 14.39 1 Corinthiens 12.28-12.30 Galates 3.5
11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.
1 Corinthiens 12.4 Hébreux 2.4 2 Corinthiens 10.13 Ephésiens 1.11 1 Corinthiens 7.17
12 Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo.
1 Corinthiens 12.27 1 Corinthiens 10.17 Ephésiens 4.12 Colossiens 3.15 Colossiens 2.19
13 Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
Colossiens 3.11 Jean 7.37-7.39 Galates 3.28 Jean 3.5 Matthieu 3.11
14 Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.
1 Corinthiens 12.12 1 Corinthiens 12.19 1 Corinthiens 12.27-12.28 Ephésiens 4.25
15 Mguu ukisema, Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si wa mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo?
2 Rois 14.9 Juges 9.8-9.15
16 Na sikio likisema, Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili; je! Si la mwili kwa sababu hiyo?
1 Corinthiens 12.22 Philippiens 2.3 Romains 12.3 Romains 12.10
17 Kama mwili wote ukiwa jicho, ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio ku wapi kunusa?
Psaumes 94.9 Proverbes 20.12 1 Corinthiens 12.21 1 Samuel 9.9 Psaumes 139.13-139.16
18 Bali Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka.
1 Corinthiens 12.28 1 Corinthiens 12.11 Romains 12.3 1 Corinthiens 3.5 Jonas 1.14
19 Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja.
1 Corinthiens 12.12 1 Corinthiens 12.14
21 Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi.
Nombres 10.31-10.32 Esdras 10.1-10.5 1 Samuel 25.32 Néhémie 4.16-4.21 Job 29.11
22 Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi.
Ecclésiaste 9.14-9.15 Proverbes 14.28 2 Corinthiens 1.11 Tite 2.9-2.10 Ecclésiaste 5.9
23 Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana.
Genèse 3.7 Genèse 3.21
24 Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;
Genèse 2.25 Genèse 3.11
25 ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe.
1 Corinthiens 1.10-1.12 2 Corinthiens 8.16 2 Corinthiens 13.11 Jean 17.21-17.26 2 Corinthiens 7.12
26 Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
Romains 12.15 Hébreux 13.3 1 Pierre 3.8 2 Corinthiens 11.28-11.29 Galates 6.2
27 Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
Romains 12.5 Ephésiens 1.23 Ephésiens 4.12 Colossiens 1.24 Ephésiens 5.30
28 Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.
Hébreux 13.24 Ephésiens 4.11-4.13 Hébreux 13.17 Ephésiens 3.5 Romains 12.6-12.8
29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?
1 Corinthiens 12.14-12.20 1 Corinthiens 12.4-12.11
30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?
1 Corinthiens 12.10
31 Takeni sana karama zilizo kuu. Hata hivyo nawaonyesha njia iliyo bora.
1 Corinthiens 14.39 1 Corinthiens 13.1-14.1 Matthieu 5.6 1 Corinthiens 8.1 Philippiens 3.8

Cette Bible est dans le domaine public.