Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 11.31
Bible en Swahili de l’est


Une mise à l’écart ni totale ni définitive

1 Basi, nauliza, Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu, mtu wa kabila ya Benyamini.
1 Samuel 12.22 2 Corinthiens 11.22 Philippiens 3.5 Jérémie 33.24-33.26 Psaumes 77.7
2 Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu,
1 Pierre 1.2 Jean 4.1-4.3 Nombres 16.15 Actes 15.18 Romains 8.29-8.30
3 Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu.
1 Rois 18.4 1 Rois 19.10-19.18 Jérémie 2.30 1 Rois 18.13 1 Rois 18.30-18.31
4 Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali.
1 Rois 19.18 Osée 13.1 Juges 2.13 2 Rois 10.19-10.20 Sophonie 1.4
5 Basi ni vivi hivi wakati huu wa sasa, yako mabaki waliochaguliwa kwa neema.
Romains 9.27 Ephésiens 1.5-1.6 Romains 9.11 Romains 11.28 Romains 11.6-11.7
6 Lakini ikiwa ni kwa neema, haiwi kwa matendo tena, au hapo neema isingekuwa neema.
2 Timothée 1.9 Deutéronome 9.4-9.6 Romains 4.4-4.5 1 Corinthiens 15.10 Ephésiens 2.4-2.9
7 Imekuwaje basi? Kitu kile ambacho Israeli alikuwa akikitafuta hakukipata; lakini wale waliochaguliwa walikipata, na wengine walitiwa uzito.
Romains 9.18 2 Corinthiens 3.14 Romains 8.28-8.30 Esaïe 6.10 1 Pierre 1.2
8 Kama ilivyoandikwa, Mungu aliwapa roho ya usingizi, macho hata wasione, na masikio hata wasisikie, hata siku hii ya leo.
Deutéronome 29.4 Esaïe 29.10 Jérémie 5.21 Ezéchiel 12.2 2 Corinthiens 3.14-3.15
9 Na Daudi asema, Meza yao na iwe tanzi na mtego, Na kitu cha kuwakwaza, na malipo kwao;
Psaumes 69.22-69.23 Hébreux 2.2 Esaïe 66.9 1 Timothée 6.17-6.19 Deutéronome 32.13-32.15
10 Macho yao yatiwe giza ili wasione, Ukawainamishe mgongo wao siku zote.
Psaumes 69.23 Romains 11.8 Esaïe 65.12 2 Pierre 2.4 Zacharie 11.17
11 Basi nasema, Je! Wamejikwaa hata waanguke kabisa? Hasha! Lakini kwa kosa lao wokovu umewafikilia Mataifa, ili wao wenyewe watiwe wivu.
Romains 10.19 Romains 11.14 Ezéchiel 18.23 Romains 11.31 Romains 11.12
12 Basi, ikiwa kosa lao limekuwa utajiri wa ulimwengu, na upungufu wao umekuwa utajiri wa Mataifa, je! Si zaidi sana utimilifu wao?
Romains 11.25 Ephésiens 3.8 Colossiens 1.27 Esaïe 66.8-66.20 Michée 5.7
13 Lakini nasema na ninyi, mlio watu wa Mataifa. Basi, kwa kadiri nilivyo mtume wa watu wa Mataifa, naitukuza huduma iliyo yangu,
Actes 9.15 1 Timothée 2.7 Romains 15.16-15.19 2 Timothée 1.11-1.12 Actes 13.2
14 nipate kuwatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao.
1 Corinthiens 7.16 1 Timothée 4.16 Romains 9.3 Jacques 5.20 Romains 11.11
15 Maana ikiwa kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa ulimwengu, je! Kukubaliwa kwao kutakuwa nini kama si uhai baada ya kufa?
Ezéchiel 37.1-37.14 Romains 11.11-11.12 Luc 15.24 Colossiens 1.20-1.21 Romains 5.10-5.11
16 Tena malimbuko yakiwa matakatifu, kadhalika na donge lote; na shina likiwa takatifu, matawi nayo kadhalika.
Lévitique 23.10 Ezéchiel 44.30 Nombres 15.17-15.21 Proverbes 3.9 Deutéronome 26.10
17 Lakini iwapo matawi mengine yamekatwa, na wewe mzeituni mwitu ulipandikizwa kati yao, ukawa mshirika wa shina la mzeituni na unono wake,
Ephésiens 2.11-2.13 Jean 15.2 Jérémie 11.16 Psaumes 52.8 Ephésiens 3.6
18 usijisifu juu ya matawi yale; au ikiwa wajisifu, si wewe ulichukuaye shina, bali ni shina likuchukualo wewe.
Romains 11.20 Proverbes 16.18 1 Rois 20.11 Ephésiens 2.19-2.20 1 Corinthiens 10.12
19 Basi utasema, Matawi yale yalikatwa kusudi ili nipandikizwe mimi.
Romains 11.17 Romains 11.23-11.24 Romains 11.11-11.12
20 Vema. Yalikatwa kwa kutokuamini kwao, na wewe wasimama kwa imani yako. Usijivune, bali uogope.
1 Corinthiens 10.12 Romains 12.16 2 Corinthiens 1.24 1 Pierre 1.17 Philippiens 2.12
21 Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, wala hatakuachia wewe.
Romains 8.32 2 Pierre 2.4-2.9 Romains 11.19 Romains 11.17 Jude 1.5
22 Tazama, basi, wema na ukali wa Mungu; kwa wale walioanguka, ukali, bali kwako wewe wema wa Mungu, ukikaa katika wema huo; kama sivyo, wewe nawe utakatiliwa mbali.
1 Corinthiens 15.2 Jean 15.2 Hébreux 3.6 Hébreux 3.14 Hébreux 10.23
23 Na hao pia, wasipokaa katika kutokuamini kwao, watapandikizwa; kwa kuwa Mungu aweza kuwapandikiza tena.
2 Corinthiens 3.16 Zacharie 12.10 Matthieu 23.39
24 Kwa maana ikiwa wewe ulikatwa ukatolewa katika mzeituni, ulio mzeituni mwitu kwa asili yake, kisha ukapandikizwa, kinyume cha asili, katika mzeituni ulio mwema, si zaidi sana wale walio wa asili kuweza kupandikizwa katika mzeituni wao wenyewe?
Romains 11.17-11.18 Romains 11.30
25 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
Luc 21.24 Romains 12.16 Romains 16.25 Apocalypse 7.9 Zacharie 14.9-14.21
26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.
Esaïe 59.20 Amos 9.14-9.15 Zacharie 10.6-10.12 Osée 3.5 Jérémie 31.31-31.37
27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao.
Esaïe 27.9 Ezéchiel 36.25-36.29 Esaïe 43.25 Hébreux 8.8-8.12 Jérémie 32.38-32.40
28 Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.
Deutéronome 10.15 Romains 9.5 Luc 1.68-1.75 Romains 11.30 Matthieu 21.43
29 Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake.
Romains 8.28 Nombres 23.19 Hébreux 7.21 Malachie 3.6 Osée 13.14
30 Kwa maana kama ninyi zamani mlivyomwasi Mungu, lakini sasa mmepata rehema kwa kuasi kwao;
Colossiens 3.7 1 Corinthiens 6.9-6.11 Ephésiens 2.19-2.21 1 Pierre 2.10 2 Corinthiens 4.1
31 kadhalika na hao wameasi sasa, ili kwa kupata rehema kwenu wao nao wapate rehema.
Romains 10.16 Romains 11.15 Romains 11.25
32 Maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kuasi ili awarehemu wote.
Romains 3.9 Galates 3.22 1 Timothée 2.4-2.6 Jean 1.7 Jean 12.32
33 Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!
Job 5.9 Psaumes 92.5 Romains 2.4 Ephésiens 3.10 Colossiens 2.2-2.3
34 Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake?
1 Corinthiens 2.16 Job 36.22 Esaïe 40.13 Job 15.8 Jérémie 23.18
35 Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena?
Job 35.7 Job 41.11
36 Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.
1 Corinthiens 8.6 Romains 16.27 1 Timothée 1.17 Jude 1.25 Philippiens 4.20

Cette Bible est dans le domaine public.