Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 11.26
Bible en Swahili de l’est


Une mise à l’écart ni totale ni définitive

1 Basi, nauliza, Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu, mtu wa kabila ya Benyamini.
2 Corinthiens 11.22 Philippiens 3.5 1 Samuel 12.22 Jérémie 33.24-33.26 Actes 22.3
2 Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu,
1 Pierre 1.2 Romains 8.29-8.30 Philippiens 1.22 Actes 3.17 Néhémie 9.30
3 Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu.
Jérémie 2.30 1 Rois 18.13 1 Rois 18.30-18.31 1 Rois 18.4 1 Rois 19.10-19.18
4 Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali.
1 Rois 19.18 2 Rois 10.19-10.20 Sophonie 1.4 Deutéronome 4.3 Jérémie 19.5
5 Basi ni vivi hivi wakati huu wa sasa, yako mabaki waliochaguliwa kwa neema.
Romains 9.27 Ephésiens 1.5-1.6 Romains 9.11 Romains 11.28 Romains 11.6-11.7
6 Lakini ikiwa ni kwa neema, haiwi kwa matendo tena, au hapo neema isingekuwa neema.
1 Corinthiens 15.10 Ephésiens 2.4-2.9 Romains 3.27-3.28 Tite 3.5 Galates 2.21
7 Imekuwaje basi? Kitu kile ambacho Israeli alikuwa akikitafuta hakukipata; lakini wale waliochaguliwa walikipata, na wengine walitiwa uzito.
Romains 9.18 2 Corinthiens 3.14 Philippiens 1.18 Proverbes 1.28 Ephésiens 1.4
8 Kama ilivyoandikwa, Mungu aliwapa roho ya usingizi, macho hata wasione, na masikio hata wasisikie, hata siku hii ya leo.
Deutéronome 29.4 Esaïe 29.10 2 Corinthiens 3.14-3.15 Matthieu 13.13-13.14 Jérémie 5.21
9 Na Daudi asema, Meza yao na iwe tanzi na mtego, Na kitu cha kuwakwaza, na malipo kwao;
Psaumes 69.22-69.23 1 Timothée 6.17-6.19 Deutéronome 32.13-32.15 1 Samuel 25.36-25.38 Psaumes 28.4
10 Macho yao yatiwe giza ili wasione, Ukawainamishe mgongo wao siku zote.
Psaumes 69.23 Zacharie 11.17 2 Pierre 2.17 Jude 1.13 Jude 1.6
11 Basi nasema, Je! Wamejikwaa hata waanguke kabisa? Hasha! Lakini kwa kosa lao wokovu umewafikilia Mataifa, ili wao wenyewe watiwe wivu.
Romains 11.14 Ezéchiel 18.23 Romains 10.19 Ezéchiel 18.32 Actes 18.6
12 Basi, ikiwa kosa lao limekuwa utajiri wa ulimwengu, na upungufu wao umekuwa utajiri wa Mataifa, je! Si zaidi sana utimilifu wao?
Romains 11.25 Michée 5.7 Apocalypse 11.15-11.19 Esaïe 60.1-60.22 Zacharie 8.20-8.23
13 Lakini nasema na ninyi, mlio watu wa Mataifa. Basi, kwa kadiri nilivyo mtume wa watu wa Mataifa, naitukuza huduma iliyo yangu,
Actes 9.15 Actes 13.2 Ephésiens 3.8 Galates 2.7-2.9 Galates 1.16
14 nipate kuwatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao.
1 Corinthiens 7.16 Romains 9.3 Jacques 5.20 1 Timothée 4.16 Philémon 1.12
15 Maana ikiwa kutupwa kwao kumeleta upatanisho kwa ulimwengu, je! Kukubaliwa kwao kutakuwa nini kama si uhai baada ya kufa?
Colossiens 1.20-1.21 Romains 5.10-5.11 Daniel 9.24 2 Corinthiens 5.18-5.20 Ephésiens 1.10
16 Tena malimbuko yakiwa matakatifu, kadhalika na donge lote; na shina likiwa takatifu, matawi nayo kadhalika.
Lévitique 23.10 Ezéchiel 44.30 Deutéronome 26.10 Exode 23.16 Genèse 17.7
17 Lakini iwapo matawi mengine yamekatwa, na wewe mzeituni mwitu ulipandikizwa kati yao, ukawa mshirika wa shina la mzeituni na unono wake,
Ephésiens 2.11-2.13 Jean 15.2 Jérémie 11.16 Psaumes 52.8 Ephésiens 3.6
18 usijisifu juu ya matawi yale; au ikiwa wajisifu, si wewe ulichukuaye shina, bali ni shina likuchukualo wewe.
Romains 11.20 Ephésiens 2.19-2.20 1 Corinthiens 10.12 Galates 3.29 Luc 18.9-18.11
19 Basi utasema, Matawi yale yalikatwa kusudi ili nipandikizwe mimi.
Romains 11.17 Romains 11.23-11.24 Romains 11.11-11.12
20 Vema. Yalikatwa kwa kutokuamini kwao, na wewe wasimama kwa imani yako. Usijivune, bali uogope.
2 Corinthiens 1.24 1 Corinthiens 10.12 Romains 12.16 1 Pierre 1.17 Philippiens 2.12
21 Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, wala hatakuachia wewe.
Romains 8.32 2 Pierre 2.4-2.9 Jude 1.5 Jérémie 49.12 Jérémie 25.29
22 Tazama, basi, wema na ukali wa Mungu; kwa wale walioanguka, ukali, bali kwako wewe wema wa Mungu, ukikaa katika wema huo; kama sivyo, wewe nawe utakatiliwa mbali.
1 Corinthiens 15.2 Jean 15.2 Hébreux 3.6 Hébreux 3.14 Hébreux 10.23
23 Na hao pia, wasipokaa katika kutokuamini kwao, watapandikizwa; kwa kuwa Mungu aweza kuwapandikiza tena.
2 Corinthiens 3.16 Zacharie 12.10 Matthieu 23.39
24 Kwa maana ikiwa wewe ulikatwa ukatolewa katika mzeituni, ulio mzeituni mwitu kwa asili yake, kisha ukapandikizwa, kinyume cha asili, katika mzeituni ulio mwema, si zaidi sana wale walio wa asili kuweza kupandikizwa katika mzeituni wao wenyewe?
Romains 11.17-11.18 Romains 11.30
25 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
Luc 21.24 Romains 12.16 Romains 16.25 Zacharie 14.9-14.21 Ephésiens 3.3-3.4
26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.
Esaïe 59.20 Zacharie 10.6-10.12 Osée 3.5 Jérémie 31.31-31.37 Amos 9.14-9.15
27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao.
Esaïe 27.9 Ezéchiel 36.25-36.29 Jérémie 32.38-32.40 Jérémie 50.20 Esaïe 59.21
28 Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.
Deutéronome 10.15 Romains 9.5 Luc 1.68-1.75 Genèse 28.14 Deutéronome 4.31
29 Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake.
Romains 8.28 Hébreux 7.21 Nombres 23.19 Malachie 3.6 Osée 13.14
30 Kwa maana kama ninyi zamani mlivyomwasi Mungu, lakini sasa mmepata rehema kwa kuasi kwao;
Colossiens 3.7 2 Corinthiens 4.1 1 Timothée 1.18 1 Corinthiens 7.25 Ephésiens 2.12-2.13
31 kadhalika na hao wameasi sasa, ili kwa kupata rehema kwenu wao nao wapate rehema.
Romains 10.16 Romains 11.15 Romains 11.25
32 Maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kuasi ili awarehemu wote.
Romains 3.9 Galates 3.22 Jean 12.32 Romains 3.22 1 Timothée 2.4-2.6
33 Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani!
Psaumes 92.5 Job 5.9 Romains 2.4 Ephésiens 3.10 Colossiens 2.2-2.3
34 Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake?
1 Corinthiens 2.16 Esaïe 40.13 Job 36.22 Job 15.8 Jérémie 23.18
35 Au ni nani aliyempa yeye kitu kwanza, naye atalipwa tena?
Job 35.7 Job 41.11
36 Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina.
1 Corinthiens 8.6 Romains 16.27 Philippiens 4.20 2 Timothée 4.18 2 Pierre 3.18

Cette Bible est dans le domaine public.