Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 20.38
Bible en Swahili de l’est


L’Évangile à Troas

1 Kishindo kile kilipokoma, Paulo akatuma kuwaita wanafunzi akawaonya, akaagana nao, kisha akaondoka aende zake mpaka Makedonia.
Actes 19.21 Actes 20.10 1 Samuel 20.41-20.42 Actes 19.23-19.41 1 Corinthiens 16.5
2 Naye akiisha kupita pande zile na kuwafariji kwa maneno mengi, akafika Uyunani.
Actes 20.6-20.7 Actes 17.10 Actes 15.41 Colossiens 1.28 Actes 20.11
3 Alipokwisha kukaa huko miezi mitatu, na Wayahudi kumfanyia vitimvi, alipotaka kwenda Shamu kwa njia ya bahari; basi akaazimu kurejea kwa njia ya Makedonia.
Actes 20.19 Actes 9.23-9.24 Actes 25.3 2 Corinthiens 11.26 Galates 1.21
4 Watu hawa wakafuatana naye, Sopatro Mberoya, mwana wa Piro, na Aristarko na Sekundo, watu wa Thesalonike; na Gayo mtu wa Derbe, na Timotheo; na Tikiko na Trofimo watu wa Asia.
Actes 19.29 Colossiens 4.7 Actes 16.1 Actes 21.29 Tite 3.12
5 Ila watu hao wamekwisha kutangulia wakamngojea Troa.
Actes 16.8 Actes 16.10-16.11 2 Timothée 4.13 Actes 20.13-20.15 2 Corinthiens 2.12
6 Sisi tukatweka baada ya siku za mikate isiyotiwa chachu, tukatoka Filipi, tukawafikia Troa, safari ya siku tano, tukakaa huko siku saba.
Actes 12.3 Actes 16.12 Exode 12.14-12.15 Exode 23.15 Exode 12.18-12.20
7 Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza maneno yake hata usiku wa manane.
Actes 20.11 1 Corinthiens 16.2 Actes 2.42 Apocalypse 1.10 Jean 20.19
8 Palikuwa na taa nyingi katika orofa ile tulipokuwa tumekusanyika.
Actes 1.13 Luc 22.12
9 Kijana mmoja, jina lake Eutiko, alikuwa ameketi dirishani, akalemewa na usingizi sana; hata Paulo alipoendelea sana kuhubiri, akazidiwa na usingizi wake akaanguka toka orofa ya tatu; akainuliwa amekwisha kufa.
Marc 9.26 Jonas 1.5-1.6 Matthieu 26.40-26.41 Actes 14.19 1 Rois 17.19
10 Paulo akashuka, akamwangukia, akamkumbatia, akasema, Msifanye ghasia, maana uzima wake ungalimo ndani yake.
Marc 5.39 Matthieu 9.23-9.24 Jean 11.40 1 Rois 17.21-17.22 Jean 11.11
11 Akapanda juu tena, akamega mkate, akala, akazidi kuongea nao hata alfajiri, ndipo akaenda zake.
Actes 20.7 Actes 20.9
12 Wakamleta yule kijana, yu mzima, wakafarijika faraja kubwa sana.
1 Thessaloniciens 3.2 Esaïe 40.1 2 Thessaloniciens 2.16 1 Thessaloniciens 5.14 1 Thessaloniciens 4.18
13 Lakini sisi tukatangulia kwenda merikebuni, tukaabiri kwenda Aso, tukikusudia kumpakia Paulo huko; kwa maana ndivyo alivyoagiza, yeye mwenyewe aliazimu kwenda kwa miguu.
Marc 6.31-6.33 Marc 6.46 Marc 1.35
14 Alipotufikia huko Aso, tukampakia, kisha tukafika Mitilene.
15 Tukatweka kutoka huko, na siku ya pili tukafika mahali panapokabili Kio; siku ya tatu tukawasili Samo, tukakaa Trogilio, siku ya nne tukafika Mileto.
Actes 20.17 2 Timothée 4.20

Paul et les anciens d’Éphèse

16 Kwa sababu Paulo amekusudia kupita Efeso merikebuni, asije akakawia katika Asia; kwa maana alikuwa na haraka, akitaka kuwahi Yerusalemu siku ya Pentekoste, kama ikiwezekana.
1 Corinthiens 16.8 Actes 2.1 Actes 19.21 Actes 20.6 Romains 15.24-15.28
17 Toka Mileto Paulo akatuma watu kwenda Efeso, akawaita wazee wa kanisa.
Actes 11.30 Actes 14.23 1 Timothée 5.17 Actes 20.28 Tite 1.5
18 Walipofika kwake, akawaambia, Ninyi wenyewe mnajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu wakati wote,
Actes 19.1 Actes 18.19 Actes 19.10 1 Thessaloniciens 1.5-1.6 2 Thessaloniciens 3.7-3.9
19 nikimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, na kwa machozi, na majaribu yaliyonipata kwa hila za Wayahudi;
Actes 20.3 Actes 20.31 2 Corinthiens 2.4 Romains 12.11 Colossiens 3.24
20 ya kuwa sikujiepusha katika kuwatangazia neno lo lote liwezalo kuwafaa bali naliwafundisha waziwazi, na nyumba kwa nyumba,
Actes 20.27 Actes 5.42 Actes 20.31 2 Timothée 4.2 2 Timothée 3.16-3.17
21 nikiwashuhudia Wayahudi na Wayunani wamtubie Mungu, na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.
Actes 2.38 1 Jean 5.11-5.13 Actes 11.18 Actes 20.24 Marc 6.12
22 Basi sasa, angalieni, nashika njia kwenda Yerusalemu hali nimefungwa rohoni, nisiyajue mambo yatakayonikuta huko;
Luc 12.50 Actes 20.16 Luc 18.31-18.33 Actes 17.16 Actes 19.21
23 isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja.
Actes 9.16 Actes 21.4 Actes 14.22 1 Thessaloniciens 3.3 Actes 21.11
24 Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo wangu na huduma ile niliyopokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.
Actes 21.13 Actes 20.21 Galates 1.1 Actes 1.17 2 Corinthiens 4.1
25 Na sasa, tazameni, mimi najua ya kuwa ninyi nyote niliowahubiria ufalme wa Mungu, nikienda huko na huko, hamtaniona uso tena.
Actes 28.31 Matthieu 4.23 Actes 20.38 Colossiens 2.1 Matthieu 4.17
26 Kwa hiyo nawashuhudia wote siku hii ya leo, ya kuwa mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote.
Actes 18.6 Job 16.19 Ezéchiel 3.18-3.21 1 Timothée 5.22 2 Corinthiens 7.2
27 Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.
Actes 20.20 1 Thessaloniciens 2.4 Galates 1.7-1.10 Matthieu 28.20 Luc 7.30
28 Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
1 Pierre 5.2-5.3 Esaïe 40.11 1 Timothée 5.17 Michée 7.14 Philippiens 1.1
29 Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi;
Matthieu 7.15 Jean 10.12 Actes 20.28 Zacharie 11.17 Jérémie 13.20
30 tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao.
1 Jean 2.19 2 Timothée 4.3-4.4 1 Timothée 1.19-1.20 Jude 1.4-1.16 Actes 11.26
31 Kwa hiyo kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi.
Actes 19.10 Actes 19.8 Hébreux 13.17 Actes 20.19 Colossiens 1.28
32 Basi, sasa nawaweka katika mikono ya Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliotakaswa.
Colossiens 1.12 Colossiens 3.24 Hébreux 9.15 Actes 26.18 Actes 14.23
33 Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu.
2 Corinthiens 11.9 1 Corinthiens 9.12 2 Corinthiens 7.2 1 Corinthiens 9.18 1 Corinthiens 9.15
34 Ninyi wenyewe mnajua ya kuwa mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami.
Actes 18.3 1 Corinthiens 4.12 1 Thessaloniciens 2.9 Actes 19.22 2 Thessaloniciens 3.8-3.9
35 Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.
2 Corinthiens 9.6-9.12 Proverbes 19.17 Luc 14.12-14.14 1 Thessaloniciens 5.14 2 Corinthiens 8.9
36 Alipokwisha kunena haya akapiga magoti, akaomba pamoja nao wote.
Actes 21.5 Luc 22.41 Actes 7.60 Ephésiens 3.14 Daniel 6.10
37 Wakalia sana wote, wakamwangukia Paulo shingoni, wakambusu-busu,
Luc 15.20 2 Timothée 1.4 1 Samuel 20.41 1 Thessaloniciens 5.26 Esdras 10.1
38 wakihuzunika zaidi kwa sababu ya neno lile alilosema, ya kwamba hawatamwona uso tena. Wakamsindikiza hata merikebuni.
Actes 15.3 Actes 20.25 1 Corinthiens 16.11 Actes 21.5 Actes 21.16

Cette Bible est dans le domaine public.