Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 1.37
Bible en Swahili de l’est


Présentation de Jésus

L’incarnation de la Parole

1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
1 Jean 1.1-1.2 Jean 17.5 Genèse 1.1 Jean 1.14 Apocalypse 19.13
2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.
3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.
Colossiens 1.16-1.17 1 Corinthiens 8.6 Apocalypse 4.11 Jean 1.10 Psaumes 33.6
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
Jean 8.12 Jean 11.25 Jean 5.26 Jean 14.6 Jean 12.46
5 Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
1 Corinthiens 2.14 Jean 3.19-3.20 Jean 12.36-12.40 Romains 1.28 Job 24.13-24.17
6 Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
Malachie 3.1 Jean 3.28 Jean 1.33 Esaïe 40.3-40.5 Luc 1.13
7 Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye.
Actes 19.4 Jean 5.33-5.35 Jean 1.19 Jean 3.26-3.36 Jean 1.12
8 Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru.
Jean 1.20 Actes 19.4 Jean 3.28
9 Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu.
1 Jean 2.8 Esaïe 49.6 Jean 12.46 Jean 1.4 Jean 1.7
10 Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua.
Jean 17.25 Hébreux 11.3 1 Jean 3.1 Actes 17.24-17.27 1 Corinthiens 1.21
11 Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea.
Esaïe 53.2-53.3 Jean 3.32 Luc 20.13-20.15 Luc 19.14 Matthieu 15.24
12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;
Galates 3.26 1 Jean 3.1 2 Corinthiens 6.17-6.18 Romains 8.14 Colossiens 2.6
13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.
Jacques 1.18 1 Jean 3.9 1 Pierre 1.23 1 Pierre 1.3 1 Jean 5.4
14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.
1 Timothée 3.16 Galates 4.4 Jean 1.1 1 Jean 4.9 Esaïe 40.5
15 Yohana alimshuhudia, akapaza sauti yake akasema, Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Ajaye nyuma yangu amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.
Matthieu 3.11 Jean 3.26-3.36 Jean 17.5 Jean 1.1-1.2 Jean 8.58
16 Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.
Colossiens 1.19 Romains 5.2 Ephésiens 4.7-4.13 1 Corinthiens 1.4-1.5 Ephésiens 3.19
17 Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.
Jean 8.32 Jean 14.6 Romains 3.19-3.26 Romains 6.14 Hébreux 9.22
18 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
Colossiens 1.15 1 Jean 4.12 Jean 6.46 1 Timothée 6.16 1 Jean 4.9

Témoignage de Jean-Baptiste sur Jésus

19 Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?
Jean 10.24 Actes 13.25 Luc 3.15-3.18 Jean 5.33-5.36 Matthieu 21.23-21.32
20 Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.
Jean 3.28-3.36 Marc 1.7-1.8 Matthieu 3.11-3.12 Luc 3.15-3.17
21 Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La.
Matthieu 11.14 Jean 1.25 Matthieu 16.14 Jean 7.40 Malachie 4.5
22 Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako?
2 Samuel 24.13
23 Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.
Matthieu 3.3 Esaïe 40.3-40.5 Marc 1.3 Luc 1.76-1.79 Luc 1.16-1.17
24 Nao wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo.
Luc 16.14 Actes 26.5 Jean 3.1-3.2 Matthieu 23.26 Luc 7.30
25 Wakamwuliza, wakamwambia, Mbona basi wabatiza, ikiwa wewe si Kristo, wala Eliya, wala nabii yule?
Deutéronome 18.18 Jean 1.20-1.22 Daniel 9.24-9.26 Actes 5.28 Deutéronome 18.15
26 Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi.
Luc 3.16 Actes 1.5 Matthieu 3.11 Marc 1.8 Jean 1.10-1.11
27 Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake.
Jean 1.30 Matthieu 3.11 Jean 1.15 Marc 1.7 Luc 3.16
28 Hayo yalifanyika huko Bethania ng’ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza.
Jean 10.40 Jean 3.23 Juges 7.24 Jean 3.26
29 Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
1 Pierre 1.19 Actes 8.32 1 Jean 3.5 Apocalypse 5.8 Jean 1.36
30 Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu.
Jean 1.27 Jean 1.15 Luc 3.16
31 Wala mimi sikumjua; lakini kusudi adhihirishwe kwa Israeli ndiyo maana mimi nalikuja nikibatiza kwa maji.
Luc 1.17 Marc 1.3-1.5 Matthieu 3.6 Luc 3.3-3.4 Esaïe 40.3-40.5
32 Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake.
Marc 1.10 Matthieu 3.16 Luc 3.22 Jean 1.7 Jean 5.32
33 Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenipeleka kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.
Matthieu 3.11 Actes 1.5 Luc 3.16 Tite 3.5-3.6 Actes 19.2-19.6
34 Nami nimeona, tena nimeshuhudia ya kuwa huyu ni Mwana wa Mungu.
Matthieu 4.3 Jean 1.49 Psaumes 2.7 Psaumes 89.26-89.27 Matthieu 11.27
35 Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.
Jean 3.25-3.26 Malachie 3.16
36 Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!
Jean 1.29 1 Pierre 1.19-1.20 Esaïe 65.1-65.2 Hébreux 12.2 Esaïe 45.22
37 Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.
Romains 10.17 Zacharie 8.21 Jean 4.39-4.42 Apocalypse 22.17 Jean 1.43
38 Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?
Jean 1.49 Jean 18.4 Jean 3.2 Jean 18.7 Jean 20.15-20.16
39 Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi.
Luc 24.29 Jean 1.46 Matthieu 11.28-11.30 Proverbes 8.17 Jean 4.40
40 Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.
Marc 1.16-1.20 Matthieu 4.18-4.22 Jean 1.40-1.42 Luc 5.2-5.11 Matthieu 10.2
41 Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo).
Jean 4.25 Jean 4.28-4.29 Jean 1.45 Jean 1.36-1.37 Actes 10.38
42 Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).
Jean 21.15-21.17 1 Corinthiens 1.12 1 Corinthiens 3.22 1 Corinthiens 9.5 Galates 2.9
43 Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.
Matthieu 9.9 Matthieu 4.18-4.21 Jean 14.8 Jean 6.7 Jean 12.21
44 Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro.
Jean 12.21 Matthieu 11.21 Matthieu 10.3 Marc 6.45 Marc 3.18
45 Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, Tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti.
Luc 24.27 Deutéronome 18.18-18.22 Matthieu 2.23 Jean 21.2 Luc 4.22
46 Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone.
Jean 7.52 Jean 4.29 Jean 7.41-7.42 1 Thessaloniciens 5.21 Luc 12.57
47 Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.
Romains 9.6 Psaumes 32.2 Jean 8.31 Romains 9.4 Apocalypse 14.5
48 Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona.
Jean 2.25 Esaïe 65.24 Matthieu 6.6 Apocalypse 2.18-2.19 Psaumes 139.1-139.2
49 Nathanaeli akamjibu, Rabi, wewe u Mwana wa Mungu, ndiwe Mfalme wa Israeli.
Jean 1.34 Zacharie 9.9 Matthieu 2.2 Matthieu 27.42 Matthieu 21.5
50 Yesu akajibu, akamwambia, Kwa sababu nilikuambia, Nilikuona chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.
Jean 20.29 Jean 11.40 Luc 1.45 Matthieu 25.29 Luc 7.9
51 Akamwambia, Amin, amin, nawaambia, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.
Genèse 28.12 Actes 7.56 Ezéchiel 1.1 Luc 3.21 Matthieu 3.16

Cette Bible est dans le domaine public.