Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 26.20
Bible en Swahili de l’est


Bénédictions et malédictions

1 Msifanye sanamu yo yote, wala msijisimamishie sanamu ya kuchonga, wala mnara, wala msiweke jiwe lo lote lililochorwa katika nchi yenu ili kulisujudia; kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Lévitique 19.4 Exode 23.24 Exode 20.4-20.5 Exode 20.23 Nombres 33.52
2 Zishikeni Sabato zangu, na kupastahi patakatifu pangu; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 19.30
3 Kama mkienda katika amri zangu, na kuyashika maagizo yangu, na kuyafanya;
Deutéronome 28.1-28.14 Deutéronome 11.13-11.15 Psaumes 81.12-81.16 Esaïe 48.18-48.19 Matthieu 7.24-7.25
4 ndipo nitazinyesha mvua zenu kwa nyakati zake, na nchi itazaa maongeo yake, na miti ya mashambani itazaa matunda yake.
Psaumes 67.6 Psaumes 68.9 Job 38.25-38.28 Joël 2.23-2.24 Deutéronome 11.14
5 Tena kupura nafaka kwenu kutaendelea hata wakati wa kuvuna zabibu, na kuvuna zabibu kutaendelea hata wakati wa kupanda mbegu; nanyi mtakula chakula chenu na kushiba, na kuketi katika nchi yenu salama.
Amos 9.13 Deutéronome 11.15 Lévitique 25.18-25.19 Joël 2.19 Joël 2.26
6 Nami nitawapa amani katika nchi, tena mtalala wala hapana atakayewatia hofu; nami nitawakomesha wanyama wabaya katika nchi yenu, wala hautapita upanga katika nchi yenu.
Sophonie 3.13 Psaumes 147.14 Jérémie 30.10 Esaïe 35.9 Psaumes 29.11
7 Nanyi mtawafukuza adui zenu, nao wataanguka mbele zenu kwa upanga.
8 Na watu watano wa kwenu watawafukuza watu mia, na watu mia wa kwenu watawafukuza watu elfu kumi; na adui zenu wataanguka mbele yenu kwa upanga.
Josué 23.10 Deutéronome 32.30 1 Chroniques 11.20 Juges 7.19-7.21 1 Chroniques 11.11
9 Nami nitawaelekezea uso wangu, na kuwapa uzazi mwingi, na kuwaongeza; nami nitalithibitisha agano langu pamoja nanyi.
Néhémie 9.23 Genèse 17.6-17.7 Exode 2.25 Psaumes 89.3 Exode 1.7
10 Nanyi mtakula akiba ya zamani mliyoiweka siku nyingi, tena hayo ya zamani mtayatoa, ili myaweke yaliyo mapya.
Lévitique 25.22 Luc 12.17 2 Rois 19.29 Josué 5.11
11 Nami nitaiweka maskani yangu kati yenu; wala roho yangu haitawachukia.
Exode 25.8 Psaumes 76.2 Apocalypse 21.3 Exode 29.45 Ezéchiel 37.26-37.28
12 Nami nitakwenda kati yenu, nami nitakuwa Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu.
2 Corinthiens 6.16 Jérémie 30.22 Jérémie 7.23 Exode 6.7 Exode 19.5-19.6
13 Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, niliyewaleta mtoke katika nchi ya Misri, ili msiwe watumwa wao; nami nimeivunja miti ya kongwa lenu, nikawaendesha mwende sawasawa.
Ezéchiel 34.27 Exode 20.2 Lévitique 25.38 1 Corinthiens 6.19-6.20 Psaumes 116.16
14 Lakini msiponisikiza, wala hamtaki kuyafanya maagizo hayo yote;
Deutéronome 28.15-28.68 Malachie 2.2 Lamentations 2.17 Lévitique 26.18 Jérémie 17.27
15 nanyi mkizikataa amri zangu, na roho yenu ikichukia hukumu zangu, hata ikawa hamtaki kuyafanya maagizo yangu yote, bali mwalivunja agano langu;
Deutéronome 31.16 2 Rois 17.15 Genèse 17.14 2 Samuel 12.9-12.10 Proverbes 1.30
16 mimi nami nitawatenda jambo hili; nitaamrisha uje juu yenu utisho, hata kifua kikuu na homa, zitakazoharibu macho yenu, na kuidhoofisha roho; nanyi mtapanda mbegu yenu bure, kwa kuwa adui zenu wataila.
Job 31.8 1 Samuel 2.33 Psaumes 78.33 Deutéronome 28.21-28.22 Michée 6.15
17 Nami nitauelekeza uso wangu kinyume chenu, nanyi mtapigwa mbele ya adui zenu; hao wawachukiao watatawala juu yenu; nanyi mtakimbia wakati ambao hapana awafukuzaye.
Proverbes 28.1 Deutéronome 28.25 Lévitique 17.10 Psaumes 53.5 Jérémie 19.7
18 Tena ikiwa baada ya hayo hamtaki kunisikiza, ndipo nitawaadhibu zaidi mara saba kwa ajili ya dhambi zenu.
Lévitique 26.28 Lévitique 26.21 Lévitique 26.24 Proverbes 24.16 1 Samuel 2.5
19 Nami nitakivunja kiburi cha uwezo wenu; nami nitazifanya mbingu zenu kuwa kama chuma, na nchi yenu kuwa kama shaba;
Deutéronome 28.23 Jérémie 14.1-14.6 Esaïe 25.11 Jérémie 13.9 1 Samuel 4.3
20 na nguvu zenu mtazitumia bure; kwa kuwa nchi yenu haitazaa mazao yake, wala miti ya nchi haitazaa matunda yake.
Psaumes 127.1 Esaïe 49.4 Lévitique 26.4 Deutéronome 11.17 Deutéronome 28.18
21 Nanyi ikiwa mwaenenda kinyume changu, wala hamtaki kunisikiza; nitaleta mapigo mara saba zaidi juu yenu, kama dhambi zenu zilivyo.
Lévitique 26.18 Lévitique 26.27
22 Nami nitaleta wanyama wakali kati yenu, ambao watawanyang’anya watoto wenu, na kuwaharibu wanyama wenu wa kufugwa, na kuwapunguza muwe wachache hesabu yenu; na njia zenu zitakuwa ni ukiwa.
Ezéchiel 14.15 Deutéronome 32.24 Juges 5.6 Lamentations 1.4 2 Rois 17.25
23 Tena kama hamtaki kurejezwa upya kwangu mimi kwa mambo haya, bali mwaendelea kunishikia kinyume; ndipo mimi nami nitaendelea kuwashikia ninyi kinyume;
Jérémie 5.3 Jérémie 2.30 Amos 4.6-4.12 Lévitique 26.21 Esaïe 1.16-1.20
24 nami nitawapiga, naam mimi, mara saba kwa ajili ya dhambi zenu.
Psaumes 18.26 2 Samuel 22.27 Esaïe 63.10 Job 9.4
25 Nami nitaleta upanga juu yenu, utakaopatiliza kisasi cha hilo agano; nanyi mtakutanishwa ndani ya miji yenu; nami nitaleta tauni kati yenu; nanyi mtatiwa mkononi mwa adui.
Nombres 14.12 Ezéchiel 5.17 Jérémie 24.10 Ezéchiel 14.17 Jérémie 29.17-29.18
26 Hapo nitakapovunja tegemeo lenu la mkate, wanawake kumi wataoka mikate yenu katika tanuu moja, nao watawapa mikate yenu tena kwa kupima kwa mizani; nanyi mtakula, lakini hamtashiba.
Michée 6.14 Esaïe 3.1 Psaumes 105.16 Ezéchiel 5.16 Ezéchiel 4.16
27 Tena ikiwa baada ya hayo yote hamtaki kunisikiza, bali mwaenenda kwa kunishikia kinyume;
Lévitique 26.21 Lévitique 26.24
28 ndipo nami nitakwenda kwa kuwashikia ninyi kinyume katika ghadhabu yangu; nami nitawaadhibu mara saba kwa dhambi zenu.
Esaïe 59.18 Esaïe 63.3 Esaïe 66.15 Jérémie 21.5 Ezéchiel 5.15
29 Nanyi mtakula nyama ya miili ya wana wenu, na nyama ya miili ya binti zenu mtaila.
Lamentations 4.10 Ezéchiel 5.10 2 Rois 6.28-6.29 Jérémie 19.9 Deutéronome 28.53-28.57
30 Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia.
2 Rois 23.20 Ezéchiel 6.3-6.6 Ezéchiel 6.13 Esaïe 27.9 Jérémie 14.19
31 Nami nitaifanya miji yenu iwe maganjo, na mahali penu patakatifu nitapatia ukiwa; wala sitasikia harufu ya manukato yenu yapendezayo.
Néhémie 2.3 Lamentations 1.10 Amos 5.21-5.23 Hébreux 10.26 Ezéchiel 9.6
32 Nami nitaitia hiyo nchi ukiwa; na adui zenu watakaokaa huko wataistaajabia.
Jérémie 9.11 Jérémie 18.16 Jérémie 19.8 Jérémie 25.11 Deutéronome 28.37
33 Nanyi nitawatapanya-tapanya katika mataifa, nami nitaufuta upanga nyuma yenu; na nchi yenu itakuwa ni ukiwa, na miji yenu maganjo.
Deutéronome 4.27 Ezéchiel 20.23 Zacharie 7.14 Psaumes 44.11 Jérémie 9.16
34 Hapo ndipo nchi itakapozifurahia Sabato zake, wakati itakapokuwa hali ya ukiwa, nanyi mtakapokuwa katika nchi ya adui zenu; ndipo nchi itakapopumzika, na kuzifurahia Sabato zake.
2 Chroniques 36.21 Lévitique 26.43 Lévitique 25.10 Lévitique 25.2-25.4
35 Wakati wote itakapokuwa na ukiwa, itapumzika; ni hayo mapumziko ambayo haikuwa nayo katika Sabato zenu, hapo mlipokaa katika nchi hiyo.
Esaïe 24.5-24.6 Romains 8.22
36 Tena hao wa kwenu watakaobaki, nitawatilia woga mioyoni mwao, katika hizo nchi za adui zao; na sauti ya jani lililopeperushwa itawakimbiza; nao watakimbia, kama mtu akimbiavyo upanga; nao wataanguka hapo ambapo hapana afukuzaye.
Ezéchiel 21.7 Lévitique 26.17 Esaïe 30.17 Esaïe 7.2 Deutéronome 28.65-28.67
37 Nao wataangukiana wenyewe kwa wenyewe, kama mbele ya upanga, hapo ambapo hapana afukuzaye; wala hamtakuwa na nguvu za kusimama mbele ya adui zenu.
Josué 7.12-7.13 Juges 2.14 Nombres 14.42 1 Samuel 14.15-14.16 Juges 7.22
38 Nanyi mtaangamia kati ya mataifa, na nchi ya adui zenu itawameza.
Deutéronome 4.26-4.27 Jérémie 42.22 Deutéronome 28.68 Esaïe 27.13 Jérémie 42.17-42.18
39 Na watu wa kwenu watakaobaki watafifia kwa ajili ya uovu wao, katika hizo nchi za adui zenu; tena watafifia kwa ajili ya uovu wa baba zao, pamoja nao.
Ezéchiel 4.17 Ezéchiel 33.10 Deutéronome 28.65 Ezéchiel 24.23 Ezéchiel 6.9
40 Nao wataukiri uovu wao, na uovu wa baba zao, katika maasi yao waliyoasi juu yangu, tena ya kuwa kwa sababu wameendelea kunishikia kinyume,
1 Jean 1.8-1.10 Proverbes 28.13 1 Rois 8.33-8.36 Lévitique 26.21 Osée 5.15-6.2
41 mimi nami nimeendelea kuwashikia kinyume wao, na kuwatia katika nchi ya adui zao; lakini hapo, kama mioyo yao isiyokuwa tohara ikinyenyekea, nao wakubali adhabu ya uovu wao;
Actes 7.51 Ezéchiel 44.7 Jérémie 9.25-9.26 Jérémie 4.4 Philippiens 3.3
42 ndipo nitakapokumbuka agano langu pamoja na Yakobo, tena agano langu na Isaka, tena agano langu na Ibrahimu nitalikumbuka; nami nitaikumbuka nchi hiyo.
Psaumes 106.45 Exode 2.24 Ezéchiel 16.60 Exode 6.5 Joël 2.18
43 Nchi nayo itaachwa na wao, nayo itazifurahia Sabato zake, itakapokuwa ukiwa pasipokuwa na wao; nao wataikubali adhabu ya uovu wao; kwa sababu, naam, ni kwa sababu wamezikataa hukumu zangu, na roho zao zimezichukia amri zangu.
Lévitique 26.15 Lévitique 26.34-26.35 Esaïe 26.16 Zacharie 11.8 Job 34.31-34.32
44 Lakini pamoja na hayo yote, watakapokuwa katika nchi ya adui zao, mimi, sitawatupa, wala sitawachukia, niwaangamize kabisa, na kulivunja agano langu pamoja nao; kwa kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wao;
Romains 11.2 Néhémie 9.31 2 Rois 13.23 Jérémie 33.20-33.21 Psaumes 94.14
45 lakini kwa ajili yao nitalikumbuka agano la baba zao, niliowaleta watoke katika nchi ya Misri mbele ya macho ya mataifa, ili kwamba niwe Mungu wao; mimi ndimi Bwana.
Lévitique 25.38 Ezéchiel 20.9 Lévitique 22.33 Ezéchiel 20.22 Genèse 15.18
46 Hizi ni amri na hukumu na sheria, Bwana alizozifanya kati ya yeye na hao wana wa Israeli katika huo mlima wa Sinai kwa mkono wa Musa.
Lévitique 27.34 Lévitique 25.1 Deutéronome 12.1 Deutéronome 6.1 Deutéronome 13.4

Cette Bible est dans le domaine public.