Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 40.11
Bible en Swahili de l’est


Vision du temple

1 Katika mwaka wa ishirini na tano wa kuhamishwa kwetu, mwanzo wa mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kupigwa mji, siku iyo hiyo, mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, akanileta huko.
Ezéchiel 33.21 Ezéchiel 32.1 Ezéchiel 37.1 Ezéchiel 3.22 Ezéchiel 3.14
2 Katika maono ya Mungu alinileta mpaka nchi ya Israeli, akaniweka juu ya mlima mrefu sana, ambao juu yake palikuwapo kana kwamba ni umbo la mji upande wa kusini.
Ezéchiel 1.1 Daniel 7.7 Daniel 7.1 Ezéchiel 8.3 1 Chroniques 28.12
3 Akanileta huko, na tazama, alikuwapo mtu, ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba, naye alikuwa na uzi wa kitani mkononi mwake, na mwanzi wa kupimia; akasimama karibu na lango.
Ezéchiel 47.3 Apocalypse 11.1 Ezéchiel 1.7 Apocalypse 1.15 Zacharie 2.1-2.2
4 Mtu yule akaniambia, Mwanadamu, tazama kwa macho yako, sikia kwa masikio yako, ukaweke moyoni mwako, yote nitakayokuonyesha; maana umeletwa hapa kusudi nikuonyeshe haya; tangaza habari ya yote utakayoyaona kwa nyumba ya Israeli.
Ezéchiel 44.5 Jérémie 26.2 Ezéchiel 43.10 Ezéchiel 2.7-2.8 Esaïe 21.10
5 Na, tazama, kulikuwa na ukuta nje ya nyumba pande zote, na katika mkono wa mtu yule mwanzi wa kupimia, urefu wake dhiraa sita, kila dhiraa, dhiraa na shubiri; basi akaupima upana wa jengo lile, mwanzi mmoja, na urefu wake, mwanzi mmoja.
Ezéchiel 42.20 Esaïe 26.1 Apocalypse 21.12 Deutéronome 3.11 Psaumes 125.2
6 Kisha akaenda mpaka lango lielekealo upande wa mashariki, akapanda madaraja yake; akakipima kizingiti cha lango; upana wake mwanzi mmoja; na kizingiti cha pili, upana wake mwanzi mmoja.
Ezéchiel 43.1 Ezéchiel 8.16 Ezéchiel 11.1 Ezéchiel 40.20 Ezéchiel 43.8
7 Na kila chumba, upana wake mwanzi mmoja, na urefu wake mwanzi mmoja; na nafasi iliyokuwa kati ya vyumba ni dhiraa tano; na kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi wa lango lililoielekea nyumba, mwanzi mmoja.
Ezéchiel 40.36 1 Chroniques 9.26 Esdras 8.29 2 Chroniques 31.11 2 Chroniques 3.9
8 Akaupima na ukumbi wa lango lililoielekea nyumba, mwanzi mmoja.
9 Kisha akaupima ukumbi wa lango, dhiraa nane; na miimo yake, dhiraa mbili; na ukumbi wa lango uliielekea nyumba.
Ezéchiel 45.19
10 Na vyumba vya walinzi, vya lango upande wa mashariki, vilikuwa vitatu upande huu, na vitatu upande huu; vyote vitatu vya kipimo kimoja; nayo miimo ilikuwa na kipimo kimoja, upande huu na upande huu.
11 Akaupima upana wa mahali pa kuliingilia lango, dhiraa kumi; na urefu wa lango, dhiraa kumi na tatu.
12 Na mpaka, mbele ya vile vyumba, dhiraa moja upande huu, na mpaka, dhiraa moja upande huu; na vile vyumba, dhiraa sita upande huu, na dhiraa sita upande huu.
13 Akalipima lango, toka paa la chumba kimoja hata paa la chumba cha pili, upana wa dhiraa ishirini na tano; mlango mmoja ukielekea mlango wa pili.
14 Akafanya miimo pia, dhiraa sitini; na uwanda uliufikilia mwimo, lango lile likizungukwa pande zote.
Exode 27.9 Ezéchiel 8.7 Ezéchiel 42.1 Psaumes 100.4 1 Chroniques 28.6
15 Na toka mahali palipo mbele ya lango, penye maingilio yake, hata mahali palipo mbele ya ukumbi wa ndani ya lango, dhiraa hamsini.
16 Na kwa vile vyumba palikuwa na madirisha yaliyofungwa, na kwa miimo yake ndani ya lango pande zote, na kwa matao yake vivyo hivyo; na madirisha yalikuwako, pande zote upande wa ndani, tena palikuwa na mitende juu ya kila mwimo.
1 Rois 6.4 2 Chroniques 3.5 Ezéchiel 41.26 1 Rois 6.32 1 Rois 6.29
17 Ndipo akanileta mpaka ua wa nje, na tazama, palikuwa na vyumba, na sakafu iliyofanyizwa kwa ule ua pande zote; vyumba thelathini vilikuwako juu ya sakafu ile.
Ezéchiel 42.1 Apocalypse 11.2 1 Chroniques 23.28 2 Chroniques 31.11 1 Chroniques 9.26
18 Na ile sakafu ilikuwa kando ya malango, urefu wake sawasawa na urefu wa malango, yaani, sakafu ya chini.
19 Kisha akaupima upana, toka mahali palipokuwa mbele ya lango la chini hata mahali palipokuwa mbele ya ua wa ndani, nje yake, dhiraa mia upande wa mashariki, na upande wa kaskazini.
Ezéchiel 40.27 Ezéchiel 40.23 Ezéchiel 46.1-46.2
20 Nalo lango la ua wa nje, lililoelekea kaskazini, akalipima urefu wake, na upana wake.
Ezéchiel 40.6
21 Na vyumba vyake vya walinzi vilikuwa vitatu upande huu, na vitatu upande huu; na miimo yake, na matao yake, kipimo chake ni sawasawa na kipimo cha lango la kwanza; urefu wake dhiraa hamsini, na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Ezéchiel 40.29-40.30 Ezéchiel 40.25-40.26 Ezéchiel 40.10-40.16 Ezéchiel 40.7-40.8 Ezéchiel 40.34
22 Na madirisha yake, na matao yake, na mitende yake, kipimo chake ni sawasawa na kipimo cha lango lililoelekea upande wa mashariki; nao hupanda kwa madaraja saba; na matao yake yalikuwa mbele yake.
Ezéchiel 40.31 Ezéchiel 40.37 Ezéchiel 40.16 Ezéchiel 40.49 Ezéchiel 40.6
23 Na ule ua wa ndani ulikuwa na lango lililoelekea lile lango la pili, upande wa kaskazini, na upande wa mashariki; akapima toka lango hata lango, dhiraa mia.
Ezéchiel 40.19 Ezéchiel 40.27-40.28 Exode 38.9-38.12 Ezéchiel 40.44 Exode 27.9-27.18
24 Akanileta mpaka upande wa kusini, na tazama, lango lililoelekea kusini; akaipima miimo yake, na matao yake, sawasawa na vipimo hivyo.
Ezéchiel 40.20-40.21 Ezéchiel 46.9 Ezéchiel 40.6 Ezéchiel 40.35-40.36 Ezéchiel 40.28-40.29
25 Tena palikuwa na madirisha ndani yake, na katika matao yake pande zote kama madirisha hayo; urefu wake dhiraa hamsini, na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Ezéchiel 40.33 Ezéchiel 40.21-40.22 Ezéchiel 40.29 Ezéchiel 40.16 1 Corinthiens 13.12
26 Tena palikuwa na madaraja saba ya kulipandia, na matao yake yalikuwa mbele yake; nalo lilikuwa na mitende, mmoja upande huu, na mmoja upande huu, juu ya miimo yake.
Ezéchiel 40.22 Ezéchiel 40.16 Ezéchiel 40.6 Cantique 7.7-7.8 Ezéchiel 40.29
27 Tena ua wa ndani ulikuwa na lango, lililoelekea kusini; akapima toka lango hata lango, kwa kuelekea upande wa kusini, dhiraa mia.
Ezéchiel 40.23 Ezéchiel 40.32 Ezéchiel 40.19 Ezéchiel 40.47
28 Kisha akanileta mpaka ua wa ndani karibu na lango lililoelekea kusini; akalipima lango la kusini kwa vipimo vivyo hivyo;
Ezéchiel 40.35 Ezéchiel 40.32
29 navyo vyumba vyake vya walinzi, na miimo yake, na matao yake, sawasawa na vipimo hivyo; tena palikuwa na madirisha ndani yake, na katika matao yake pande zote; urefu wake dhiraa hamsini, na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Ezéchiel 40.25 Ezéchiel 40.7 Ezéchiel 40.16 Ezéchiel 40.10 Jérémie 36.10
30 Tena palikuwa na matao pande zote, urefu wake dhiraa ishirini na tano na upana wake dhiraa tano.
Ezéchiel 40.21 Ezéchiel 40.36 Ezéchiel 40.33 Ezéchiel 40.25 Ezéchiel 40.29
31 Na matao yake yaliuelekea ua wa nje, na mitende ilikuwa juu ya miimo yake; palikuwa na madaraja manane ya kuupandia.
Ezéchiel 40.26 Ezéchiel 40.34 Ezéchiel 40.22 Ezéchiel 40.37
32 Akanileta mpaka ua wa ndani ulioelekea upande wa mashariki, akalipima lango kwa vipimo vivyo hivyo;
Ezéchiel 40.28-40.31 Ezéchiel 40.35
33 navyo vyumba vyake vya walinzi, na miimo yake, na matao yake, kwa vipimo hivyo; tena palikuwa na madirisha ndani yake, na katika matao yake pande zote; urefu wake dhiraa hamsini, na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Ezéchiel 40.21 Ezéchiel 40.36 Ezéchiel 40.25
34 Na matao yake yaliuelekea ua wa nje; na mitende ilikuwa juu ya miimo yake, upande huu na upande huu; tena palikuwa na madaraja manane ya kuupandia.
Ezéchiel 40.22 Ezéchiel 40.37 Ezéchiel 40.31 Ezéchiel 40.49 Ezéchiel 40.26
35 Akanileta mpaka lango lililoelekea upande wa kaskazini; akalipima kwa vipimo vivyo hivyo;
Ezéchiel 47.2 Ezéchiel 44.4 Ezéchiel 40.32 Ezéchiel 40.27
36 vyumba vyake vya walinzi, na miimo yake, na matao yake; tena palikuwa na madirisha ndani yake pande zote; urefu wake dhiraa hamsini, na upana wake dhiraa ishirini na tano.
Ezéchiel 40.29 Ezéchiel 40.21 Ezéchiel 40.16 Ezéchiel 40.7
37 Na miimo yake iliuelekea ua wa nje; na mitende ilikuwa juu ya miimo yake, upande huu na upande huu; tena palikuwa na madaraja manane ya kuupandia.
Ezéchiel 40.34 Ezéchiel 40.31
38 Na chumba, pamoja na lango lake, kilikuwa karibu na miimo ya malango; ndiko walikoiosha sadaka ya kuteketezwa.
2 Chroniques 4.6 Lévitique 8.21 Ezéchiel 42.13 1 Rois 6.8 Ezéchiel 40.12
39 Na katika ukumbi wa lango palikuwa na meza mbili upande huu, na meza mbili upande huu, ili kuichinja sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya dhambi, na sadaka ya hatia.
Ezéchiel 46.2 Lévitique 4.2-4.3 Lévitique 1.3-1.17 Malachie 1.7 Luc 22.30
40 Na upande mmoja, nje, penye madaraja ya kuliingia lango lililoelekea kaskazini, palikuwa na meza mbili; na upande wa pili, ulio wa ukumbi wa lango hilo, palikuwa na meza mbili.
41 Palikuwa na meza nne upande huu, na meza nne upande huu, karibu na lango; meza nane ambazo juu yake walizichinja sadaka.
Ezéchiel 40.39-40.40
42 Tena palikuwa na meza nne kwa sadaka za kuteketezwa, za mawe yaliyochongwa; urefu wake dhiraa moja na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja; juu yake waliviweka vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na sadaka.
Ezéchiel 40.39 Exode 20.25
43 Tena hizo kulabu, ambazo urefu wake ni shubiri, zilifungwa ndani pande zote; na juu ya meza hizo ilikuwako nyama ya matoleo.
Lévitique 1.6 Lévitique 1.8 Lévitique 8.20
44 Tena nje ya lango la ndani palikuwa na vyumba kwa waimbaji, katika ua wa ndani, uliokuwa kando ya lango lililoelekea kaskazini, navyo vilikabili upande wa kusini; na kimoja kando ya lango lililoelekea upande wa mashariki, kilikabili upande wa kaskazini.
1 Chroniques 6.31-6.32 Ezéchiel 40.23 Ezéchiel 40.27 1 Chroniques 16.41-16.43 Ephésiens 5.19
45 Akaniambia, Chumba hiki kinachokabili upande wa kusini ni kwa makuhani, yaani, hao walinzi wa malindo ya nyumba.
1 Chroniques 9.23 Psaumes 134.1 Lévitique 8.35 Nombres 18.5 Nombres 3.32
46 Nacho chumba kinachokabili upande wa kaskazini ni kwa makuhani, walinzi wa malindo ya madhabahu; hao ni wana wa Sadoki, ambao miongoni mwa wana wa Lawi wamkaribia Bwana, ili kumtumikia.
Ezéchiel 44.15 1 Rois 2.35 Ezéchiel 43.19 Nombres 16.5 Nombres 18.5
47 Akaupima huo ua, na urefu wake ulikuwa dhiraa mia, na upana wake dhiraa mia, mraba; nayo dhabahu ilikuwa mbele ya nyumba.
Ezéchiel 40.23 Ezéchiel 40.19 Ezéchiel 40.27
48 Ndipo akanileta mpaka ukumbi wa nyumba, akapima kila mwimo wa ukumbi, dhiraa tano upande huu, na dhiraa tano upande huu; na upana wa lango ulikuwa dhiraa tatu upande huu, na dhiraa tatu upande huu.
1 Rois 6.3 2 Chroniques 3.4
49 Urefu wa ukumbi ulikuwa dhiraa ishirini, na upana wake dhiraa kumi na moja; karibu na madaraja ambayo waliupandia; tena palikuwa na nguzo karibu na miimo, moja upande huu, na moja upande huu.
1 Rois 7.15-7.21 Ezéchiel 40.31 Apocalypse 3.12 Ezéchiel 40.37 Ezéchiel 40.34

Cette Bible est dans le domaine public.