Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 48.2
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Moab

1 Habari za Moabu. Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Ole wake Nebo! Kwa maana umeharibika; Kiriathaimu umeaibishwa, umetwaliwa; Misgabu umeaibishwa, nao umebomolewa.
Nombres 32.37-32.38 Nombres 32.3 Jérémie 48.22-48.23 Jérémie 25.21 Amos 2.1-2.2
2 Sifa za Moabu haziko tena; katika Heshboni wameazimia mabaya juu yake, Haya! Njoni, na tumkatilie mbali asiwe taifa. Wewe nawe, Ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
Esaïe 16.14 Nombres 32.37 Jérémie 31.36 Esaïe 15.1 Jérémie 48.45
3 Sauti ya kilio toka Horonaimu, Ya kutekwa na uharibifu mkuu.
Esaïe 15.5 Jérémie 48.34 Jérémie 48.5 Esaïe 15.8 Esaïe 15.2
4 Moabu umeharibika; Wadogo wake wamewasikiza watu kilio.
Nombres 21.27-21.30 Psaumes 137.9 Esther 8.11
5 Kwa maana watu wapandapo huko Luhithi Watapanda wasiache kulia; Nao watu watelemkapo huko Horonaimu Wameisikia huzuni ya kilio cha uharibifu.
Esaïe 15.5
6 Haya! Kimbieni! Jiokoeni nafsi zenu! Mkawe kama mtu aliye mkiwa.
Jérémie 17.6 Jérémie 51.6 Job 30.3-30.7 Luc 3.7 Matthieu 24.16-24.18
7 Maana, kwa kuwa umeyatumainia matendo yako, na hazina zako, wewe nawe utatwaliwa; na Kemoshi atatoka aende katika uhamisho, makuhani wake na wakuu wake pamoja.
Nombres 21.29 Jérémie 49.3 Jérémie 48.46 Jérémie 48.13 Psaumes 52.7
8 Naye mwenye kuteka nyara atakuja juu ya kila mji, wala hapana mji utakaookoka; bonde nalo litaangamia, nayo nchi tambarare itaharibiwa; kama Bwana alivyosema.
Jérémie 6.26 Josué 13.21 Jérémie 51.56 Jérémie 25.9 Ezéchiel 25.9
9 Mpe Moabu mabawa, apate kuruka na kwenda zake; na miji yake itakuwa ukiwa, isiwe na mtu wa kukaa ndani yake.
Psaumes 11.1 Jérémie 48.28 Esaïe 16.2 Jérémie 46.19 Sophonie 2.9
10 Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu; na alaaniwe auzuiaye upanga wake usimwage damu.
1 Rois 20.42 1 Samuel 15.3 1 Samuel 15.9 Juges 5.23 1 Samuel 15.13-15.35
11 Moabu amestarehe tangu ujana wake, naye ametulia juu ya sira zake, wala hakumiminwa kutoka chombo kimoja kutiwa chombo kingine, wala hakwenda kufungwa; kwa hiyo ladha yake anakaa nayo, wala harufu yake haikubadilika.
Sophonie 1.12 Zacharie 1.15 Nahum 2.2 Psaumes 73.4-73.8 Esaïe 24.3
12 Basi, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo nitampelekea wamiminao, nao watammimina, nao watamwaga vyote vilivyomo vyomboni mwake, na kuzivunja chupa zake vipande vipande.
Jérémie 14.3 Jérémie 25.34 Jérémie 48.8 Jérémie 25.9 Ezéchiel 25.9-25.10
13 Na Moabu ataona haya kwa ajili ya Kemoshi, kama nyumba ya Israeli ilivyoona haya kwa ajili ya Betheli, matumaini yao.
Jérémie 48.39 Osée 8.5-8.6 Esaïe 45.16 Juges 11.24 Jérémie 48.7
14 Mwasemaje ninyi, Sisi tu mashujaa, watu hodari wa vita.
Psaumes 33.16 Esaïe 10.16 Esaïe 10.13 Jérémie 9.23 Esaïe 16.6
15 Moabu ameharibika, na moshi wa miji yake umepanda; na vijana wake wateule wametelemka kwenda kuchinjwa, asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana wa majeshi.
Jérémie 50.27 Jérémie 46.18 Jérémie 51.57 Malachie 1.14 Esaïe 40.30-40.31
16 Msiba wa Moabu umefika karibu, Na mateso yake yanafanya haraka.
Esaïe 13.22 2 Pierre 2.3 Ezéchiel 12.23 Jérémie 1.12 Esaïe 16.13-16.14
17 Ninyi nyote mnaomzunguka, mlilieni, Nanyi nyote mlijuao jina lake, semeni, Jinsi ilivyovunjika fimbo ya enzi, Fimbo ile iliyokuwa nzuri!
Esaïe 9.4 Jérémie 48.31-48.33 Apocalypse 18.14-18.20 Ezéchiel 19.11-19.14 Jérémie 9.17-9.20
18 Ee binti ukaaye Diboni, Shuka toka utukufu wako, ukae katika kiu; Maana atekaye Moabu amepanda juu yako, Ameziharibu ngome zako.
Nombres 21.30 Esaïe 47.1 Esaïe 15.2 Josué 13.17 Jérémie 48.22
19 Wewe ukaaye Aroeri, Simama kando ya njia upeleleze; Mwulize mwanamume akimbiaye na mwanamke atorokaye, Sema, Imetendeka nini?
Deutéronome 2.36 1 Samuel 4.16 1 Samuel 4.13-4.14 2 Samuel 18.24-18.32 1 Chroniques 5.8
20 Moabu ameaibishwa, kwa maana amevunjika; Pigeni yowe na kulia; Tangazeni habari hii katika Arnoni, Ya kuwa Moabu ameharibika.
Esaïe 16.2 Esaïe 15.8 Nombres 21.26-21.28 Jérémie 48.1-48.5 Esaïe 16.7-16.11
21 Na hukumu imeifikilia nchi tambarare; juu ya Holoni, na juu ya Yasa, na juu ya Mefaathi;
Josué 13.18 Esaïe 15.4 Nombres 21.23 Jérémie 48.8 Sophonie 2.9
22 na juu ya Diboni, na juu ya Nebo, na juu ya Beth-diblathaimu;
Jérémie 48.18 Nombres 33.46 Ezéchiel 6.14 Jérémie 48.1 Nombres 32.34
23 na juu ya Kiriathaimu, na juu ya Beth-gamuli, na juu ya Beth-meoni;
Josué 13.17 Jérémie 48.1 Nombres 32.38 Josué 13.19 Genèse 14.5
24 na juu ya Keriothi, na juu ya Bozra, na juu ya miji yote ya nchi ya Moabu, iliyo mbali na iliyo karibu.
Amos 2.2 Jérémie 48.41 Josué 21.36 Deutéronome 4.43 Sophonie 2.8-2.10
25 Pembe ya Moabu imekatika, na mkono wake umevunjika, asema Bwana. Mlevyeni; kwa maana alijitukuza juu ya Bwana
Psaumes 75.10 Psaumes 10.15 Job 22.9 Zacharie 1.19-1.21 Lamentations 2.3
26 na Moabu atagaa-gaa katika matapiko yake, naye atadhihakiwa. Kwa maana Israeli, je! Hakuwa dhihaka kwako?
Jérémie 51.39 Esaïe 19.14 Esaïe 29.9 Jérémie 48.42 Daniel 5.23
27 Alionekana kati ya wevi? Maana kila umtajapo watikisa kichwa chako.
Jérémie 2.26 Michée 7.8-7.10 Sophonie 2.8 Lamentations 2.15-2.17 Ezéchiel 25.8
28 Enyi mkaao Moabu, iacheni miji, Enendeni kukaa majabalini; Mkawe kama njiwa afanyaye kioto chake Katika ubavu wa mdomo wa shimo.
Psaumes 55.6-55.7 Cantique 2.14 Juges 6.2 Esaïe 2.19 Jérémie 48.9
29 Tumesikia habari za kiburi cha Moabu; Ya kuwa ana kiburi kingi; Jeuri yake, na kiburi chake, na majivuno yake, Na jinsi alivyotakabari moyoni mwake.
Esaïe 16.6 Psaumes 138.6 Proverbes 18.12 Luc 14.11 Proverbes 8.13
30 Najua ghadhabu yake, asema Bwana, ya kuwa si kitu; majisifu yake hayakutenda neno lo lote.
Jérémie 50.36 Esaïe 16.6 Psaumes 33.10 Job 9.12-9.13 Esaïe 37.28-37.29
31 Kwa sababu hiyo nitampigia yowe Moabu, naam, nitapiga kelele kwa ajili ya Moabu yote; nitawaombolezea watu wa Kir-heresi.
Esaïe 15.5 2 Rois 3.25 Jérémie 48.36 Esaïe 16.7-16.11
32 Nitakulilia, Ee mzabibu wa Sibma, kwa vilio vipitavyo vilio vya Yazeri; matawi yako yalipita juu ya bahari, yalifika hata bahari ya Yazeri; atekaye nyara ameyaangukia matunda yako ya wakati wa jua, na mavuno yako ya zabibu.
Esaïe 16.8-16.9 Nombres 21.32 Josué 13.19 Jérémie 48.15 Josué 21.39
33 Furaha na shangwe zimeondoshwa, katika shamba lizaalo sana, na katika nchi ya Moabu; nami nimeikomesha divai katika mashinikizo; hapana mtu atakayekanyaga zabibu kwa shangwe; shangwe ile itakuwa si shangwe.
Aggée 2.16 Esaïe 5.10 Esaïe 32.9-32.14 Joël 1.12-1.13 Jérémie 25.9-25.10
34 Toka kilio cha Heshboni mpaka Eleale, naam, mpaka Yahasa, wametoa sauti zao, toka Soari mpaka Horonaimu, hata Eglath-shelishia; maana maji ya Nimrimu nayo yatakuwa ukiwa.
Esaïe 15.4-15.6 Nombres 32.3 Jérémie 48.2-48.3 Nombres 32.36-32.37 Deutéronome 34.3
35 Pamoja na hayo, asema Bwana, nitamkomesha katika Moabu mtu atoaye sadaka katika mahali pa juu, naye awafukiziaye uvumba miungu yake.
Esaïe 15.2 Esaïe 16.12 Jérémie 48.7 Jérémie 11.13 Nombres 28.14
36 Kwa sababu hiyo moyo wangu watoa sauti kama filimbi kwa ajili ya Moabu, na kwa ajili ya watu wa Kir-heresi, moyo wangu watoa sauti kama filimbi; kwa kuwa wingi aliojipatia umepotea.
Esaïe 15.7 Esaïe 16.11 Esaïe 15.5 Proverbes 18.11 Jérémie 17.11
37 Maana kila kichwa kina upaa, na ndevu zote zimenyolewa; mikono yote ina alama za chale, na viuno vyote vimevikwa nguo za magunia.
Jérémie 41.5 Esaïe 15.2-15.3 Genèse 37.34 Jérémie 47.5 Esaïe 20.2
38 Juu ya dari zote za nyumba za Moabu, na katika njia kuu zake, pana maombolezo, kila mahali; kwa maana nimevunja Moabu kama chombo kisichopendeza, asema Bwana.
Jérémie 22.28 Jérémie 25.34 Esaïe 22.1 Apocalypse 2.27 2 Timothée 2.20-2.21
39 Jinsi alivyovunjika! Pigeni yowe! Jinsi Moabu alivyogeuza kisogo kwa haya! Hivyo ndivyo Moabu atakavyokuwa dhihaka, na sababu ya kuwashangaza watu wote wamzungukao.
Lamentations 2.1 Apocalypse 18.15-18.16 Esaïe 20.4-20.6 Ezéchiel 26.16-26.18 Jérémie 48.26-48.27
40 Maana Bwana asema hivi, Tazama, ataruka kama tai, na kutandaza mabawa yake juu ya Moabu.
Esaïe 8.8 Deutéronome 28.49 Jérémie 49.22 Ezéchiel 17.3 Osée 8.1
41 Miji imetwaliwa, ngome zimeshambuliwa, na mioyo ya mashujaa wa Moabu siku hiyo itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wake.
Esaïe 13.8 Esaïe 21.3 Jérémie 6.24 Jérémie 30.6 Michée 4.9-4.10
42 Na Moabu ataangamizwa, asiwe taifa tena, kwa sababu alijitukuza juu ya Bwana.
Jérémie 48.2 Esaïe 37.23 Esaïe 7.8 Psaumes 83.4-83.8 Apocalypse 13.6
43 Hofu, na shimo, na mtego, zaja juu yako, Ee mwenyeji wa Moabu, asema Bwana.
Lamentations 3.47 Esaïe 24.17-24.18 Psaumes 11.6 Deutéronome 32.23-32.25
44 Aikimbiaye hofu ataanguka shimoni; na yeye atokaye shimoni atanaswa kwa mtego; maana nitaleta juu yake, yaani, juu ya Moabu, mwaka wa kujiliwa kwake, asema Bwana.
Jérémie 11.23 1 Rois 19.17 Amos 5.19 Jérémie 46.21 Jérémie 23.12
45 Wamekimbia, wasio na nguvu Wanasimama chini ya kivuli cha Heshboni; Ila moto umetoka katika Heshboni, Na mwali wa moto toka kati ya Sihoni Nao umekula pembe ya Moabu, Na utosi wa kichwa wa watu wapigao kelele.
Nombres 24.17 Nombres 21.28 Nombres 21.26 Matthieu 21.42 Zacharie 10.4
46 Ole wako! Ee Moabu, Watu wa Kemoshi wamepotea; Maana wana wako wamechukuliwa mateka, Na binti zako wamekwenda utumwani.
Nombres 21.29 1 Rois 11.7 Juges 11.24 Jérémie 48.13 Jérémie 48.7
47 Lakini nitawarudisha watu wa Moabu walio utumwani, siku za mwisho, asema Bwana. Hukumu ya Moabu imefikilia hapa.
Jérémie 49.39 Jérémie 49.6 Osée 3.5 Esaïe 19.18-19.23 Daniel 10.14

Cette Bible est dans le domaine public.