Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 49.16
Bible en Swahili de l’est


Le Sauveur d’Israël et des nations

1 Nisikilizeni, enyi visiwa; tegeni masikio yenu, enyi kabila za watu mlio mbali sana; Bwana ameniita tangu tumboni; toka tumbo la mama yangu amenitaja jina langu.
Jérémie 1.5 Esaïe 44.2 Galates 1.15 Luc 1.15 Luc 1.31
2 Naye anifanya kinywa changu kuwa kama upanga mkali; katika kivuli cha mkono wake amenisitiri; naye amenifanya kuwa mshale uliosuguliwa; katika podo lake amenificha;
Esaïe 11.4 Apocalypse 1.16 Hébreux 4.12 Esaïe 51.16 Osée 6.5
3 akaniambia; Wewe u mtumishi wangu, Israeli, ambaye katika wewe nitatukuzwa.
Esaïe 44.23 Zacharie 3.8 1 Pierre 2.9 Esaïe 42.1 Esaïe 52.13
4 Lakini nikasema, Nimejitaabisha bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida; lakini hakika hukumu yangu ina Bwana, na thawabu yangu ina Mungu wangu.
Esaïe 53.10-53.12 Esaïe 65.23 Esaïe 35.4 Matthieu 23.37 Philippiens 2.9-2.10
5 Na sasa Bwana asema hivi, yeye aliyeniumba tangu tumboni niwe mtumishi wake, ili nimletee Yakobo tena, na Israeli wakusanyike mbele zake tena; (maana mimi nimepata heshima mbele ya macho ya Bwana, na Mungu wangu amekuwa nguvu zangu);
1 Pierre 3.22 Matthieu 17.5 Matthieu 28.18 Romains 15.8 Esaïe 50.4
6 naam, asema hivi, Ni neno dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kuziinua kabila za Yakobo, na kuwarejeza watu wa Israeli waliohifadhiwa; zaidi ya hayo nitakutoa uwe nuru ya mataifa, upate kuwa wokovu wangu hata miisho ya dunia.
Actes 13.47 Luc 2.32 Esaïe 42.6 Luc 24.46-24.47 Psaumes 98.2-98.3
7 Bwana, mkombozi wa Israeli, Mtakatifu wake, amwambia hivi yeye anayedharauliwa na wanadamu; yeye anayechukiwa na taifa hili; yeye aliye mtumishi wao watawalao; Wafalme wataona, watasimama; wakuu nao watasujudu; kwa sababu ya Bwana aliye mwaminifu, Mtakatifu wa Israeli aliyekuchagua
Matthieu 26.67 1 Pierre 2.4 Esaïe 53.3 Psaumes 22.6-22.8 Esaïe 52.15
8 Bwana asema hivi, Wakati uliokubalika nimekujibu, na siku ya wokovu nimekusaidia; nami nitakuhifadhi, nitakutoa uwe agano la watu hawa, ili kuiinua nchi hii, na kuwarithisha urithi uliokuwa ukiwa;
2 Corinthiens 6.2 Esaïe 42.6 Psaumes 69.13 Esaïe 61.4 Esaïe 50.7-50.9
9 kuwaambia waliofungwa, Haya, tokeni; na hao walio katika giza, Jionyesheni. Watajilisha katika njia, na juu ya majabali watapata malisho.
Esaïe 42.7 Esaïe 42.16 Esaïe 61.1 Esaïe 41.18 Luc 4.18
10 Hawataona njaa, wala hawataona kiu; hari haitawapiga, wala jua; kwa maana yeye aliyewarehemu atawatangulia, naam, karibu na chemchemi za maji atawaongoza.
Apocalypse 7.16-7.17 Esaïe 40.11 Esaïe 54.10 Jérémie 31.9 Psaumes 23.2-23.4
11 Nami nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na njia kuu zangu zitatukuzwa zote.
Esaïe 11.16 Esaïe 62.10 Esaïe 43.19 Esaïe 40.3-40.4 Psaumes 107.4
12 Tazama, hawa watakuja kutoka mbali; na tazama, hawa kutoka kaskazini, na kutoka magharibi, na hawa kutoka nchi ya Sinimu.
Esaïe 43.5-43.6 Luc 13.29 Zacharie 8.20-8.23 Esaïe 66.19-66.20 Apocalypse 11.15
13 Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi; Pazeni sauti ya kuimba, enyi milima; Kwa kuwa Bwana amewafariji watu wake, Naye atawahurumia watu wake walioteswa.
Esaïe 44.23 Esaïe 51.3 Jérémie 31.13 Psaumes 96.11-96.13 Esaïe 42.10-42.11
14 Bali Sayuni alisema, YEHOVA ameniacha, Bwana amenisahau.
Esaïe 40.27 Romains 11.1-11.5 Psaumes 31.22 Lamentations 5.20 Psaumes 89.38-89.46
15 Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.
Esaïe 44.21 Osée 11.1 Lamentations 4.3 Lamentations 4.10 Matthieu 7.11
16 Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.
Exode 13.9 Psaumes 48.12-48.13 Esaïe 60.18 Apocalypse 21.10-21.21 Esaïe 26.1
17 Watoto wako wafanya haraka, hao wakuharibuo, nao waliokufanya ukiwa, watatoka kwako.
Esaïe 51.13 Esaïe 51.22-51.23 Esaïe 62.5 Néhémie 2.4-2.9 Néhémie 2.17
18 Inua macho yako, ukatazame pande zote; hao wote wanajikusanya na kukujia. Kama niishivyo, asema Bwana, hakika utajivika na hao wote, kama kwa uzuri, nawe utajifungia hao, kama bibi arusi.
Esaïe 54.9 Esaïe 54.1-54.3 Esaïe 54.7 Esaïe 61.10 Esaïe 49.12
19 Maana katika habari za mahali pako palipokuwa ukiwa, pasipokaliwa na watu, na nchi yako iliyoharibika hakika sasa utakuwa mwembamba usiwatoshe wenyeji wako, nao waliokumeza watakuwa mbali.
Zacharie 10.10 Osée 1.10-1.11 Psaumes 56.1-56.2 Esaïe 54.1-54.2 Esaïe 49.25-49.26
20 Watoto ulionyang’anywa watasema masikioni mwako, Mahali hapa ni pembamba, hapanitoshi; nipe nafasi nipate kukaa.
Esaïe 51.3 Josué 17.14-17.16 Matthieu 3.9 Esaïe 60.4 2 Rois 6.1
21 Ndipo utasema moyoni mwako, Ni nani aliyenizalia watoto hawa, na mimi nimefiwa na watoto wangu, nami ni peke yangu, nimehamishwa, ninatanga-tanga huko na huku? Tena ni nani aliyewalea hawa? Tazama, naliachwa peke yangu; hawa je! Walikuwa wapi?
Esaïe 51.17-51.20 Romains 11.26-11.31 Esaïe 5.13 Esaïe 52.2 Matthieu 24.29-24.30
22 Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, nitawainulia mataifa mkono wangu, na kuwatwekea kabila za watu bendera yangu; nao wataleta wana wako vifuani mwao, na binti zako watachukuliwa mabegani mwao.
Esaïe 11.10-11.12 Psaumes 72.17 Esaïe 42.1-42.4 Esaïe 49.12 Esaïe 66.20
23 Na wafalme watakuwa baba zako za kulea, na malkia zao mama zako za kulea; watainama mbele yako kifudifudi, na kuramba mavumbi ya miguu yako; nawe utajua ya kuwa mimi ni Bwana, tena waningojeao hawatatahayarika.
Esaïe 60.16 Michée 7.17 Esaïe 60.14 Esaïe 60.3 Esaïe 45.14
24 Je! Aliye hodari aweza kunyang’anywa mateka yake, au jeshi lao waliofungwa halali wataokoka?
Matthieu 12.29 Jérémie 25.11-25.14 Ezéchiel 37.11 Jérémie 25.6-25.9 Esaïe 42.22
25 Naam, Bwana asema hivi, Hata jeshi la wafungwa wake aliye hodari watapokonywa mikononi mwake, na mateka yake aliye jabari wataokoka; kwa maana nitateta na yeye atetaye nawe, nami nitawaletea wana wako wokovu.
Esaïe 35.4 Jérémie 50.33-50.34 Esaïe 54.15-54.17 Esaïe 41.11-41.12 Romains 8.31-8.39
26 Na hao wanaokuonea nitawalisha nyama yao wenyewe, nao watalewa kwa kuinywa damu yao wenyewe, kama kwa mvinyo mpya; na wote wenye mwili watajua ya kuwa mimi, Bwana, ni mwokozi wako, na Mkombozi wako ni Mwenye enzi wa Yakobo.
Esaïe 9.20 Ezéchiel 39.7 Apocalypse 16.6 Apocalypse 15.3-15.4 Apocalypse 14.20

Cette Bible est dans le domaine public.