Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 8.9
Bible en Swahili de l’est


L’activité de la sagesse

1 Je! Hekima halii? Ufahamu hatoi sauti yake?
Romains 15.18-15.21 Matthieu 3.3 Actes 22.21 Proverbes 9.1-9.3 Marc 16.15-16.16
2 Juu ya mahali palipoinuka karibu na njia, Penye njia panda, ndipo asimamapo.
Proverbes 9.14 Proverbes 9.3
3 Karibu na malango, mahali pa kuingia mjini, Mahali pa kuyaingilia malango anapiga kelele.
Matthieu 22.9 Job 29.7 Luc 14.21-14.23 Actes 5.20 Jean 18.20
4 Enyi watu, nawaita ninyi; Na sauti yangu ni kwa wanadamu.
Apocalypse 22.17 Colossiens 1.23 Matthieu 11.15 Colossiens 1.28 Psaumes 49.1-49.3
5 Enyi wajinga, fahamuni werevu, Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.
Proverbes 1.22 Proverbes 1.4 Apocalypse 3.17-3.18 Actes 26.18 Psaumes 19.7
6 Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri, Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.
Matthieu 7.28-7.29 Proverbes 23.16 Proverbes 22.20-22.21 Psaumes 19.7-19.11 Proverbes 4.20-4.22
7 Maana kinywa changu kitasema kweli, Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.
Jean 8.14 Job 36.4 Psaumes 37.30 Apocalypse 3.14 Jean 18.37
8 Maneno yote ya kinywa changu yana haki; Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi.
Deutéronome 32.5 Proverbes 8.13 Jean 7.46 Esaïe 45.23 Esaïe 63.1
9 Yote humwelea yule afahamuye, Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.
Proverbes 14.6 1 Corinthiens 2.14-2.15 Proverbes 18.1-18.2 Jean 6.45 Psaumes 19.7-19.8
10 Pokea mafundisho yangu, wala si fedha, Na maarifa kuliko dhahabu safi.
Ecclésiaste 7.11 Psaumes 119.72 Psaumes 119.127 Proverbes 23.23 Proverbes 3.13-3.15
11 Maana hekima ni bora kuliko marijani; Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.
Psaumes 19.10 Job 28.15-28.19 Proverbes 16.16 Proverbes 3.14-3.15 Matthieu 16.26
12 Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa kao langu; Natafuta maarifa na busara.
Proverbes 1.4 Ephésiens 1.11 1 Rois 7.14 Psaumes 104.24 Esaïe 28.26
13 Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.
Psaumes 97.10 Proverbes 16.6 1 Thessaloniciens 5.22 1 Samuel 2.3 1 Pierre 5.5
14 Shauri ni langu, na maarifa yaliyo sahihi; Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu.
Ecclésiaste 7.19 Esaïe 9.6 Romains 11.33-11.34 1 Corinthiens 1.30 Jean 1.9
15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki.
Daniel 2.21 Romains 13.1 Apocalypse 19.16 Matthieu 28.18 Esaïe 32.1-32.2
16 Kwa msaada wangu wakuu hutawala, Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.
17 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Jean 14.21 Psaumes 91.14 1 Samuel 2.30 Jean 14.23 Jacques 1.5
18 Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia.
Matthieu 6.33 Proverbes 3.16 1 Timothée 6.17-6.19 Luc 16.11-16.12 2 Corinthiens 6.10
19 Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, Na faida yangu hupita fedha iliyo teule.
Proverbes 3.14 Proverbes 10.20 Proverbes 8.10 Ecclésiaste 7.12
20 Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.
Jean 10.27-10.28 Deutéronome 5.32 Proverbes 4.25-4.27 Proverbes 3.6 Psaumes 23.3
21 Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao.
Romains 8.17 Matthieu 25.46 Proverbes 6.31 Proverbes 1.13 Apocalypse 21.7
22 Bwana alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake, Kabla ya matendo yake ya kale.
Colossiens 1.17 Jean 1.1-1.2 Proverbes 3.19 Psaumes 104.24 Job 28.26-28.28
23 Nalitukuka tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia.
Jean 17.24 Psaumes 2.6 Michée 5.2 Jean 17.5 Ephésiens 1.10-1.11
24 Wakati visipokuwako vilindi nalizaliwa, Wakati zisipokuwako chemchemi zilizojaa maji.
Proverbes 3.20 Psaumes 2.7 Jean 5.20 Jean 3.16 1 Jean 4.9
25 Kabla milima haijawekwa imara, Kabla ya vilima nalizaliwa.
Psaumes 90.2 Job 38.4-38.11 Hébreux 1.10 Job 15.7-15.8 Psaumes 102.25-102.28
26 Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makonde Wala chanzo cha mavumbi ya dunia;
Genèse 1.1-1.31
27 Alipozithibitisha mbingu nalikuwako; Alipopiga duara katika uso wa bahari;
Esaïe 40.22 Proverbes 3.19 Esaïe 40.11 Psaumes 136.5 Job 26.10
28 Alipofanya imara mawingu yaliyo juu; Chemchemi za bahari zilipopata nguvu;
29 Alipoipa bahari mpaka wake, Kwamba maji yake yasiasi amri yake; Alipoiagiza misingi ya nchi;
Psaumes 104.9 Genèse 1.9-1.10 Jérémie 5.22 Psaumes 33.7 Psaumes 104.5
30 Ndipo nilipokuwa pamoja naye, kama stadi wa kazi; Nikawa furaha yake kila siku; Nikifurahi daima mbele zake;
Jean 1.1-1.3 Esaïe 42.1 Matthieu 3.17 Colossiens 1.13 Jean 16.28
31 Nikiifurahia dunia inayokaliwa na watu; Na furaha yangu ilikuwa pamoja na wanadamu.
Psaumes 16.3 Jean 13.1 Psaumes 40.6-40.8 2 Corinthiens 8.9 Jean 4.34
32 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa; Maana heri hao wazishikao amri zangu.
Luc 11.28 Psaumes 119.1-119.2 Psaumes 128.1 Proverbes 5.7 Proverbes 7.24
33 Sikieni mafundisho, mpate hekima, Wala msiikatae.
Proverbes 4.1 Proverbes 1.8 Proverbes 5.1 Proverbes 1.2-1.3 Psaumes 81.11-81.12
34 Ana heri mtu yule anisikilizaye, Akisubiri sikuzote malangoni pangu, Akingoja penye vizingiti vya milango yangu.
Proverbes 3.13 Proverbes 2.3-2.4 Actes 17.11-17.12 Jacques 1.22-1.25 Jean 8.31-8.32
35 Maana yeye anionaye mimi aona uzima, Naye atapata kibali kwa Bwana.
Proverbes 12.2 Colossiens 3.3 Proverbes 4.22 Proverbes 1.33 Jean 3.36
36 Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe, Na wao wanichukiao hupenda mauti.
Proverbes 15.32 Proverbes 1.31 Proverbes 20.2 1 Corinthiens 16.22 Hébreux 10.29

Cette Bible est dans le domaine public.