Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 8
Bible en Swahili de l’est


L’activité de la sagesse

1 Je! Hekima halii? Ufahamu hatoi sauti yake?
Romains 15.18-15.21 Esaïe 55.1-55.3 Luc 24.47 Matthieu 28.19-28.20 Marc 13.10
2 Juu ya mahali palipoinuka karibu na njia, Penye njia panda, ndipo asimamapo.
Proverbes 9.14 Proverbes 9.3
3 Karibu na malango, mahali pa kuingia mjini, Mahali pa kuyaingilia malango anapiga kelele.
Job 29.7 Luc 14.21-14.23 Matthieu 22.9 Jean 18.20 Actes 5.20
4 Enyi watu, nawaita ninyi; Na sauti yangu ni kwa wanadamu.
Apocalypse 22.17 2 Corinthiens 5.19-5.20 Psaumes 50.1 Tite 2.11-2.12 Jean 3.16
5 Enyi wajinga, fahamuni werevu, Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.
Proverbes 1.22 Apocalypse 3.17-3.18 Proverbes 1.4 Proverbes 9.4 Esaïe 42.13
6 Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri, Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.
Matthieu 7.28-7.29 Proverbes 2.6-2.7 Matthieu 5.2-5.12 Matthieu 13.35 Psaumes 49.3
7 Maana kinywa changu kitasema kweli, Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.
Jean 8.14 Psaumes 37.30 Job 36.4 Jean 1.17 Proverbes 16.12
8 Maneno yote ya kinywa changu yana haki; Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi.
Esaïe 45.23 Esaïe 63.1 Psaumes 12.6 Deutéronome 32.5 Proverbes 8.13
9 Yote humwelea yule afahamuye, Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.
Proverbes 14.6 Esaïe 35.8 Psaumes 25.12-25.14 Proverbes 15.24 Matthieu 13.11-13.12
10 Pokea mafundisho yangu, wala si fedha, Na maarifa kuliko dhahabu safi.
Psaumes 119.127 Ecclésiaste 7.11 Psaumes 119.72 Psaumes 119.162 2 Corinthiens 6.10
11 Maana hekima ni bora kuliko marijani; Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.
Proverbes 3.14-3.15 Psaumes 19.10 Job 28.15-28.19 Proverbes 16.16 Proverbes 4.5-4.7
12 Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa kao langu; Natafuta maarifa na busara.
Proverbes 1.4 Esaïe 55.8-55.9 Ephésiens 1.8 Exode 35.30-36.4 Colossiens 2.3
13 Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.
Psaumes 97.10 Proverbes 16.6 1 Thessaloniciens 5.22 1 Samuel 2.3 1 Pierre 5.5
14 Shauri ni langu, na maarifa yaliyo sahihi; Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu.
Ecclésiaste 7.19 Esaïe 9.6 Ecclésiaste 9.16-9.18 1 Corinthiens 1.24 Colossiens 2.3
15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki.
Romains 13.1 Daniel 2.21 Apocalypse 19.16 Matthieu 28.18 1 Samuel 9.17
16 Kwa msaada wangu wakuu hutawala, Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.
17 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Jean 14.21 1 Samuel 2.30 Psaumes 91.14 Jean 14.23 Jacques 1.5
18 Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia.
Proverbes 3.16 Matthieu 6.33 Matthieu 6.19-6.20 Jacques 2.5 Apocalypse 3.18
19 Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, Na faida yangu hupita fedha iliyo teule.
Proverbes 3.14 Proverbes 8.10 Proverbes 10.20 Ecclésiaste 7.12
20 Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.
Jean 10.27-10.28 Deutéronome 5.32 Esaïe 55.4 Esaïe 49.10 Psaumes 32.8
21 Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao.
Apocalypse 21.7 1 Pierre 1.4 Hébreux 10.34 Genèse 15.14 Jean 1.1-1.18
22 Bwana alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake, Kabla ya matendo yake ya kale.
Colossiens 1.17 Jean 1.1-1.2 Psaumes 104.24 Proverbes 3.19 Job 28.26-28.28
23 Nalitukuka tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia.
Jean 17.24 Psaumes 2.6 Michée 5.2 Ephésiens 1.10-1.11 Genèse 1.26
24 Wakati visipokuwako vilindi nalizaliwa, Wakati zisipokuwako chemchemi zilizojaa maji.
1 Jean 4.9 Genèse 1.2 Jean 1.14 Hébreux 1.5 Proverbes 3.20
25 Kabla milima haijawekwa imara, Kabla ya vilima nalizaliwa.
Psaumes 90.2 Job 15.7-15.8 Psaumes 102.25-102.28 Job 38.4-38.11 Hébreux 1.10
26 Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makonde Wala chanzo cha mavumbi ya dunia;
Genèse 1.1-1.31
27 Alipozithibitisha mbingu nalikuwako; Alipopiga duara katika uso wa bahari;
Esaïe 40.22 Proverbes 3.19 Psaumes 103.19 Jérémie 10.12 Hébreux 1.2
28 Alipofanya imara mawingu yaliyo juu; Chemchemi za bahari zilipopata nguvu;
29 Alipoipa bahari mpaka wake, Kwamba maji yake yasiasi amri yake; Alipoiagiza misingi ya nchi;
Psaumes 104.9 Genèse 1.9-1.10 Job 38.4-38.11 Jérémie 5.22 Psaumes 33.7
30 Ndipo nilipokuwa pamoja naye, kama stadi wa kazi; Nikawa furaha yake kila siku; Nikifurahi daima mbele zake;
Esaïe 42.1 Jean 1.1-1.3 Matthieu 3.17 Jean 12.28 Jean 1.18
31 Nikiifurahia dunia inayokaliwa na watu; Na furaha yangu ilikuwa pamoja na wanadamu.
Psaumes 16.3 Psaumes 40.6-40.8 Jean 13.1 Jean 4.34 2 Corinthiens 8.9
32 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa; Maana heri hao wazishikao amri zangu.
Psaumes 119.1-119.2 Luc 11.28 Psaumes 128.1 Proverbes 7.24 Psaumes 1.1-1.4
33 Sikieni mafundisho, mpate hekima, Wala msiikatae.
Proverbes 4.1 Proverbes 1.2-1.3 Proverbes 1.8 Proverbes 5.1 Romains 10.16-10.17
34 Ana heri mtu yule anisikilizaye, Akisubiri sikuzote malangoni pangu, Akingoja penye vizingiti vya milango yangu.
Proverbes 3.13 Psaumes 92.13 Proverbes 1.21 Proverbes 3.18 Psaumes 27.4
35 Maana yeye anionaye mimi aona uzima, Naye atapata kibali kwa Bwana.
Proverbes 12.2 Colossiens 3.3 1 Jean 5.11-5.12 Jean 3.16 Proverbes 3.13-3.18
36 Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe, Na wao wanichukiao hupenda mauti.
Proverbes 1.31 Proverbes 20.2 Proverbes 15.32 Actes 13.46 Hébreux 2.3

Cette Bible est dans le domaine public.