Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 8.31
Bible en Swahili de l’est


L’activité de la sagesse

1 Je! Hekima halii? Ufahamu hatoi sauti yake?
Romains 15.18-15.21 Proverbes 1.20-1.21 Actes 1.8 Esaïe 49.1-49.6 Jean 7.37
2 Juu ya mahali palipoinuka karibu na njia, Penye njia panda, ndipo asimamapo.
Proverbes 9.14 Proverbes 9.3
3 Karibu na malango, mahali pa kuingia mjini, Mahali pa kuyaingilia malango anapiga kelele.
Job 29.7 Luc 14.21-14.23 Matthieu 22.9 Jean 18.20 Actes 5.20
4 Enyi watu, nawaita ninyi; Na sauti yangu ni kwa wanadamu.
Apocalypse 22.17 Tite 2.11-2.12 Jean 3.16 1 Timothée 2.4-2.6 Colossiens 1.23
5 Enyi wajinga, fahamuni werevu, Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.
Proverbes 1.22 Proverbes 1.4 Apocalypse 3.17-3.18 Psaumes 94.8 Esaïe 55.1-55.3
6 Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri, Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.
Matthieu 7.28-7.29 Proverbes 4.2 1 Corinthiens 2.6-2.7 Colossiens 1.26 Job 33.1-33.3
7 Maana kinywa changu kitasema kweli, Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.
Jean 8.14 Job 36.4 Psaumes 37.30 Jean 8.45-8.46 Proverbes 29.27
8 Maneno yote ya kinywa changu yana haki; Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi.
Esaïe 45.23 Esaïe 63.1 Psaumes 12.6 Deutéronome 32.5 Proverbes 8.13
9 Yote humwelea yule afahamuye, Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.
Proverbes 14.6 Jean 7.17 Psaumes 119.98-119.100 Proverbes 18.15 Jacques 1.5
10 Pokea mafundisho yangu, wala si fedha, Na maarifa kuliko dhahabu safi.
Ecclésiaste 7.11 Psaumes 119.72 Psaumes 119.127 Proverbes 2.4-2.5 Proverbes 8.19
11 Maana hekima ni bora kuliko marijani; Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.
Psaumes 19.10 Job 28.15-28.19 Proverbes 16.16 Proverbes 3.14-3.15 Proverbes 20.15
12 Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa kao langu; Natafuta maarifa na busara.
Proverbes 1.4 Romains 11.33 2 Chroniques 13.14 1 Chroniques 28.12 Ephésiens 3.10
13 Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.
Psaumes 97.10 Proverbes 16.6 1 Thessaloniciens 5.22 Psaumes 101.3 Proverbes 4.24
14 Shauri ni langu, na maarifa yaliyo sahihi; Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu.
Ecclésiaste 7.19 Esaïe 9.6 Proverbes 24.5 Proverbes 2.6-2.7 Romains 11.33-11.34
15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki.
Romains 13.1 Daniel 2.21 Matthieu 28.18 Apocalypse 19.16 1 Rois 10.9
16 Kwa msaada wangu wakuu hutawala, Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.
17 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Jean 14.21 Psaumes 91.14 1 Samuel 2.30 Jean 14.23 Jacques 1.5
18 Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia.
Matthieu 6.33 Proverbes 3.16 Ephésiens 3.8 Philippiens 3.8-3.9 Psaumes 36.6
19 Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, Na faida yangu hupita fedha iliyo teule.
Proverbes 3.14 Proverbes 8.10 Proverbes 10.20 Ecclésiaste 7.12
20 Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.
Deutéronome 5.32 Jean 10.27-10.28 Jean 10.3 Esaïe 2.3 Proverbes 4.11-4.12
21 Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao.
Proverbes 8.18 Psaumes 16.11 Ephésiens 3.19-3.20 Proverbes 24.4 1 Samuel 2.8
22 Bwana alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake, Kabla ya matendo yake ya kale.
Colossiens 1.17 Jean 1.1-1.2 Psaumes 104.24 Proverbes 3.19 Job 28.26-28.28
23 Nalitukuka tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia.
Jean 17.24 Psaumes 2.6 Michée 5.2 Ephésiens 1.10-1.11 Genèse 1.26
24 Wakati visipokuwako vilindi nalizaliwa, Wakati zisipokuwako chemchemi zilizojaa maji.
Genèse 1.2 Jean 1.14 Hébreux 1.5 Proverbes 3.20 Psaumes 2.7
25 Kabla milima haijawekwa imara, Kabla ya vilima nalizaliwa.
Psaumes 90.2 Job 15.7-15.8 Psaumes 102.25-102.28 Job 38.4-38.11 Hébreux 1.10
26 Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makonde Wala chanzo cha mavumbi ya dunia;
Genèse 1.1-1.31
27 Alipozithibitisha mbingu nalikuwako; Alipopiga duara katika uso wa bahari;
Proverbes 3.19 Esaïe 40.22 Hébreux 1.2 Colossiens 1.16 Esaïe 40.11
28 Alipofanya imara mawingu yaliyo juu; Chemchemi za bahari zilipopata nguvu;
29 Alipoipa bahari mpaka wake, Kwamba maji yake yasiasi amri yake; Alipoiagiza misingi ya nchi;
Psaumes 104.9 Genèse 1.9-1.10 Job 38.4-38.11 Jérémie 5.22 Psaumes 33.7
30 Ndipo nilipokuwa pamoja naye, kama stadi wa kazi; Nikawa furaha yake kila siku; Nikifurahi daima mbele zake;
Esaïe 42.1 Jean 1.1-1.3 Matthieu 3.17 Jean 1.18 Colossiens 1.13
31 Nikiifurahia dunia inayokaliwa na watu; Na furaha yangu ilikuwa pamoja na wanadamu.
Psaumes 16.3 Psaumes 40.6-40.8 Jean 13.1 Jean 4.34 2 Corinthiens 8.9
32 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa; Maana heri hao wazishikao amri zangu.
Psaumes 119.1-119.2 Luc 11.28 Psaumes 128.1 Proverbes 7.24 Psaumes 1.1-1.4
33 Sikieni mafundisho, mpate hekima, Wala msiikatae.
Proverbes 4.1 Proverbes 1.8 Proverbes 5.1 Proverbes 1.2-1.3 Actes 7.35-7.37
34 Ana heri mtu yule anisikilizaye, Akisubiri sikuzote malangoni pangu, Akingoja penye vizingiti vya milango yangu.
Proverbes 3.13 Actes 2.42 Matthieu 7.24 Psaumes 84.10 Luc 1.6
35 Maana yeye anionaye mimi aona uzima, Naye atapata kibali kwa Bwana.
Proverbes 12.2 Colossiens 3.3 Jean 17.3 Philippiens 3.8 Jean 14.6
36 Bali anikosaye hujidhuru nafsi yake mwenyewe, Na wao wanichukiao hupenda mauti.
Proverbes 15.32 Proverbes 1.31 Proverbes 20.2 Ezéchiel 18.31 Proverbes 12.1

Cette Bible est dans le domaine public.