Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 16.31
Bible en Swahili de l’est


Organisation du service du tabernacle

1 Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
1 Chroniques 15.1 1 Chroniques 15.12 Esdras 6.16-6.18 2 Samuel 6.17-6.19 2 Chroniques 1.4
2 Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.
Hébreux 7.7 Josué 22.6 2 Samuel 6.18 Genèse 47.10 Luc 24.50-24.51
3 Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.
2 Chroniques 35.7-35.8 1 Pierre 4.9 Néhémie 8.10 Ezéchiel 45.17 2 Chroniques 30.24
4 Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;
Genèse 32.28 1 Rois 8.15 Psaumes 105.5 Psaumes 103.2 Nombres 18.1-18.6
5 Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;
1 Chroniques 6.39 2 Chroniques 29.25 1 Chroniques 15.16-15.24 1 Chroniques 25.1-25.6
6 nao makuhani Benaya na Yahazieli wenye baragumu daima, mbele ya sanduku la agano la Mungu.
2 Chroniques 29.26-29.28 2 Chroniques 5.12-5.13 2 Chroniques 13.12 Nombres 10.8
7 Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru Bwana, kwa mkono wa Asafu na nduguze.
2 Samuel 22.1 2 Samuel 23.1-23.2 2 Chroniques 29.30 Psaumes 12.1 Psaumes 18.1
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Wajulisheni watu matendo yake.
Psaumes 105.1-105.15 2 Rois 19.19 Esaïe 12.4 1 Corinthiens 1.2 1 Rois 8.43
9 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi; Zitafakarini ajabu zake zote.
Ephésiens 5.19 Jacques 5.13 Matthieu 26.30 Colossiens 3.16 Psaumes 95.1-95.2
10 Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.
Jérémie 9.23-9.24 Jérémie 29.13 1 Chroniques 28.9 Psaumes 34.2 1 Corinthiens 1.30-1.31
11 Mtakeni Bwana na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.
Psaumes 24.6 Psaumes 67.1 Psaumes 27.8-27.9 Psaumes 4.6 2 Chroniques 6.41
12 Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya; Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;
Psaumes 78.43 Psaumes 103.2 Romains 11.33 1 Chroniques 16.8-16.9 Psaumes 19.9
13 Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake, Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
1 Pierre 2.9 Genèse 35.10-35.12 Genèse 28.13-28.14 Deutéronome 7.6 Exode 19.5-19.6
14 Yeye, Bwana, ndiye Mungu wetu; Duniani mwote mna hukumu zake.
Psaumes 100.3 Psaumes 48.10-48.11 Esaïe 26.9 Psaumes 118.28 Psaumes 63.1
15 Likumbukeni agano lake milele, Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
Deutéronome 7.9 Psaumes 25.10 Psaumes 44.17 Malachie 4.4 Psaumes 105.8
16 Agano alilofanya na Ibrahimu, Na uapo wake kwa Isaka;
Genèse 17.2 Genèse 26.3 Genèse 15.18 Genèse 35.11 Genèse 12.7
17 Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri, Na Israeli liwe agano la milele.
Genèse 35.11-35.12 Jérémie 11.2 Hébreux 13.20 Esaïe 55.3 2 Samuel 23.5
18 Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani, Iwe urithi wenu mliopimiwa;
Genèse 13.15 Genèse 12.7 Genèse 28.13-28.14 Genèse 35.11-35.12 Genèse 17.8
19 Mlipokuwa watu wawezao kuhesabiwa; Naam, watu wachache na wageni ndani yake.
Genèse 34.30 Deutéronome 7.7 Actes 7.5 Hébreux 11.13
20 Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa, Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.
Genèse 46.6 Genèse 12.10 Genèse 20.1 Genèse 46.3
21 Hakumwacha mtu awaonee; Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao;
Genèse 20.3 Genèse 12.17 Exode 7.15-7.18 Exode 9.13-9.18 Genèse 31.24
22 Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.
Genèse 20.7 Genèse 27.39-27.40 1 Jean 2.27 Psaumes 105.15 Genèse 48.19-48.20
23 Mwimbieni Bwana, nchi yote; Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
Psaumes 96.1-96.13 Exode 15.21 Psaumes 40.10 1 Chroniques 16.9 Esaïe 12.5
24 Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za maajabu yake.
Psaumes 22.27 2 Rois 19.19 Daniel 4.1-4.3 Esaïe 12.2-12.6
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana; Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
Psaumes 89.7 Psaumes 76.7 Psaumes 66.3-66.5 Psaumes 144.3-144.6 Exode 15.11
26 Maana miungu yote ya watu si kitu; Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu.
Lévitique 19.4 Psaumes 102.25 Esaïe 42.5 Esaïe 44.24 Esaïe 40.26
27 Heshima na adhama ziko mbele zake; Nguvu na furaha zipo mahali pake.
Psaumes 43.2-43.4 Psaumes 16.11 Psaumes 63.2-63.3 Psaumes 27.4-27.6 Psaumes 28.7-28.8
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za watu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Psaumes 29.1-29.2 Psaumes 66.1-66.2 Psaumes 86.8-86.10 Psaumes 68.34 Psaumes 115.1-115.2
29 Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Leteni sadaka, mje mbele zake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu;
Psaumes 29.2 Psaumes 110.3 Psaumes 96.9 Psaumes 72.15 Psaumes 108.3-108.5
30 Tetemekeni mbele zake, nchi yote.
Psaumes 96.9 Apocalypse 11.15 Hébreux 1.3 Jérémie 10.12 1 Chroniques 16.23
31 Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie; Na waseme katika mataifa, Bwana ametamalaki;
Apocalypse 19.6 Psaumes 97.1 Esaïe 49.13 Psaumes 96.10 Psaumes 99.1
32 Bahari na ivume na vyote viijazavyo; Mashamba na yashangilie na vyote vilivyomo;
Psaumes 93.4 Esaïe 44.23 Psaumes 98.7-98.8 Psaumes 148.9-148.10
33 Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha,
Psaumes 96.12-96.13 Psaumes 98.9 2 Thessaloniciens 1.10 Ezéchiel 17.22-17.24 Apocalypse 11.17-11.18
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Jérémie 33.11 2 Chroniques 5.13 Esdras 3.11 2 Chroniques 7.3 Psaumes 106.1
35 Nanyi mkaseme, Ee Mungu wa wokovu wetu, utuokoe, Utukusanye kwa kututoa katika mataifa, Tulishukuru jina lako takatifu, Tuzifanyie shangwe sifa zako.
Psaumes 106.47-106.48 Psaumes 14.7 Esaïe 43.21 Esaïe 45.25 Psaumes 79.9-79.10
36 Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele hata milele. Na watu wote wakasema, Amina; wakamhimidi Bwana.
1 Rois 8.15 Psaumes 72.18-72.19 Néhémie 8.6 Psaumes 106.48 1 Rois 8.56
37 Basi akawaacha huko, mbele ya sanduku la agano la Bwana, Asafu na nduguze, ili watumike mbele ya sanduku daima, kila siku kama ilivyokuwa kazi yake.
2 Chroniques 8.14 Esdras 3.4 1 Chroniques 15.17-15.24 1 Chroniques 16.4-16.6 1 Chroniques 25.1-25.6
38 Naye Obed-edomu, pamoja na ndugu zao, sitini na wanane; Obed-edomu na mwana wa Yeduthuni, na Hosa, wawe mabawabu;
1 Chroniques 13.14 1 Chroniques 26.10 1 Chroniques 26.4-26.8 1 Chroniques 25.3
39 na Sadoki kuhani, na nduguze makuhani, mbele ya maskani ya Bwana katika mahali pa juu palipokuwa huko Gibeoni,
1 Rois 3.4 1 Chroniques 15.11 2 Chroniques 1.13 2 Chroniques 1.3-1.4 1 Chroniques 21.29
40 ili kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa daima asubuhi na jioni, naam, sawasawa na yote yaliyoandikwa katika torati ya Bwana, aliyowaamuru Israeli;
Nombres 28.3-28.8 Exode 29.38-29.42 2 Chroniques 2.4 Daniel 9.21 1 Rois 18.29
41 na pamoja nao Hemani na Yeduthuni, na wale wengine waliochaguliwa, waliotajwa majina yao, ili kumshukuru Bwana, kwa kuwa fadhili zake ni za milele;
2 Chroniques 5.13 1 Chroniques 25.1-25.6 Nombres 1.17 1 Chroniques 16.34 Esdras 3.11
42 na pamoja nao Hemani na Yeduthuni wenye baragumu na matoazi, kwa hao watakaovumisha sauti, na vinanda kwa ajili ya hizo nyimbo za Mungu; na hao wana wa Yeduthuni wawepo mlangoni.
1 Chroniques 25.6-25.7 2 Chroniques 29.25-29.28 2 Chroniques 7.6 Psaumes 150.3-150.6 Psaumes 84.10
43 Kisha watu wote wakaenda zao kila mtu nyumbani kwake; naye Daudi akarudi ili awabariki watu wa nyumbani mwake.
2 Samuel 6.19-6.20 Genèse 18.19 Psaumes 101.2 Josué 24.15 1 Rois 8.66

Cette Bible est dans le domaine public.