Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 16.2
Bible en Swahili de l’est


Organisation du service du tabernacle

1 Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
1 Chroniques 15.1 2 Chroniques 5.6-5.7 Psaumes 132.8 1 Rois 8.5-8.6 1 Chroniques 15.12
2 Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.
Genèse 20.7 Lévitique 1.3 2 Chroniques 30.27 2 Chroniques 30.18-30.20 Hébreux 7.7
3 Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.
1 Pierre 4.9 Néhémie 8.10 Ezéchiel 45.17 2 Chroniques 30.24 2 Chroniques 35.7-35.8
4 Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;
1 Chroniques 23.2-23.6 1 Chroniques 16.37-16.42 1 Chroniques 15.16 1 Chroniques 16.8 Genèse 33.20
5 Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;
1 Chroniques 6.39 1 Chroniques 15.16-15.24 1 Chroniques 25.1-25.6 2 Chroniques 29.25
6 nao makuhani Benaya na Yahazieli wenye baragumu daima, mbele ya sanduku la agano la Mungu.
2 Chroniques 5.12-5.13 2 Chroniques 13.12 Nombres 10.8 2 Chroniques 29.26-29.28
7 Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru Bwana, kwa mkono wa Asafu na nduguze.
2 Samuel 22.1 Psaumes 12.1 Psaumes 18.1 Néhémie 12.24 2 Samuel 23.1-23.2
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Wajulisheni watu matendo yake.
Psaumes 105.1-105.15 2 Rois 19.19 Esaïe 12.4 1 Corinthiens 1.2 1 Rois 8.43
9 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi; Zitafakarini ajabu zake zote.
Colossiens 3.16 Ephésiens 5.19 Jacques 5.13 Matthieu 26.30 Psaumes 71.17
10 Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.
Esaïe 55.6-55.7 Esaïe 45.25 Proverbes 8.17 Matthieu 7.7-7.8 Jérémie 9.23-9.24
11 Mtakeni Bwana na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.
Psaumes 27.8-27.9 Psaumes 24.6 Psaumes 67.1 2 Chroniques 6.41 Sophonie 2.2-2.3
12 Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya; Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;
Psaumes 103.2 Psaumes 78.43 Psaumes 119.137 Psaumes 119.13 Apocalypse 19.2
13 Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake, Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
Deutéronome 7.6 Exode 19.5-19.6 Genèse 17.7 Psaumes 135.4 1 Pierre 2.9
14 Yeye, Bwana, ndiye Mungu wetu; Duniani mwote mna hukumu zake.
1 Chroniques 16.12 Psaumes 97.8-97.9 Psaumes 95.7 Exode 15.2 Psaumes 100.3
15 Likumbukeni agano lake milele, Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
Psaumes 25.10 Psaumes 44.17 Malachie 4.4 Psaumes 105.8 Deutéronome 7.9
16 Agano alilofanya na Ibrahimu, Na uapo wake kwa Isaka;
Genèse 17.2 Genèse 26.3 Genèse 35.11 Genèse 15.18 Galates 3.15-3.17
17 Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri, Na Israeli liwe agano la milele.
Genèse 35.11-35.12 Genèse 17.7-17.8 Exode 3.17 Josué 24.11-24.13 Jérémie 11.2
18 Akisema, Nitakupa wewe nchi ya Kanaani, Iwe urithi wenu mliopimiwa;
Genèse 13.15 Deutéronome 32.8 Michée 2.5 Nombres 26.53-26.56 Genèse 12.7
19 Mlipokuwa watu wawezao kuhesabiwa; Naam, watu wachache na wageni ndani yake.
Genèse 34.30 Deutéronome 7.7 Actes 7.5 Hébreux 11.13
20 Wakatanga-tanga toka taifa hata taifa, Toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.
Genèse 12.10 Genèse 20.1 Genèse 46.3 Genèse 46.6
21 Hakumwacha mtu awaonee; Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao;
Genèse 12.17 Genèse 20.3 Exode 7.15-7.18 Genèse 31.24 Genèse 31.29
22 Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.
Genèse 20.7 Psaumes 105.15 Genèse 48.19-48.20 1 Rois 19.16 Genèse 49.8-49.10
23 Mwimbieni Bwana, nchi yote; Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.
Psaumes 96.1-96.13 Esaïe 51.6-51.8 Psaumes 71.15 Psaumes 30.4 Exode 15.21
24 Wahubirini mataifa habari za utukufu wake, Na watu wote habari za maajabu yake.
2 Rois 19.19 Daniel 4.1-4.3 Esaïe 12.2-12.6 Psaumes 22.27
25 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kusifiwa sana; Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
Psaumes 89.7 Psaumes 66.3-66.5 Psaumes 144.3-144.6 Psaumes 76.7 Jérémie 10.6-10.10
26 Maana miungu yote ya watu si kitu; Lakini Bwana ndiye aliyezifanya mbingu.
Psaumes 102.25 Lévitique 19.4 Esaïe 44.24 Esaïe 42.5 1 Corinthiens 8.4
27 Heshima na adhama ziko mbele zake; Nguvu na furaha zipo mahali pake.
Psaumes 43.2-43.4 Psaumes 28.7-28.8 Psaumes 8.1 Jean 17.24 Psaumes 96.6
28 Mpeni Bwana, enyi jamaa za watu, Mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Psaumes 29.1-29.2 Ephésiens 1.6 1 Chroniques 29.10-29.14 Philippiens 4.13 Psaumes 66.1-66.2
29 Mpeni Bwana utukufu wa jina lake; Leteni sadaka, mje mbele zake; Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu;
Psaumes 29.2 Psaumes 110.3 Psaumes 68.30-68.31 Apocalypse 7.12 Esaïe 6.3
30 Tetemekeni mbele zake, nchi yote.
Psaumes 33.9 Esaïe 49.8 Psaumes 148.5-148.6 Colossiens 1.17 Psaumes 96.9
31 Mbingu na zifurahi, nchi na ishangilie; Na waseme katika mataifa, Bwana ametamalaki;
Psaumes 96.10 Psaumes 99.1 Apocalypse 19.6 Psaumes 97.1 Esaïe 49.13
32 Bahari na ivume na vyote viijazavyo; Mashamba na yashangilie na vyote vilivyomo;
Esaïe 44.23 Psaumes 98.7-98.8 Psaumes 148.9-148.10 Psaumes 93.4
33 Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha,
Psaumes 96.12-96.13 Psaumes 98.9 2 Thessaloniciens 1.8 2 Pierre 3.14 2 Thessaloniciens 1.10
34 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Jérémie 33.11 2 Chroniques 5.13 Esdras 3.11 2 Chroniques 7.3 Psaumes 136.1-136.26
35 Nanyi mkaseme, Ee Mungu wa wokovu wetu, utuokoe, Utukusanye kwa kututoa katika mataifa, Tulishukuru jina lako takatifu, Tuzifanyie shangwe sifa zako.
Psaumes 106.47-106.48 Psaumes 14.7 Ephésiens 1.12 1 Chroniques 16.9-16.10 Esaïe 43.21
36 Na ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele hata milele. Na watu wote wakasema, Amina; wakamhimidi Bwana.
1 Rois 8.15 1 Rois 8.56 Psaumes 72.18-72.19 Néhémie 8.6 Psaumes 106.48
37 Basi akawaacha huko, mbele ya sanduku la agano la Bwana, Asafu na nduguze, ili watumike mbele ya sanduku daima, kila siku kama ilivyokuwa kazi yake.
2 Chroniques 8.14 Esdras 3.4 1 Chroniques 16.4-16.6 1 Chroniques 25.1-25.6 1 Chroniques 15.17-15.24
38 Naye Obed-edomu, pamoja na ndugu zao, sitini na wanane; Obed-edomu na mwana wa Yeduthuni, na Hosa, wawe mabawabu;
1 Chroniques 26.10 1 Chroniques 13.14 1 Chroniques 26.4-26.8 1 Chroniques 25.3
39 na Sadoki kuhani, na nduguze makuhani, mbele ya maskani ya Bwana katika mahali pa juu palipokuwa huko Gibeoni,
1 Rois 3.4 1 Chroniques 15.11 2 Chroniques 1.13 2 Chroniques 1.3-1.4 1 Chroniques 21.29
40 ili kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa daima asubuhi na jioni, naam, sawasawa na yote yaliyoandikwa katika torati ya Bwana, aliyowaamuru Israeli;
Nombres 28.3-28.8 Exode 29.38-29.42 Esdras 3.3 Amos 4.4 2 Chroniques 31.3
41 na pamoja nao Hemani na Yeduthuni, na wale wengine waliochaguliwa, waliotajwa majina yao, ili kumshukuru Bwana, kwa kuwa fadhili zake ni za milele;
2 Chroniques 5.13 1 Chroniques 25.1-25.6 1 Chroniques 6.33 Nombres 1.17 1 Chroniques 16.34
42 na pamoja nao Hemani na Yeduthuni wenye baragumu na matoazi, kwa hao watakaovumisha sauti, na vinanda kwa ajili ya hizo nyimbo za Mungu; na hao wana wa Yeduthuni wawepo mlangoni.
2 Chroniques 29.25-29.28 2 Chroniques 7.6 Psaumes 150.3-150.6 Psaumes 84.10 1 Chroniques 25.6-25.7
43 Kisha watu wote wakaenda zao kila mtu nyumbani kwake; naye Daudi akarudi ili awabariki watu wa nyumbani mwake.
2 Samuel 6.19-6.20 Psaumes 101.2 Josué 24.15 1 Rois 8.66 Genèse 18.19

Cette Bible est dans le domaine public.