Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 4.6
Bible en Swahili de l’est


Miracles accomplis par Élisée

1 Basi, mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha, akasema, Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha Bwana; na aliyemwia amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa.
2 Rois 2.3 Néhémie 5.2-5.5 Lévitique 25.39-25.41 Lévitique 25.48 Matthieu 18.25
2 Elisha akamwambia, Nikufanyie nini? Niambie; una kitu gani nyumbani? Akasema, Mimi mjakazi wako sina kitu nyumbani, ila chupa ya mafuta.
1 Rois 17.12 Jean 6.5-6.7 Matthieu 15.34 2 Rois 6.26-6.27 2 Rois 2.9
3 Akasema, Nenda, ukatake vyombo huko nje kwa jirani zako wote, vyombo vitupu; wala usitake vichache.
Jean 2.7 2 Rois 13.18-13.19 Psaumes 81.10 2 Rois 3.16 Jean 16.24
4 Kisha uingie ndani, ukajifungie mlango wewe na wanao, ukavimiminie mafuta vyombo vile vyote; navyo vilivyojaa ukavitenge.
Marc 8.5-8.9 2 Rois 4.32-4.33 Ephésiens 3.20 Esaïe 26.20 Matthieu 6.6
5 Basi akamwacha, akajifungia mlango yeye na wanawe; hao wakamletea vile vyombo, na yeye akamimina.
Luc 1.45 2 Rois 5.11 Hébreux 11.7-11.8 1 Rois 17.15-17.16
6 Ikawa, vilipokwisha kujaa vile vyombo, akamwambia mwanawe, Niletee tena chombo. Akamwambia, Hakuna tena chombo. Mafuta yakakoma.
Matthieu 14.20 2 Rois 13.19 Matthieu 13.58 Luc 6.19 Jean 6.12
7 Ndipo akaja akamwambia yule mtu wa Mungu. Naye akasema, Enenda ukayauze mafuta haya, uilipe deni yako; nayo yaliyosalia uyatumie wewe na watoto wako.
2 Thessaloniciens 3.7-3.12 1 Thessaloniciens 4.12 Romains 12.17 1 Rois 12.22 1 Thessaloniciens 2.9-2.10
8 Hata ikawa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; naye akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula.
Josué 19.18 2 Samuel 19.32 Job 32.9 2 Rois 4.11-4.12 Genèse 19.3
9 Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu wa Mungu.
2 Rois 4.7 Proverbes 31.10-31.11 1 Rois 17.24 1 Thessaloniciens 2.10 1 Rois 17.18
10 Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa; na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.
Romains 12.13 Matthieu 10.41-10.42 Matthieu 25.40 1 Pierre 4.9-4.10 Hébreux 13.2
11 Ikawa siku moja akafika huko, akaingia katika chumba kile akalala.
12 Akamwambia Gehazi mtumishi wake, Mwite yule Mshunami. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mbele yake.
2 Rois 8.4-8.5 2 Rois 5.20-5.27 2 Rois 4.29-4.31 1 Rois 18.43 1 Rois 19.3
13 Akamwambia, Sema naye sasa, Tazama, wewe umetutunza sana namna hii; utendewe nini basi? Je! Uombewe neno kwa mfalme, au kwa amiri wa jeshi? Yule mwanamke akamjibu, Mimi ninakaa katika watu wangu mwenyewe.
2 Samuel 19.13 2 Rois 9.5 Ruth 1.1-1.4 1 Thessaloniciens 5.12-5.13 Philippiens 4.18-4.19
14 Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee.
Juges 13.2 Genèse 18.10-18.14 1 Samuel 1.8 Genèse 25.21 1 Samuel 1.2
15 Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni.
16 Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana. Akasema, La! Bwana wangu, wewe mtu wa Mungu, usiniambie mimi mjakazi wako uongo.
2 Rois 4.28 Genèse 18.10 2 Rois 5.10-5.11 2 Rois 2.19 1 Rois 18.9
17 Yule mwanamke akachukua mimba, akazaa mtoto mume wakati uo huo mwakani, kama Elisha alivyomwambia.
Genèse 21.1 1 Samuel 1.19-1.20 Luc 1.24-1.25 Luc 1.36 Hébreux 11.11
18 Hata yule mtoto alipokua, ikawa siku moja alitoka kwenda kwa baba yake kwenye wavunao.
Ruth 2.4
19 Akamwambia baba yake, Kichwa changu! Kichwa changu! Naye akamwambia mtumishi wake, Mchukue kwa mama yake.
Jérémie 4.19 Job 14.1-14.2
20 Akamchukua, akampeleka kwa mama yake, naye akakaa magotini mwake hata adhuhuri, kisha akafa.
Jean 11.3 Jean 11.5 Jean 11.14 Luc 7.12 Esaïe 66.13
21 Mamaye akapanda juu, akamlaza juu ya kitanda cha yule mtu wa Mungu, akamfungia mlango, akatoka.
2 Rois 4.32 2 Rois 4.7 1 Rois 17.19 2 Rois 4.10
22 Kisha akamwita mumewe, akasema, Tafadhali, uniletee mtu mmoja wa watumishi, na punda mmoja, ili nimwendee yule mtu wa Mungu kwa haraka, nikarudi tena.
Actes 9.38 2 Rois 4.24 Jean 11.3 2 Rois 4.26
23 Akasema, Kwa nini kumwendea leo? Sio mwandamo wa mwezi, wala sabato. Akasema, Si neno.
1 Chroniques 23.31 Nombres 28.11 Nombres 10.10 Esaïe 1.13-1.15
24 Akatandika punda, akamwambia mtumishi wake, Mwendeshe, twendelee mbele. Usinipunguzie mwendo, nisipokuambia.
1 Rois 13.23 Exode 4.20 1 Rois 13.13 1 Samuel 25.19-25.20
25 Basi akaenda, akafika kwa yule mtu wa Mungu, katika mlima wa Karmeli. Ikawa, yule mtu wa Mungu alipomwona kwa mbali, akamwambia Gehazi mtumishi wake, Tazama, Mshunami yule kule.
2 Rois 2.25 1 Rois 18.19 Esaïe 35.2 1 Rois 18.42
26 Tafadhali piga mbio sasa kwenda kumlaki, ukamwambie, Hujambo? Mume wako hajambo? Mtoto hajambo? Akajibu, Hawajambo.
Actes 15.36 Genèse 29.6 1 Samuel 17.18 Genèse 37.14 Psaumes 39.9
27 Naye alipofika kwa yule mtu wa Mungu kilimani, alimshika miguu. Gehazi akakaribia amwondoe; lakini mtu wa Mungu akamwambia, Mwache; maana roho yake ndani yake ina uchungu; na Bwana amenificha, wala hakuniambia.
Matthieu 15.23 Matthieu 28.9 Matthieu 20.31 1 Samuel 1.10 Genèse 18.17
28 Yule mwanamke akasema, Je! Naliomba mwana kwa bwana wangu? Mimi sikusema, Usinidanganye?
2 Rois 4.16 Genèse 30.1
29 Ndipo Elisha akamwambia Gehazi, Jikaze viuno, ukachukue fimbo yangu mkononi mwako, ukaende zako; ukikutana na mtu, usimsalimu; na mtu akikusalimu, usimjibu; ukaweke fimbo yangu juu ya uso wa mtoto.
2 Rois 2.14 Exode 14.16 1 Rois 18.46 Luc 10.4 2 Rois 9.1
30 Na mama yake yule mtoto akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha. Basi akaondoka, akamfuata.
2 Rois 2.4 2 Rois 2.2 Ruth 1.16-1.18 Exode 33.12-33.16
31 Na Gehazi akawatangulia, akaiweka ile fimbo juu ya uso wa mtoto; lakini hapakuwa na sauti, wala majibu. Basi akarudi ili kumlaki, akamwambia, akisema, Mtoto hakuamka.
Jean 11.11 1 Samuel 28.6 Ezéchiel 14.3 Job 14.12 Marc 5.39
32 Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake.
Jean 11.17 Luc 8.52-8.53 1 Rois 17.17
33 Basi akaingia ndani, akajifungia mlango, yeye na yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana.
Matthieu 6.6 2 Rois 4.4 1 Rois 18.26-18.27 Actes 9.40 2 Rois 6.17-6.18
34 Akapanda juu ya kitanda, akajilaza juu ya mtoto, akaweka kinywa chake juu ya kinywa chake, na macho yake juu ya macho yake, na mikono yake juu ya mikono yake; akajinyosha juu yake; mwili wake yule mtoto ukaanza kupata moto.
1 Rois 17.21 Actes 20.10
35 Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko na huko mara moja; akapanda, akajinyosha juu yake; na yule mtoto akapiga chafya mara saba, na mtoto akafumbua macho yake.
2 Rois 8.5 2 Rois 13.21 Actes 9.40 2 Rois 8.1 Luc 8.55
36 Akamwita Gehazi, akasema, Mwite yule Mshunami. Basi akamwita. Na alipofika kwake, Elisha akasema, Haya! Mchukue mwanao.
Hébreux 11.35 1 Rois 17.23 Luc 7.15
37 Ndipo akaingia, akamwangukia miguu akainama mpaka nchi; kisha akamchukua mwanawe, akatoka.
Hébreux 11.35 2 Rois 4.27 2 Rois 2.15 1 Rois 17.24
38 Elisha akafika Gilgali tena; na kulikuwa na njaa katika nchi; na hao wana wa manabii walikuwa wakikaa mbele yake. Akamwambia mtumishi wake, Teleka sufuria kubwa, uwapikie wana wa manabii.
2 Rois 2.1 2 Rois 2.3 2 Rois 8.1 Actes 22.3 Luc 10.39
39 Na mmoja wao akaenda nje kondeni ili kuchuma mboga, akaona mtango-mwitu, akayachuma matango-mwitu, hata nguo yake ikawa imejaa, akaja akayapasua-pasua sufuriani; kwa maana hawakuyajua.
Jérémie 2.21 Hébreux 12.15 Matthieu 15.13 Esaïe 5.4
40 Basi wakawapakulia hao watu ili wale. Ikawa, walipokuwa katika kula chakula, wakapiga kelele, wakasema, Mauti imo sufuriani, Ee mtu wa Mungu. Wala hawakuweza kula.
Exode 10.17 1 Rois 17.18 Exode 15.23 2 Rois 4.9 2 Rois 1.13
41 Lakini yeye akasema, Leteni unga. Naye akautupa ndani ya sufuria; akasema, Wapakulie watu, ili wale. Wala hakikuwamo kitu kibaya sufuriani.
2 Rois 2.21 Exode 15.25 2 Rois 5.10 2 Rois 6.6 Jean 9.6
42 Tena, akaja mtu kutoka Baal-shalisha, akamletea mtu wa Mungu chakula cha malimbuko, mikate ishirini ya shayiri, na masuke mabichi ya ngano guniani. Akasema, Uwape watu, ili wale.
1 Samuel 9.7 1 Samuel 9.4 Jean 6.9 Jean 6.13 Proverbes 3.9-3.10
43 Na mtumishi wake akasema, Je! Niwaandikie hiki watu mia? Lakini akasema, Uwape watu, ili wale; kwa kuwa Bwana asema hivi, Watakula na kusaza.
Luc 9.13 Jean 6.9 Matthieu 14.20 Matthieu 14.16-14.17 Matthieu 16.8-16.10
44 Basi akawaandikia, nao wakala, wakasaza, sawasawa na neno la Bwana.

Cette Bible est dans le domaine public.