Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 4.19
Bible en Swahili de l’est


Miracles accomplis par Élisée

1 Basi, mwanamke mmoja miongoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha, akasema, Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha Bwana; na aliyemwia amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa.
2 Rois 2.3 Lévitique 25.48 Matthieu 18.25 Néhémie 5.2-5.5 Lévitique 25.39-25.41
2 Elisha akamwambia, Nikufanyie nini? Niambie; una kitu gani nyumbani? Akasema, Mimi mjakazi wako sina kitu nyumbani, ila chupa ya mafuta.
1 Rois 17.12 2 Rois 2.9 2 Corinthiens 6.10 Actes 3.6 Jacques 2.5
3 Akasema, Nenda, ukatake vyombo huko nje kwa jirani zako wote, vyombo vitupu; wala usitake vichache.
2 Rois 3.16 Jean 16.24 Jean 2.7 2 Rois 13.18-13.19 Psaumes 81.10
4 Kisha uingie ndani, ukajifungie mlango wewe na wanao, ukavimiminie mafuta vyombo vile vyote; navyo vilivyojaa ukavitenge.
Marc 8.5-8.9 Matthieu 6.6 Jean 2.7-2.9 Actes 9.40 Marc 5.40
5 Basi akamwacha, akajifungia mlango yeye na wanawe; hao wakamletea vile vyombo, na yeye akamimina.
Hébreux 11.7-11.8 1 Rois 17.15-17.16 Luc 1.45 2 Rois 5.11
6 Ikawa, vilipokwisha kujaa vile vyombo, akamwambia mwanawe, Niletee tena chombo. Akamwambia, Hakuna tena chombo. Mafuta yakakoma.
Matthieu 14.20 Jean 6.12 Josué 5.12 2 Rois 4.43-4.44 1 Rois 17.14
7 Ndipo akaja akamwambia yule mtu wa Mungu. Naye akasema, Enenda ukayauze mafuta haya, uilipe deni yako; nayo yaliyosalia uyatumie wewe na watoto wako.
2 Thessaloniciens 3.7-3.12 1 Thessaloniciens 2.9-2.10 Psaumes 37.21 Philippiens 4.8 1 Thessaloniciens 4.12
8 Hata ikawa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; naye akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula.
Josué 19.18 2 Samuel 19.32 2 Rois 4.11-4.12 Genèse 19.3 Proverbes 7.21
9 Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu wa Mungu.
2 Rois 4.7 Proverbes 31.10-31.11 1 Rois 17.24 1 Thessaloniciens 2.10 1 Rois 17.18
10 Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa; na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.
Romains 12.13 Matthieu 10.41-10.42 Matthieu 25.40 1 Rois 17.19 Marc 9.41
11 Ikawa siku moja akafika huko, akaingia katika chumba kile akalala.
12 Akamwambia Gehazi mtumishi wake, Mwite yule Mshunami. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mbele yake.
2 Rois 8.4-8.5 2 Rois 5.20-5.27 2 Rois 4.29-4.31 2 Rois 3.11 Actes 13.5
13 Akamwambia, Sema naye sasa, Tazama, wewe umetutunza sana namna hii; utendewe nini basi? Je! Uombewe neno kwa mfalme, au kwa amiri wa jeshi? Yule mwanamke akamjibu, Mimi ninakaa katika watu wangu mwenyewe.
2 Samuel 19.13 Luc 9.3-9.5 2 Timothée 1.16-1.18 Psaumes 37.3 2 Rois 3.15-3.18
14 Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee.
Genèse 25.21 1 Samuel 1.2 Luc 1.7 Genèse 15.2-15.3 Genèse 17.17
15 Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni.
16 Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana. Akasema, La! Bwana wangu, wewe mtu wa Mungu, usiniambie mimi mjakazi wako uongo.
2 Rois 4.28 Genèse 18.10 1 Rois 17.18 Genèse 17.16-17.17 Luc 1.13
17 Yule mwanamke akachukua mimba, akazaa mtoto mume wakati uo huo mwakani, kama Elisha alivyomwambia.
Luc 1.36 Hébreux 11.11 Psaumes 113.9 Genèse 21.1 1 Samuel 1.19-1.20
18 Hata yule mtoto alipokua, ikawa siku moja alitoka kwenda kwa baba yake kwenye wavunao.
Ruth 2.4
19 Akamwambia baba yake, Kichwa changu! Kichwa changu! Naye akamwambia mtumishi wake, Mchukue kwa mama yake.
Jérémie 4.19 Job 14.1-14.2
20 Akamchukua, akampeleka kwa mama yake, naye akakaa magotini mwake hata adhuhuri, kisha akafa.
Jean 11.5 Jean 11.14 Luc 7.12 Jean 11.3 Genèse 37.3
21 Mamaye akapanda juu, akamlaza juu ya kitanda cha yule mtu wa Mungu, akamfungia mlango, akatoka.
2 Rois 4.32 2 Rois 4.10 2 Rois 4.7 1 Rois 17.19
22 Kisha akamwita mumewe, akasema, Tafadhali, uniletee mtu mmoja wa watumishi, na punda mmoja, ili nimwendee yule mtu wa Mungu kwa haraka, nikarudi tena.
Jean 11.3 2 Rois 4.26 Actes 9.38 2 Rois 4.24
23 Akasema, Kwa nini kumwendea leo? Sio mwandamo wa mwezi, wala sabato. Akasema, Si neno.
Nombres 10.10 1 Chroniques 23.31 Nombres 28.11 Esaïe 1.13-1.15
24 Akatandika punda, akamwambia mtumishi wake, Mwendeshe, twendelee mbele. Usinipunguzie mwendo, nisipokuambia.
1 Rois 13.23 1 Rois 13.13 1 Samuel 25.19-25.20 Exode 4.20
25 Basi akaenda, akafika kwa yule mtu wa Mungu, katika mlima wa Karmeli. Ikawa, yule mtu wa Mungu alipomwona kwa mbali, akamwambia Gehazi mtumishi wake, Tazama, Mshunami yule kule.
2 Rois 2.25 Esaïe 35.2 1 Rois 18.42 1 Rois 18.19
26 Tafadhali piga mbio sasa kwenda kumlaki, ukamwambie, Hujambo? Mume wako hajambo? Mtoto hajambo? Akajibu, Hawajambo.
Actes 15.36 Psaumes 39.9 1 Samuel 3.18 Job 1.21-1.22 2 Rois 4.23
27 Naye alipofika kwa yule mtu wa Mungu kilimani, alimshika miguu. Gehazi akakaribia amwondoe; lakini mtu wa Mungu akamwambia, Mwache; maana roho yake ndani yake ina uchungu; na Bwana amenificha, wala hakuniambia.
1 Samuel 1.10 Genèse 18.17 Marc 14.6 Job 10.1 Jean 12.4-12.7
28 Yule mwanamke akasema, Je! Naliomba mwana kwa bwana wangu? Mimi sikusema, Usinidanganye?
2 Rois 4.16 Genèse 30.1
29 Ndipo Elisha akamwambia Gehazi, Jikaze viuno, ukachukue fimbo yangu mkononi mwako, ukaende zako; ukikutana na mtu, usimsalimu; na mtu akikusalimu, usimjibu; ukaweke fimbo yangu juu ya uso wa mtoto.
2 Rois 2.14 1 Rois 18.46 Exode 14.16 Luc 10.4 2 Rois 9.1
30 Na mama yake yule mtoto akasema, Kama Bwana aishivyo, na roho yako iishivyo, sitakuacha. Basi akaondoka, akamfuata.
2 Rois 2.4 2 Rois 2.2 Ruth 1.16-1.18 Exode 33.12-33.16
31 Na Gehazi akawatangulia, akaiweka ile fimbo juu ya uso wa mtoto; lakini hapakuwa na sauti, wala majibu. Basi akarudi ili kumlaki, akamwambia, akisema, Mtoto hakuamka.
Jean 11.11 Marc 5.39 Marc 9.19-9.29 Jean 11.43-11.44 Matthieu 17.16-17.20
32 Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake.
Luc 8.52-8.53 1 Rois 17.17 Jean 11.17
33 Basi akaingia ndani, akajifungia mlango, yeye na yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana.
Matthieu 6.6 2 Rois 4.4 2 Rois 6.17-6.18 1 Rois 17.20-17.21 2 Rois 5.11
34 Akapanda juu ya kitanda, akajilaza juu ya mtoto, akaweka kinywa chake juu ya kinywa chake, na macho yake juu ya macho yake, na mikono yake juu ya mikono yake; akajinyosha juu yake; mwili wake yule mtoto ukaanza kupata moto.
1 Rois 17.21 Actes 20.10
35 Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko na huko mara moja; akapanda, akajinyosha juu yake; na yule mtoto akapiga chafya mara saba, na mtoto akafumbua macho yake.
2 Rois 8.5 2 Rois 8.1 Luc 8.55 Luc 7.14-7.15 Jean 11.43-11.44
36 Akamwita Gehazi, akasema, Mwite yule Mshunami. Basi akamwita. Na alipofika kwake, Elisha akasema, Haya! Mchukue mwanao.
Hébreux 11.35 1 Rois 17.23 Luc 7.15
37 Ndipo akaingia, akamwangukia miguu akainama mpaka nchi; kisha akamchukua mwanawe, akatoka.
2 Rois 2.15 1 Rois 17.24 Hébreux 11.35 2 Rois 4.27
38 Elisha akafika Gilgali tena; na kulikuwa na njaa katika nchi; na hao wana wa manabii walikuwa wakikaa mbele yake. Akamwambia mtumishi wake, Teleka sufuria kubwa, uwapikie wana wa manabii.
2 Rois 2.3 2 Rois 8.1 2 Rois 2.1 Luc 10.39 Actes 22.3
39 Na mmoja wao akaenda nje kondeni ili kuchuma mboga, akaona mtango-mwitu, akayachuma matango-mwitu, hata nguo yake ikawa imejaa, akaja akayapasua-pasua sufuriani; kwa maana hawakuyajua.
Matthieu 15.13 Esaïe 5.4 Jérémie 2.21 Hébreux 12.15
40 Basi wakawapakulia hao watu ili wale. Ikawa, walipokuwa katika kula chakula, wakapiga kelele, wakasema, Mauti imo sufuriani, Ee mtu wa Mungu. Wala hawakuweza kula.
Exode 10.17 2 Rois 4.9 2 Rois 1.13 Deutéronome 33.1 2 Rois 1.11
41 Lakini yeye akasema, Leteni unga. Naye akautupa ndani ya sufuria; akasema, Wapakulie watu, ili wale. Wala hakikuwamo kitu kibaya sufuriani.
Exode 15.25 2 Rois 2.21 Jean 9.6 1 Corinthiens 1.25 Actes 28.5
42 Tena, akaja mtu kutoka Baal-shalisha, akamletea mtu wa Mungu chakula cha malimbuko, mikate ishirini ya shayiri, na masuke mabichi ya ngano guniani. Akasema, Uwape watu, ili wale.
1 Samuel 9.7 1 Samuel 9.4 Jean 6.9 Jean 6.13 2 Rois 4.38
43 Na mtumishi wake akasema, Je! Niwaandikie hiki watu mia? Lakini akasema, Uwape watu, ili wale; kwa kuwa Bwana asema hivi, Watakula na kusaza.
Luc 9.13 Jean 6.9 Matthieu 14.20 Matthieu 15.33-15.34 Matthieu 15.37
44 Basi akawaandikia, nao wakala, wakasaza, sawasawa na neno la Bwana.

Cette Bible est dans le domaine public.