Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 4.11
Bible en Swahili de l’est


Les hauts fonctionnaires de Salomon

1 Basi mfalme Sulemani akawa mfalme juu ya Israeli wote.
Ecclésiaste 1.12 1 Chroniques 12.38 2 Chroniques 9.30 1 Rois 11.13 1 Rois 11.35-11.36
2 Na hawa ndio wakuu aliokuwa nao; Azaria mwana wa Sadoki, kuhani,
Exode 18.21 1 Chroniques 6.8-6.10 2 Samuel 8.15-8.18 1 Chroniques 27.17 1 Corinthiens 12.28
3 Elihorefu na Ahiya, wana wa Shausha, waandishi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi mwenye kuandika tarehe;
2 Samuel 8.16 Esaïe 62.6 2 Samuel 20.24-20.25 1 Chroniques 18.6 1 Chroniques 18.15
4 na Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya jeshi; na Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
1 Rois 2.35 1 Rois 2.26-2.27
5 na Azaria mwana wa Nathani alikuwa juu ya maakida; na Zabudi mwana wa Nathani alikuwa kuhani, rafiki wake mfalme.
2 Samuel 15.37 2 Samuel 16.16 1 Chroniques 27.33 2 Samuel 12.25 2 Samuel 8.18
6 Na Ahishari alikuwa juu ya nyumba; na Adoramu mwana wa Abda alikuwa juu ya shokoa.
2 Samuel 20.24 1 Rois 12.18 1 Rois 9.15 1 Rois 5.13-5.14
7 Sulemani alikuwa na maakida kumi na wawili juu ya Israeli wote, walioleta chakula cha mfalme na nyumba yake; kila mtu alikuwa na mwezi mmoja katika mwaka kuleta chakula.
1 Chroniques 27.1-27.15
8 Na haya ndiyo majina yao. Mwana wa Huri, mlimani mwa Efraimu.
Josué 24.33 Juges 17.1 Juges 19.1
9 Mwana wa Dekari, kutoka Makasi, na Shaalbimu na Bethshemeshi na Elon-beth-hanani.
Josué 21.16 Juges 1.35 Josué 19.42 1 Samuel 6.20 1 Samuel 6.12
10 Mwana wa Hesedi, katika Arubothi; na Soko ilikuwa kwake na nchi yote ya Heferi.
Josué 15.35 Josué 12.17 Josué 17.2
11 Mwana wa Abinadabu katika Nafath-dori yote; ndiye aliyekuwa naye Tafathi binti Sulemani kuwa mke wake.
Josué 11.2 Josué 17.11 Josué 12.23 Juges 1.27
12 Baana mwana wa Ahiludi, katika Taanaki na Megido, na Beth-sheani yote, iliyo kando ya Sarethani, chini ya Yezreeli, tangu Beth-sheani mpaka Abel-mehola, hata kupita Yokmeamu.
Josué 17.11 Josué 3.16 1 Rois 19.16 Juges 5.19 1 Rois 7.46
13 Mwana wa Geberi katika Ramoth-gileadi; na kwake ilikuwa miji ya Yairi mwana wa Manase iliyomo Gileadi; na kwake ilikuwa wilaya ya Argobu, iliyomo Bashani, miji mikubwa sitini yenye kuta na makomeo ya shaba.
Nombres 32.41 Deutéronome 3.4 1 Rois 22.3 Psaumes 68.15 Deutéronome 3.13-3.14
14 Ahinadabu mwana wa Ido, katika Mahanaimu.
2 Samuel 17.27 Genèse 32.2 Josué 13.26 2 Samuel 17.24 2 Samuel 2.8
15 Ahimaasi, katika Naftali; naye ndiye aliyemwoa Basemathi binti Sulemani.
1 Rois 4.11 1 Samuel 18.18 2 Samuel 15.27 Josué 19.32-19.39
16 Baana mwana wa Hushai, katika Asheri na Bealothi.
Josué 19.24-19.31 2 Samuel 15.32
17 Yehoshafati mwana wa Parua, katika Isakari.
Josué 19.17-19.23
18 Shimei mwana wa Ela, katika Benyamini.
1 Rois 1.8 Zacharie 12.13 Josué 18.20-18.28
19 Geberi mwana wa Uri, katika nchi ya Gileadi, nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, na Ogu mfalme wa Bashani; naye alikuwa akida wa pekee katika nchi hiyo.
Nombres 21.21-21.35 Deutéronome 2.26-3.17 Josué 13.9-13.12

Puissance de Salomon

20 Yuda na Israeli walikuwa wengi kama mchanga wa pwani kwa wingi, wakila, na kunywa, na kufurahi.
1 Rois 3.8 Genèse 22.17 Genèse 32.12 Genèse 13.16 Genèse 15.5
21 Sulemani akatawala juu ya falme zote, toka Mto mpaka nchi ya Wafilisti, na hata mpaka wa Misri; walimletea tunu, na kumtumikia Sulemani siku zote za maisha yake.
Josué 1.4 Genèse 15.18 Psaumes 68.29 Exode 23.31 Psaumes 72.8-72.11
22 Na vyakula vya Sulemani vya siku moja vilikuwa kori therathini za unga wa mzuri, na kori sitini za ngano.
23 na ng’ombe kumi walionona, na ng’ombe ishirini za malisho, na kondoo mia, pamoja na ayala, na paa, na kulungu, na kuku walionona.
Néhémie 5.17-5.18
24 Kwani alikuwa akitawala nchi yote upande huu wa Mto, toka Tifsa mpaka Gaza, juu ya wafalme wote wa upande huu wa Mto; naye alikuwa na amani pande zake zote.
1 Chroniques 22.9 Psaumes 72.11 Genèse 10.19 Hébreux 7.1-7.2 Psaumes 72.3
25 Yuda na Israeli wakakaa salama, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, tokea Dani mpaka Beer-sheba, siku zote za Sulemani.
Michée 4.4 Zacharie 3.10 2 Rois 18.31 Juges 20.1 Ezéchiel 38.11
26 Tena Sulemani alikuwa na mabanda ya farasi arobaini elfu kwa magari yake, na wapandao farasi kumi na mbili elfu.
2 Chroniques 1.14 2 Chroniques 9.25 2 Samuel 8.4 Psaumes 20.7 Deutéronome 17.16
27 Na maakida wale wakaleta chakula kwa mfalme Sulemani na kwa wote walioijia meza ya mfalme Sulemani, kila mtu katika mwezi wake, kisipunguke kitu.
28 Shayiri pia na majani kwa farasi, na kwa wanyama wenye mbio, wakaleta mahali walipokuwapo, kila mtu kwa kadiri ya kazi yake.
Esther 8.10 Esther 8.14 Michée 1.13
29 Mungu akampa Sulemani hekima, na akili nyingi sana, na moyo mkuu, kama mchanga ulioko pwani.
1 Rois 3.12 1 Rois 4.20 Ecclésiaste 1.16 Psaumes 119.34 1 Rois 3.28
30 Hekima ya Sulemani ikapita hekima ya wana wote wa mashariki, na hekima zote za Misri.
Actes 7.22 Genèse 25.6 Daniel 1.20 Daniel 4.7 Matthieu 2.16
31 Kwa kuwa alikuwa na hekima kuliko watu wote; kuliko Ethani Mwezrahi, na Hemani, na Kalkoli, na Darda, wana wa Maholi; zikaenea sifa zake kati ya mataifa yote yaliyozunguka.
1 Chroniques 2.6 1 Chroniques 15.19 1 Rois 3.12 1 Chroniques 6.33 Psaumes 89.1-89.52
32 Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.
Ecclésiaste 12.9 Proverbes 1.1-1.31 Matthieu 13.35 Cantique 1.1-1.17
33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.
Genèse 1.20-1.25 Nombres 19.18 Psaumes 51.7 Psaumes 92.12 Nombres 24.6
34 Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake.
1 Rois 10.1 2 Chroniques 9.23 2 Chroniques 9.1 Esaïe 2.2 Zacharie 8.23

Cette Bible est dans le domaine public.