Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 4
Bible en Swahili de l’est


Caïn et Abel

1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana.
Genèse 3.15 Genèse 5.29 1 Jean 3.12 Genèse 4.25
2 Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.
1 Jean 3.15 1 Jean 3.12 Luc 11.51 1 Jean 3.10 Jean 8.44
3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana.
Nombres 18.12 Lévitique 2.1-2.11 Néhémie 13.6
4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;
Hébreux 11.4 Proverbes 3.9 Exode 13.12 Nombres 18.17 Apocalypse 13.8
5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.
Hébreux 11.4 Actes 13.45 Job 5.2 Luc 15.28-15.30 Matthieu 20.15
6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
Esaïe 1.18 Luc 15.31-15.32 Job 5.2
7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
Jacques 1.15 Romains 7.8-7.9 Esaïe 3.10-3.11 Romains 6.16 Romains 2.6-2.10
8 Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani,Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua.
Matthieu 23.35 Jude 1.11 1 Jean 3.12-3.15 Luc 11.51 Michée 7.6
9 Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?
Jean 8.44 Proverbes 28.13 Genèse 3.9-3.11 Psaumes 9.12 Psaumes 10.13-10.14
10 Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
Hébreux 12.24 Psaumes 72.14 Jacques 5.4 Job 31.38-31.39 Nombres 35.33
11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
Galates 3.10 Genèse 3.14 Deutéronome 28.15-28.20 Apocalypse 12.16 Deutéronome 27.16-27.26
12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
Deutéronome 28.23-28.24 Lévitique 26.36 Romains 8.20 Genèse 4.14 Lévitique 26.20
13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
Apocalypse 16.9 Job 15.22 Apocalypse 16.11 Apocalypse 16.21
14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.
Job 15.20-15.24 Nombres 35.19 Proverbes 28.1 Deutéronome 28.65 Genèse 9.5-9.6
15 Bwana akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga.
Ezéchiel 9.4 Ezéchiel 9.6 Genèse 4.24 Psaumes 79.12 Apocalypse 14.11

Descendance de Caïn

16 Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, akakaa katika nchi ya Nodi, mbele ya Edeni.
2 Rois 24.20 Jérémie 23.39 Genèse 3.8 Exode 20.18 2 Rois 13.23
17 Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe.
Psaumes 49.11 2 Samuel 18.18 Genèse 11.4 Genèse 5.22 Ecclésiaste 2.4-2.11
18 Henoko akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli; Mehuyaeli akamzaa Methushaeli; Methushaeli akamzaa Lameki.
Genèse 5.21 Genèse 36.2
19 Lameki akajitwalia wake wawili, jina la wa kwanza ni Ada, na jina la wa pili ni Sila.
Genèse 2.24 Matthieu 19.4-19.6 Genèse 2.18 Matthieu 19.8
20 Ada akamzaa Yabali; huyo ndiye baba yao wakaao katika hema na kufuga wanyama.
Jérémie 35.9-35.10 1 Chroniques 4.4-4.5 Genèse 4.2 Genèse 4.21 Genèse 25.27
21 Na jina la nduguye aliitwa Yubali; huyo ndiye baba yao wapigao kinubi na filimbi.
Job 21.12 Genèse 31.27 Romains 4.11-4.12 Amos 6.5 Esaïe 5.12
22 Sila naye akamzaa Tubal-kaini, mfua kila chombo cha kukatia, cha shaba na cha chuma; na umbu lake Tubal-kaini alikuwa Naama.
Deutéronome 33.25 Deutéronome 8.9 2 Chroniques 2.7 Nombres 31.22 Exode 25.3
23 Lameki akawaambia wake zake, Sikieni sauti yangu, Ada na Sila; Enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; Maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; Kijana kwa kunichubua;
Juges 9.7 Lévitique 19.18 Nombres 23.18 Exode 20.13
24 Kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, Hakika Lameki atalipiwa mara sabini na saba.
Genèse 4.15 Matthieu 18.22
25 Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pa Habili; kwa sababu Kaini alimwua.
Genèse 4.8 1 Chroniques 1.1 Genèse 4.10-4.11 Genèse 4.1-4.3 Genèse 5.3-5.4
26 Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la Bwana.
Sophonie 3.9 Psaumes 116.17 1 Corinthiens 1.2 Joël 2.32 1 Rois 18.24

Cette Bible est dans le domaine public.