Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 37.4
Bible en Swahili de l’est


Histoire de Joseph

Joseph vendu par ses frères

1 Yakobo akakaa katika nchi aliyosafiri baba yake, katika nchi ya Kanaani.
Genèse 17.8 Genèse 28.4 Genèse 36.7 Hébreux 11.9-11.16 Genèse 23.4
2 Hivi ndivyo vizazi vya Yakobo. Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya.
Genèse 35.25-35.26 1 Samuel 2.22-2.24 1 Corinthiens 11.18 Jean 7.7 Genèse 5.1
3 Basi Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote, maana ni mwana wa uzee wake, akamfanyia kanzu ndefu.
Genèse 37.32 Genèse 37.23 2 Samuel 13.18 Jean 13.22-13.23 Ezéchiel 16.16
4 Ndugu zake wakaona ya kuwa baba yao anampenda kuliko ndugu zake wote, wakamchukia, wala hawakuweza kusema naye kwa amani.
Genèse 27.41 1 Jean 4.20 Genèse 49.23 1 Samuel 17.28 1 Jean 3.12
5 Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;
Genèse 28.12 Daniel 4.5 Jean 17.14 Amos 3.7 Joël 2.28
6 akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota.
Genèse 44.18 Juges 9.7
7 Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu.
Genèse 44.14 Genèse 42.9 Genèse 43.26 Genèse 42.6 Colossiens 1.18
8 Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatutawala sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake.
Luc 19.14 Genèse 49.26 Actes 4.27-4.28 1 Samuel 10.27 Hébreux 10.29
9 Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia.
Actes 7.9-7.14 Genèse 46.29 Genèse 45.9 Daniel 8.10 Genèse 44.19
10 Akawaambia baba yake na ndugu zake; baba yake akamkemea akamwambia, Ni ndoto gani hii uliyoiota? Je! Mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi?
Genèse 27.29 Esaïe 60.14 Philippiens 2.10-2.11 Genèse 37.7
11 Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.
Luc 2.51 Actes 7.9 Luc 2.19 Daniel 7.28 Esaïe 11.13
12 Ndugu zake wakaenda kuchunga kondoo za baba yao huko Shekemu.
Genèse 33.18 Genèse 34.25-34.31 Genèse 37.1
13 Israeli akamwambia Yusufu, Je! Ndugu zako hawachungi kondoo katika Shekemu? Njoo, nikutume kwao. Akamwambia, Mimi hapa.
Genèse 22.1 1 Samuel 3.16 Genèse 27.18 Matthieu 10.16 1 Samuel 3.4-3.6
14 Akamwambia, Enenda, basi, ukaone kama ndugu zako hawajambo, na kundi nalo li salama, ukaniletee habari. Basi akampeleka kutoka bonde la Hebroni, akafika Shekemu.
Genèse 35.27 Genèse 23.2 Genèse 13.18 Josué 14.15 1 Samuel 17.17-17.18
15 Mtu mmoja akamkuta, naye alikuwa anazunguka-zunguka katika nyika; yule mtu akamwuliza, akisema, Unatafuta nini?
Juges 4.22 Jean 4.27 Jean 1.38 Jean 18.7 Jean 18.4
16 Akasema, Nawatafuta ndugu zangu; tafadhali uniambie mahali wanakochunga.
Luc 19.10 Cantique 1.7
17 Yule mtu akasema, Wametoka hapa, maana niliwasikia wakisema, Twendeni Dothani. Basi Yusufu akawafuata ndugu zake akawakuta huko Dothani.
2 Rois 6.13
18 Wakamwona toka mbali, na kabla hajawakaribia, wakafanya shauri juu yake ili wamwue.
Psaumes 37.12 Actes 23.12 Psaumes 37.32 Marc 14.1 1 Samuel 19.1
19 Wakasemezana wao kwa wao, Tazama, yule bwana wa ndoto anakuja.
Genèse 37.11 Genèse 37.5 Genèse 49.23 Genèse 28.12
20 Haya, twende, tukamwue na kumtupa katika birika mojawapo, nasi tutasema, Mnyama mkali amemla; kisha tutaona zitakuwaje ndoto zake.
Marc 15.29-15.32 Jean 3.12 Actes 4.16-4.18 1 Samuel 26.2 1 Samuel 24.20
21 Reubeni akasikia akamwokoa katika mikono yao, akasema, Tusimwue.
Genèse 42.22 Genèse 9.5 Genèse 35.22 Matthieu 10.28 Josué 10.28
22 Reubeni akawaambia, Msimwage damu; mtupeni katika birika hii iliyopo nyikani, wala msimguse; ili apate kumwokoa katika mikono yao, akamrudishe kwa baba yake.
Deutéronome 13.9 Matthieu 27.24 Exode 24.11 Actes 12.1 Genèse 42.22
23 Ikawa Yusufu alipofika kwa ndugu zake, wakamvua Yusufu kanzu yake, kanzu ile ndefu aliyoivaa,
Genèse 37.3 Genèse 42.21 Genèse 37.31-37.33 Matthieu 27.28 Psaumes 22.18
24 wakamtwaa wakamtupa katika birika; na hiyo birika ilikuwa tupu, hamna maji.
Jérémie 38.6 Psaumes 35.7 Psaumes 130.1-130.2 Lamentations 3.52-3.55 Psaumes 88.6
25 Nao wakakaa kitako kula chakula; wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na zeri na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri.
Genèse 43.11 Genèse 37.28 Jérémie 8.22 Genèse 16.11-16.12 Genèse 37.36
26 Yuda akawaambia ndugu zake, Kwafaa nini kumwua ndugu yetu, na kuificha damu yake?
Genèse 37.20 Genèse 4.10 Deutéronome 17.8 Genèse 25.32 Job 16.18
27 Haya, na tumwuze kwa hawa Waishmaeli, wala mikono yetu isimdhuru, maana yeye ni ndugu yetu, na damu yetu. Ndugu zake wakakubali.
Genèse 42.21 1 Samuel 18.17 Genèse 37.22 Néhémie 5.8 Matthieu 26.15
28 Wakapita wafanya biashara Wamidiani; basi wakamtoa Yusufu, wakampandisha kumtoa katika birika, wakamwuza Yusufu kwa Waishmaeli kwa vipande vya fedha ishirini; nao wakamchukua Yusufu mpaka Misri.
Psaumes 105.17 Actes 7.9 Genèse 45.4-45.5 Juges 6.1-6.3 Genèse 25.2
29 Akarudi Reubeni birikani, kumbe! Yusufu hayumo katika birika, akararua nguo zake.
Job 1.20 Genèse 37.34 Nombres 14.6 Genèse 44.13 2 Rois 19.1
30 Akarudi kwa ndugu zake, akasema, Mtoto hayuko, nami niende wapi?
Genèse 42.13 Genèse 42.32 Jérémie 31.15 Genèse 42.35-42.36 Genèse 37.20
31 Wakaitwaa kanzu ya Yusufu, wakachinja mwana-mbuzi, na kuichovya kanzu katika damu.
Genèse 37.23 Genèse 37.3 Proverbes 28.13
32 Wakaenda nayo ile kanzu ndefu, wakamletea baba yao, wakasema, Tumeona hii; basi, utambue kama kanzu hii ni ya mwanao, ama siyo.
Genèse 44.20-44.23 Luc 15.30 Genèse 37.3
33 Akaitambua, akasema, Ndiyo kanzu ya mwanangu, mnyama mkali amemla; bila shaka Yusufu ameraruliwa.
Genèse 44.28 Genèse 37.20 1 Rois 13.24 Proverbes 14.15 2 Rois 2.24
34 Yakobo akararua mavazi yake, akajivika gunia viunoni, na kumlilia mwanawe siku nyingi.
Genèse 37.29 2 Samuel 3.31 1 Rois 21.27 Josué 7.6 Job 1.20
35 Wanawe wote, na binti zake wote, wakaondoka wamtulize, lakini akakataa kutulizwa, akasema, La! Nitamshukia mwanangu, nikisikitika, hata kuzimu. Baba yake akamlilia.
Genèse 42.38 2 Samuel 12.17 Genèse 35.22-35.26 Genèse 45.28 Genèse 31.43
36 Nao Wamidiani wakamwuza huko Misri, kwa Potifa, akida wa Farao, mkuu wa askari.
Genèse 37.28 Genèse 40.4 Esaïe 56.3 Esther 1.10 2 Rois 25.8

Cette Bible est dans le domaine public.