Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 34.8
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Dina, binti Lea, ambaye Lea alimzalia Yakobo, akatoka kuwaona binti za nchi.
Genèse 30.21 Genèse 46.15 Genèse 30.13 Genèse 28.6 Genèse 26.34
2 Shekemu, mwana wa Hamori, Mhivi, mkuu wa nchi, akamwona akamtwaa, akalala naye, akambikiri.
Matthieu 5.28 Genèse 10.17 Job 31.9 Genèse 20.2 Juges 14.1
3 Moyo wake ukaambatana na Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana, akasema na huyu msichana kwa maneno mazuri.
Osée 2.14 Ruth 1.14 Esaïe 40.2 2 Samuel 19.7 2 Chroniques 30.22
4 Shekemu akamwambia Hamori, babaye, akasema, Unipatie msichana huyu awe mke wangu.
Juges 14.2 2 Samuel 13.13 Genèse 21.21
5 Basi Yakobo akasikia ya kwamba amembikiri Dina, binti yake. Na wanawe walikuwako pamoja na wanyama wake nyikani. Yakobo akanyamaza, hata walipokuja.
2 Samuel 13.22 1 Samuel 16.11 1 Samuel 10.27 Lévitique 10.3 Genèse 30.35
6 Akatoka Hamori, babaye Shekemu, kumwendea Yakobo, aseme naye.
7 Wanawe Yakobo waliposikia hayo, wakaja kutoka nyikani; nao wakasikitika sana, wakakasirika mno, kwa sababu amefanya upumbavu katika Israeli kwa kulala na binti Yakobo, neno lisilojuzu kutendeka.
Juges 20.6 Josué 7.15 Deutéronome 22.21 Genèse 20.9 Hébreux 13.4
8 Hamori akasema nao, akinena, Roho ya Shekemu, mwanangu, inamtamani binti yenu, tafadhalini, mpeni amwoe.
1 Rois 11.2 Genèse 34.3 Psaumes 84.2 Psaumes 63.1 Psaumes 119.20
9 Mkaoane na sisi, mtupe sisi binti zenu, nanyi mkatwae binti zetu.
Deutéronome 7.3 Genèse 24.3 Genèse 26.34-26.35 Genèse 19.14 Genèse 27.46
10 Nanyi mtakaa nasi, na nchi hii itakuwa mbele yenu; kaeni, na kufanya biashara humo, mkapate mali humo.
Genèse 20.15 Genèse 47.27 Genèse 42.34 Genèse 13.9 Genèse 34.21-34.23
11 Shekemu akamwambia babaye yule msichana na nduguze, Na nikubalike machoni penu, na mtakavyoniambia nitatoa.
Genèse 33.15 Genèse 18.3
12 Mjapoongeza sana mahari na zawadi, nitatoa kadiri ya mtakavyoniambia, lakini mnipe huyu msichana, awe mke wangu.
Exode 22.16-22.17 Genèse 29.18 1 Samuel 18.25-18.27 Genèse 31.41 2 Samuel 3.14
13 Wana wa Yakobo wakawajibu Shekemu na Hamori babaye, kwa hila, maana amemharibu Dina, umbu lao,
Proverbes 24.28-24.29 Michée 7.2 1 Thessaloniciens 5.15 Psaumes 12.2 2 Samuel 13.23-13.29
14 wakawaambia, Hatuwezi kufanya neno hili, tumpe umbu letu mtu asiyetahiriwa; ingekuwa aibu kwetu.
1 Samuel 14.6 Genèse 17.11 Matthieu 2.13 1 Rois 21.9 1 Samuel 17.26
15 Lakini kwa sharti hii tu tutapatana nanyi; mkiwa kama sisi, akitahiriwa kila mwanamume wenu,
Galates 4.12
16 ndipo tutawapa ninyi binti yetu, na sisi tutatwaa binti zenu tutakaa pamoja nanyi, nasi tutakuwa watu wamoja.
17 Lakini kama hamtusikii na kutahiriwa, basi tutamtwaa umbu letu, nasi tutakwenda zetu.
18 Maneno yao yakawa mema machoni pa Hamori, na machoni pa Shekemu, mwana wa Hamori.
19 Na yule kijana hakukawia kulifanya neno lile, maana amependezewa na binti Yakobo, naye alikuwa mwenye heshima kuliko wote nyumbani mwa babaye.
1 Chroniques 4.9 Actes 17.12 2 Rois 5.1 Genèse 41.20 Cantique 8.6
20 Hamori, na Shekemu mwanawe, wakaja langoni pa mji wao, wakasema na watu wa mji wao, wakinena,
Ruth 4.1 Genèse 22.17 Job 29.7 Zacharie 8.16 Proverbes 31.23
21 Watu hawa wana amani nasi, basi na wakae katika nchi, na kufanya biashara humo; kwa maana nchi ni kubwa, yawatosha; na tuwatwae binti zao kuwa wake zetu, na binti zetu tuwape wao.
22 Lakini kwa sharti hiyo moja tu watapatana nasi wakae wote kwetu, tuwe watu wamoja, kama tukitahiriwa kila mwanamume, kama hawa walivyotahiriwa.
23 Je! Kondoo zao, na mali zao, na wanyama wao wote hawatakuwa mali zetu? Basi na tupatane nao tu, nao watakaa kwetu.
Proverbes 1.12-1.13 Jean 2.16 Proverbes 28.20 1 Timothée 6.6-6.10 Jean 6.26-6.27
24 Wakawasikia Hamori na Shekemu mwanawe, wote watokao katika lango la mji wake. Wakatahiriwa kila mwanamume, wote watokao katika lango la mji wake.
Genèse 23.10 Romains 2.28-2.29 Genèse 17.23 Genèse 23.18 Esaïe 1.10-1.16
25 Ikawa siku ya tatu, walipokuwa wakiumwa sana, wana wawili wa Yakobo, Simeoni na Lawi, nduguze Dina, wakatwaa kila mtu upanga wake, wakaujia mji kwa ujasiri, wakawaua waume wote.
Genèse 49.5-49.7 Genèse 29.33-29.34 Nombres 31.17 Nombres 31.7 Josué 5.6
26 Wakawaua Hamori, na Shekemu mwanawe, kwa makali ya upanga, wakamtwaa Dina katika nyumba ya Shekemu, wakatoka.
Esaïe 31.8 2 Samuel 2.26 Deutéronome 32.42
27 Wana wa Yakobo wakawajilia hao waliouawa, wakauteka nyara mji kwa sababu wamemharibu umbu lao.
1 Timothée 6.10 Exode 2.14 Esther 9.16 Genèse 34.2 Esther 9.10
28 Wakachukua kondoo zao, na ng’ombe zao, na punda zao, na vitu vilivyokuwamo mjini, navyo vilivyokuwako kondeni.
Job 20.5 Nombres 31.17 Job 1.15-1.16 Deutéronome 8.17-8.18
29 Wakatwaa na mali zao zote, na watoto wao wote, na wake zao, na vyote vilivyokuwamo nyumbani mwao wakavichukua mateka.
30 Yakobo akawaambia Simeoni na Lawi, Mmenitaabisha, kunifanya ninuke vibaya kati ya watu wa nchi hii, Wakanaani na Waperizi; na mimi, kwa kuwa watu wangu ni haba, watanikusanyikia, na kunipiga, nami nitaangamizwa, mimi na nyumba yangu.
Josué 7.25 Exode 5.21 1 Samuel 13.4 Psaumes 105.12 Genèse 13.7
31 Nao wakasema, Je! Ni vema amtendee umbu letu kama kahaba?
Proverbes 6.34 Genèse 49.7 Genèse 34.13

Cette Bible est dans le domaine public.