Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 34.23
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Dina, binti Lea, ambaye Lea alimzalia Yakobo, akatoka kuwaona binti za nchi.
Genèse 30.21 Jérémie 2.36 Tite 2.5 1 Timothée 5.13 Genèse 46.15
2 Shekemu, mwana wa Hamori, Mhivi, mkuu wa nchi, akamwona akamtwaa, akalala naye, akambikiri.
Deutéronome 22.29 Proverbes 13.20 Genèse 39.6-39.7 Deutéronome 21.14 Ezéchiel 22.10-22.11
3 Moyo wake ukaambatana na Dina binti Yakobo, akampenda huyu msichana, akasema na huyu msichana kwa maneno mazuri.
2 Samuel 19.7 2 Chroniques 30.22 1 Samuel 18.1 Osée 2.14 Ruth 1.14
4 Shekemu akamwambia Hamori, babaye, akasema, Unipatie msichana huyu awe mke wangu.
Juges 14.2 2 Samuel 13.13 Genèse 21.21
5 Basi Yakobo akasikia ya kwamba amembikiri Dina, binti yake. Na wanawe walikuwako pamoja na wanyama wake nyikani. Yakobo akanyamaza, hata walipokuja.
2 Samuel 13.22 Genèse 37.13-37.14 Luc 15.29 1 Samuel 16.11 1 Samuel 10.27
6 Akatoka Hamori, babaye Shekemu, kumwendea Yakobo, aseme naye.
7 Wanawe Yakobo waliposikia hayo, wakaja kutoka nyikani; nao wakasikitika sana, wakakasirika mno, kwa sababu amefanya upumbavu katika Israeli kwa kulala na binti Yakobo, neno lisilojuzu kutendeka.
Juges 20.6 Josué 7.15 Deutéronome 22.21 Genèse 20.9 Hébreux 13.4
8 Hamori akasema nao, akinena, Roho ya Shekemu, mwanangu, inamtamani binti yenu, tafadhalini, mpeni amwoe.
1 Rois 11.2 Psaumes 63.1 Psaumes 119.20 Genèse 34.3 Psaumes 84.2
9 Mkaoane na sisi, mtupe sisi binti zenu, nanyi mkatwae binti zetu.
Deutéronome 7.3 Genèse 27.46 Genèse 6.2 Genèse 24.3 Genèse 26.34-26.35
10 Nanyi mtakaa nasi, na nchi hii itakuwa mbele yenu; kaeni, na kufanya biashara humo, mkapate mali humo.
Genèse 42.34 Genèse 13.9 Genèse 20.15 Genèse 47.27 Genèse 34.21-34.23
11 Shekemu akamwambia babaye yule msichana na nduguze, Na nikubalike machoni penu, na mtakavyoniambia nitatoa.
Genèse 33.15 Genèse 18.3
12 Mjapoongeza sana mahari na zawadi, nitatoa kadiri ya mtakavyoniambia, lakini mnipe huyu msichana, awe mke wangu.
Exode 22.16-22.17 Genèse 24.53 Deutéronome 22.28-22.29 Genèse 29.18 1 Samuel 18.25-18.27
13 Wana wa Yakobo wakawajibu Shekemu na Hamori babaye, kwa hila, maana amemharibu Dina, umbu lao,
Esaïe 59.13 Juges 15.3 Proverbes 12.13 Job 13.7 Romains 12.19
14 wakawaambia, Hatuwezi kufanya neno hili, tumpe umbu letu mtu asiyetahiriwa; ingekuwa aibu kwetu.
2 Samuel 1.20 1 Samuel 17.36 Josué 5.2-5.9 1 Samuel 14.6 Genèse 17.11
15 Lakini kwa sharti hii tu tutapatana nanyi; mkiwa kama sisi, akitahiriwa kila mwanamume wenu,
Galates 4.12
16 ndipo tutawapa ninyi binti yetu, na sisi tutatwaa binti zenu tutakaa pamoja nanyi, nasi tutakuwa watu wamoja.
17 Lakini kama hamtusikii na kutahiriwa, basi tutamtwaa umbu letu, nasi tutakwenda zetu.
18 Maneno yao yakawa mema machoni pa Hamori, na machoni pa Shekemu, mwana wa Hamori.
19 Na yule kijana hakukawia kulifanya neno lile, maana amependezewa na binti Yakobo, naye alikuwa mwenye heshima kuliko wote nyumbani mwa babaye.
1 Chroniques 4.9 1 Samuel 22.14 Genèse 29.20 Actes 17.12 2 Rois 5.1
20 Hamori, na Shekemu mwanawe, wakaja langoni pa mji wao, wakasema na watu wa mji wao, wakinena,
Ruth 4.1 Amos 5.12 Deutéronome 17.5 Amos 5.15 Genèse 22.17
21 Watu hawa wana amani nasi, basi na wakae katika nchi, na kufanya biashara humo; kwa maana nchi ni kubwa, yawatosha; na tuwatwae binti zao kuwa wake zetu, na binti zetu tuwape wao.
22 Lakini kwa sharti hiyo moja tu watapatana nasi wakae wote kwetu, tuwe watu wamoja, kama tukitahiriwa kila mwanamume, kama hawa walivyotahiriwa.
23 Je! Kondoo zao, na mali zao, na wanyama wao wote hawatakuwa mali zetu? Basi na tupatane nao tu, nao watakaa kwetu.
Proverbes 1.12-1.13 Jean 6.26-6.27 Actes 19.24-19.26 Proverbes 23.4-23.5 Jean 2.16
24 Wakawasikia Hamori na Shekemu mwanawe, wote watokao katika lango la mji wake. Wakatahiriwa kila mwanamume, wote watokao katika lango la mji wake.
Genèse 23.10 1 Corinthiens 7.19 Matthieu 7.6 Romains 2.28-2.29 Genèse 17.23
25 Ikawa siku ya tatu, walipokuwa wakiumwa sana, wana wawili wa Yakobo, Simeoni na Lawi, nduguze Dina, wakatwaa kila mtu upanga wake, wakaujia mji kwa ujasiri, wakawaua waume wote.
Genèse 49.5-49.7 Genèse 29.33-29.34 Josué 5.8 2 Chroniques 32.25 Nombres 31.17
26 Wakawaua Hamori, na Shekemu mwanawe, kwa makali ya upanga, wakamtwaa Dina katika nyumba ya Shekemu, wakatoka.
Esaïe 31.8 2 Samuel 2.26 Deutéronome 32.42
27 Wana wa Yakobo wakawajilia hao waliouawa, wakauteka nyara mji kwa sababu wamemharibu umbu lao.
Genèse 34.31 Josué 7.21 Josué 7.13 1 Timothée 6.10 Exode 2.14
28 Wakachukua kondoo zao, na ng’ombe zao, na punda zao, na vitu vilivyokuwamo mjini, navyo vilivyokuwako kondeni.
Nombres 31.17 Job 1.15-1.16 Deutéronome 8.17-8.18 Job 20.5
29 Wakatwaa na mali zao zote, na watoto wao wote, na wake zao, na vyote vilivyokuwamo nyumbani mwao wakavichukua mateka.
30 Yakobo akawaambia Simeoni na Lawi, Mmenitaabisha, kunifanya ninuke vibaya kati ya watu wa nchi hii, Wakanaani na Waperizi; na mimi, kwa kuwa watu wangu ni haba, watanikusanyikia, na kunipiga, nami nitaangamizwa, mimi na nyumba yangu.
Psaumes 105.12 Josué 7.25 Exode 5.21 1 Samuel 13.4 Genèse 49.5-49.7
31 Nao wakasema, Je! Ni vema amtendee umbu letu kama kahaba?
Proverbes 6.34 Genèse 49.7 Genèse 34.13

Cette Bible est dans le domaine public.