Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ephésiens 6.21
Bible en Swahili de l’est


1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
Proverbes 23.22 Proverbes 6.20 Proverbes 1.8 Colossiens 3.20-3.25 Deutéronome 21.18
2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,
Exode 20.12 Deutéronome 27.16 Malachie 1.6 Proverbes 20.20 Marc 7.9-7.13
3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia.
Deutéronome 6.18 Psaumes 128.1-128.2 Deutéronome 4.40 Esaïe 3.10 Deutéronome 12.25
4 Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.
Colossiens 3.21 Proverbes 19.18 Proverbes 22.6 Deutéronome 6.7 Proverbes 29.15
5 Enyi watumwa, watiini wao walio bwana zenu kwa jinsi ya mwili, kwa hofu na kutetemeka, kwa unyofu wa moyo, kana kwamba ni kumtii Kristo;
Ephésiens 5.22 1 Pierre 2.18-2.21 Colossiens 3.17-3.24 Malachie 1.6 Tite 2.9-2.10
6 wala si kwa utumwa wa macho tu kama wajipendekazao kwa wanadamu bali kama watumwa wa Kristo, mkitenda yampendezayo Mungu kwa moyo;
Colossiens 3.22-3.23 1 Thessaloniciens 2.4 Galates 1.10 Matthieu 7.21 Philippiens 2.12
7 kwa nia njema kama kumtumikia Bwana wala si mwanadamu;
Genèse 31.38-31.40 Ephésiens 6.5-6.6 Colossiens 3.23 Genèse 31.6 1 Corinthiens 10.31
8 mkijua ya kuwa kila neno jema alitendalo mtu atapewa lilo hilo na Bwana kwamba ni mtumwa au kwamba ni huru.
Colossiens 3.24 Colossiens 3.11 Matthieu 16.27 2 Corinthiens 5.10 Galates 3.28
9 Nanyi, akina bwana, watendeeni wao yayo hayo, mkiacha kuwaogofya, huku mkijua ya kuwa yeye aliye Bwana wao na wenu yuko mbinguni, wala kwake hakuna upendeleo.
Actes 10.34 Jacques 2.8 Job 31.13-31.15 Colossiens 3.25-4.1 Jean 13.13

L’armure du chrétien

10 Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.
Ephésiens 1.19 1 Corinthiens 16.13 Philippiens 4.13 1 Pierre 5.10 Deutéronome 20.3-20.4
11 Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
2 Corinthiens 10.4 Romains 13.12 1 Pierre 5.8 Ephésiens 6.13 1 Thessaloniciens 5.8
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
Colossiens 1.13 Ephésiens 2.2 1 Corinthiens 9.25-9.27 Colossiens 2.15 2 Corinthiens 4.4
13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
Ephésiens 5.16 Ephésiens 6.11-6.17 2 Corinthiens 10.4 Ecclésiaste 12.1 Colossiens 4.12
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
Esaïe 59.17 Luc 12.35 1 Thessaloniciens 5.8 1 Pierre 1.13 Esaïe 11.5
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
Esaïe 52.7 Romains 10.15 2 Corinthiens 5.18-5.21 Luc 15.22
16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
1 Pierre 5.8-5.9 1 Jean 5.4-5.5 Genèse 15.1 Psaumes 56.3-56.4 Psaumes 56.10-56.11
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;
Hébreux 4.12 Esaïe 59.17 1 Thessaloniciens 5.8 Esaïe 49.2 Apocalypse 19.15
18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
1 Thessaloniciens 5.17 Colossiens 4.2 Philippiens 4.6 1 Timothée 2.1 Jude 1.20
19 pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;
Actes 4.29 Colossiens 4.3 1 Thessaloniciens 5.25 2 Corinthiens 3.12 2 Thessaloniciens 3.1
20 ambayo kwa ajili yake mimi ni mjumbe katika minyororo; hata nipate ujasiri katika huyo kunena jinsi inipasavyo kunena.
2 Corinthiens 5.20 Actes 28.20 Philémon 1.10 Philippiens 1.7 Ephésiens 3.1

Salutations

21 Basi ninyi nanyi mpate kuzijua habari zangu, ni hali gani, Tikiko, ndugu mpendwa, mhudumu mwaminifu katika Bwana, atawajulisheni mambo yote;
Actes 20.4 2 Timothée 4.12 Tite 3.12 Colossiens 4.7-4.9 1 Corinthiens 4.17
22 ambaye nampeleka kwenu kwa kusudi lilo hilo mpate kuzijua habari zetu, naye awafariji mioyo yenu.
Colossiens 4.7-4.8 Philippiens 2.25 2 Thessaloniciens 2.17 Colossiens 2.2 Philippiens 2.19
23 Amani na iwe kwa ndugu, na pendo, pamoja na imani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.
1 Pierre 5.14 Galates 6.16 Galates 5.6 Philémon 1.5-1.7 2 Thessaloniciens 3.16
24 Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.
Matthieu 22.37 Tite 2.7 Matthieu 28.20 Colossiens 4.18 2 Corinthiens 13.14

Cette Bible est dans le domaine public.