Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 15.39
Bible en Swahili de l’est


La question des non-Juifs et de la loi

1 Wakashuka watu waliotoka Uyahudi wakawafundisha wale ndugu ya kwamba, Msipotahiriwa kama desturi ya Musa hamwezi kuokoka.
Actes 15.24 Actes 15.5 Lévitique 12.3 1 Corinthiens 7.18-7.19 Galates 5.1-5.4
2 Basi baada ya Paulo na Barnaba kushindana na watu hawa na kuhojiana nao sana, ndugu wakaamuru kwamba Paulo na Barnaba na wengine miongoni mwao wapande kwenda Yerusalemu kwa mitume na wazee kwa habari ya swali hilo.
Actes 15.22-15.23 Actes 15.6-15.7 Actes 15.4 Actes 11.30 Galates 2.1-2.2
3 Basi, wakisafirishwa na kanisa, wakapita kati ya nchi ya Foinike na Samaria, wakitangaza habari za kuongoka kwao Mataifa; wakawafurahisha ndugu sana.
Actes 14.27 Tite 3.13 1 Corinthiens 16.11 Actes 21.5 1 Corinthiens 16.6
4 Walipofika Yerusalemu wakakaribishwa na kanisa na mitume na wazee, nao wakawaeleza mambo yote Mungu aliyoyafanya pamoja nao.
Actes 15.12 Actes 14.27 Actes 15.3 Actes 21.17 3 Jean 1.8-1.10
5 Lakini baadhi ya madhehebu ya Mafarisayo walioamini wakasimama wakisema, Ni lazima kuwatahiri na kuwaagiza kuishika torati ya Musa.
Actes 15.1 Actes 26.5-26.6 Galates 5.1-5.3 Actes 21.20 Actes 24.5
6 Mitume na wazee wakakusanyika wapate kulifikiri neno hilo.
Actes 15.25 Actes 15.4 Hébreux 13.17 Matthieu 18.20 Hébreux 13.7
7 Na baada ya hoja nyingi Petro akasimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini.
Actes 15.2 Actes 10.20 Romains 10.17-10.18 Galates 2.7-2.9 Actes 13.2
8 Na Mungu, ajuaye mioyo ya watu, akawashuhudia, akiwapa Roho Mtakatifu vile vile kama alivyotupa sisi;
Actes 1.24 Actes 2.4 Actes 14.3 Actes 10.47 Actes 10.44-10.45
9 wala hakufanya tofauti kati yetu sisi na wao, akiwasafisha mioyo yao kwa imani.
Actes 10.28 Romains 3.22 Actes 10.34 Actes 11.12 Ephésiens 3.6
10 Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulichukua.
Matthieu 23.4 Esaïe 7.12 Galates 5.1 Matthieu 11.28-11.30 Exode 17.2
11 Bali twaamini kwamba tutaokoka kwa neema ya Bwana Yesu vile vile kama wao.
Romains 3.24 Tite 3.4-3.7 2 Corinthiens 13.14 Galates 1.6 Apocalypse 5.9
12 Basi mkutano wote wakanyamaza, wakawasikiliza Barnaba na Paulo wakiwapasha habari za ishara na maajabu, ambayo Mungu aliyafanya kwa ujumbe wao katika Mataifa.
Actes 14.27 Actes 15.4 Actes 21.19 Jean 4.48
13 Na hao walipokwisha kunyamaza Yakobo akajibu, akisema, Ndugu zangu, nisikilizeni.
Actes 12.17 Marc 15.40 Actes 2.29 1 Corinthiens 14.30-14.33 Jacques 1.19
14 Simeoni ametueleza jinsi Mungu hapo kwanza alivyowaangalia Mataifa ili achague watu katika hao kwa ajili ya jina lake.
2 Pierre 1.1 Esaïe 43.21 Romains 11.36 1 Pierre 2.9-2.10 Esaïe 55.11-55.13
15 Na maneno ya manabii yapatana na hayo, kama ilivyoandikwa,
Actes 13.47 Romains 15.8-15.12
16 Baada ya mambo haya nitarejea, Nami nitaijenga tena nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena maanguko yake, Nami nitaisimamisha;
Amos 9.11-9.12 Esaïe 9.6-9.7 Psaumes 89.35-89.49 Luc 1.31-1.33 Matthieu 1.20-1.25
17 Ili wanadamu waliosalia wamtafute Bwana, Na mataifa yote ambao jina langu limetajwa kwao;
Zacharie 2.11 Osée 2.23 Zacharie 8.20-8.23 Jérémie 16.19 Genèse 22.18
18 Asema Bwana, ajulishaye hayo tangu milele.
Matthieu 13.35 Ephésiens 3.9 Esaïe 44.7 Ephésiens 1.4 2 Thessaloniciens 2.13
19 Kwa sababu hiyo mimi naamua hivi; Tusiwataabishe wale waliomgeukia Mungu katika Mataifa;
Actes 15.28 Galates 1.7-1.10 Esaïe 55.7 Actes 15.24 Osée 14.2
20 bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu.
Lévitique 3.17 Actes 15.29 Apocalypse 2.20 Apocalypse 2.14 Genèse 9.4
21 Kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi.
Actes 13.15 Actes 13.27 Néhémie 8.1-8.12 2 Corinthiens 3.14-3.15 Luc 4.16
22 Basi ikawapendeza mitume na wazee na kanisa lote kuwachagua watu miongoni mwao na kuwapeleka Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba; nao ni hawa, Yuda aliyeitwa Barsaba, na Sila, waliokuwa watu wakuu katika ndugu. Wakaandika hivi na kupeleka kwa mikono yao,
Actes 15.27 Actes 15.40 1 Pierre 5.12 Actes 15.32 Actes 17.10
23 Mitume na ndugu wazee, kwa ndugu zetu walioko Antiokia na Shamu na Kilikia, walio wa Mataifa; Salamu.
Jacques 1.1 Actes 23.26 Actes 15.22 Actes 15.41 Galates 1.21
24 Kwa kuwa tumesikia ya kwamba watu waliotoka kwetu wamewasumbua kwa maneno yao, wakipotosha roho zenu, ambao sisi hatukuwaagiza;
Actes 15.1 Galates 5.12 Galates 5.10 Tite 1.10-1.11 Galates 1.7
25 sisi tumeona vema, hali tumepatana kwa moyo mmoja, kuwachagua watu na kuwapeleka kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo,
2 Pierre 3.15 Actes 1.14 Actes 15.2 Colossiens 4.9 Actes 2.46
26 watu waliohatirisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
Actes 14.19 Actes 9.23-9.25 1 Corinthiens 15.30 Juges 5.18 2 Corinthiens 11.23-11.27
27 Basi tumewatuma Yuda na Sila, watakaowaambia wenyewe maneno yayo hayo kwa vinywa vyao.
Actes 15.22 3 Jean 1.13 2 Jean 1.12 Actes 15.32
28 Kwa maana ilimpendeza Roho Mtakatifu na sisi, tusiwatwike mzigo ila hayo yaliyo lazima,
Jean 16.13 Apocalypse 2.24 Actes 5.32 1 Corinthiens 7.40 Actes 15.19
29 yaani, mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati. Mkijizuia na hayo, mtafanya vema. Wasalamu.
Actes 15.20 Actes 21.25 2 Corinthiens 11.9 Apocalypse 2.20 Apocalypse 2.14
30 Hata hao wakiisha kupewa ruhusa wakatelemkia Antiokia; na baada ya kuwakusanya jamii yote wakawapa ile barua.
Actes 6.2 Actes 23.33 Actes 16.4 Actes 21.22
31 Nao walipokwisha kuisoma wakafurahi kwa ajili ya faraja ile.
Galates 5.1 Philippiens 3.3 Actes 16.5 Actes 15.10 Galates 2.4-2.5
32 Tena Yuda na Sila, kwa kuwa wao wenyewe ni manabii, wakawausia ndugu kwa maneno mengi, wakawathibitisha.
Actes 11.23 Actes 14.22 Actes 13.1 1 Pierre 5.12 Luc 11.49
33 Na wakiisha kukaa huko muda, wakaruhusiwa na ndugu waende kwa amani kwa hao waliowatuma. [
1 Corinthiens 16.11 Hébreux 11.31 Actes 16.36 Genèse 26.29 Marc 5.34
34 Lakini Sila akaona vema kukaa huko.]
35 Na Paulo na Barnaba wakakaa huko Antiokia, wakifundisha na kulihubiri neno la Bwana, pamoja na watu wengine wengi.
Actes 13.1 Colossiens 1.28 1 Timothée 2.7 Matthieu 28.19-28.20 Actes 8.4

Deuxième voyage missionnaire

De nouvelles équipes

36 Baada ya siku kadha wa kadha Paulo akamwambia Barnaba, Haya! Mrejee sasa tukawaangalie hao ndugu katika kila mji tulipolihubiri neno la Bwana, wa hali gani.
Actes 13.51 Actes 13.4 Actes 14.6 Actes 13.13-13.14 Actes 14.24-14.25
37 Barnaba akaazimu kumchukua Yohana aliyeitwa Marko pamoja nao.
Actes 12.12 Colossiens 4.10 Actes 13.5 Actes 12.25 Actes 13.13
38 Bali Paulo hakuona vema kumchukua huyo aliyewaacha huko Pamfilia, asiende nao kazini.
Actes 13.13 Luc 9.61 Psaumes 78.9 Luc 14.27-14.34 Proverbes 25.19
39 Basi palitokea mashindano baina yao hata wakatengana. Barnaba akamchukua Marko akatweka kwenda Kipro.
Colossiens 4.10 Actes 4.36 Actes 6.1 Actes 13.4-13.12 Actes 11.20
40 Lakini Paulo akamchagua Sila, akaondoka, akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana.
Actes 14.26 Actes 15.22 Actes 11.23 2 Jean 1.10-1.11 Actes 16.1-16.3
41 Akapita katika Shamu na Kilikia akiyathibitisha makanisa.
Actes 15.23 Actes 15.32 Galates 1.21 Actes 18.18 Actes 16.4-16.5

Cette Bible est dans le domaine public.