Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 4.50
Bible en Swahili de l’est


Jésus et la femme samaritaine

1 Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,
Jean 3.26 Jean 3.22 Jacques 2.1 2 Corinthiens 4.5 1 Corinthiens 2.8
2 (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,)
1 Corinthiens 1.13-1.17 Actes 10.48
3 aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.
Jean 3.22 Jean 11.54 Matthieu 10.23 Jean 1.43 Jean 10.40
4 Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.
Luc 2.49 Matthieu 10.5-10.6 Luc 17.11 Luc 9.51-9.52
5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.
Josué 24.32 Genèse 48.22 Genèse 33.19 Jean 4.12
6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
Matthieu 4.2 Matthieu 8.24 2 Corinthiens 8.9 Matthieu 27.45 Hébreux 4.15
7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
Genèse 24.43 2 Samuel 23.15-23.17 1 Rois 17.10 Matthieu 10.42 Jean 4.10
8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.
Jean 4.5 Jean 4.39 Jean 6.5-6.7 Luc 9.13
9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)
Actes 10.28 Jean 8.48 Jean 4.27 Luc 17.16-17.19 Matthieu 10.5
10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.
Jérémie 2.13 Jean 4.14 Apocalypse 22.17 Apocalypse 21.6 Apocalypse 7.17
11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai?
Jean 3.4 1 Corinthiens 2.14
12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?
Jean 4.6 Jean 8.53 Esaïe 53.2-53.3 Matthieu 12.42 Hébreux 3.3
13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
Esaïe 65.13-65.14 Jean 6.27 Luc 16.24 Jean 6.49
14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Jean 6.35 Esaïe 49.10 Apocalypse 7.16 Ephésiens 1.13-1.14 Jean 6.58
15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
Jean 6.34 Romains 8.5 Jean 17.2-17.3 Romains 6.23 Psaumes 4.6
16 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa.
Jean 4.18 Jean 21.17 Jean 1.47-1.48 Jean 2.24-2.25 Apocalypse 2.23
17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume;
18 kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.
Genèse 34.7-34.8 Genèse 34.2 Genèse 20.3 Jérémie 3.20 Marc 10.12
19 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!
Luc 7.39 Jean 6.14 Luc 7.16 Jean 9.17 Matthieu 21.11
20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.
Deutéronome 27.12 Deutéronome 11.29 Genèse 12.6-12.7 Genèse 33.18-33.20 Deutéronome 12.5-12.11
21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.
1 Timothée 2.8 Malachie 1.11 Jean 4.23 Ephésiens 3.14 Ephésiens 2.18
22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.
Esaïe 2.3 Romains 9.4-9.5 Psaumes 147.19 Actes 17.23 Romains 3.1-3.2
23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.
Philippiens 3.3 Galates 4.6 Jean 12.23 Jean 5.25 Ephésiens 6.18
24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
2 Corinthiens 3.17 Psaumes 51.17 Philippiens 3.3 1 Samuel 16.7 Esaïe 57.15
25 Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.
Jean 1.49 Jean 4.29 Jean 4.42 Jean 4.39 Matthieu 1.16
26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye.
Romains 10.20-10.21 Luc 13.30 Marc 14.61-14.62 Matthieu 20.15 Matthieu 26.63-26.64
27 Mara hiyo wakaja wanafunzi wake, wakastaajabu kwa sababu alikuwa akisema na mwanamke; lakini hakuna aliyesema, Unatafuta nini? Au, Mbona unasema naye?
Luc 7.39 Jean 4.8-4.9
28 Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu,
Jean 4.7 Luc 24.9 Marc 16.8-16.10 Matthieu 28.8 Luc 24.33
29 Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?
Jean 4.17-4.18 Jean 4.25 Jean 1.41-1.49 Apocalypse 22.17 Jean 7.31
30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea.
Matthieu 12.40-12.42 Actes 8.5-8.8 Esaïe 60.8 Luc 17.16-17.18 Actes 28.28
31 Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.
Jean 1.38 Matthieu 23.7 Actes 16.30-16.34 Genèse 24.33
32 Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.
Job 23.12 Psaumes 119.103 Jean 4.34 Jérémie 15.16 Esaïe 53.11
33 Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?
Matthieu 16.6-16.11 Luc 9.45
34 Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.
Jean 6.38 Jean 19.30 Jean 17.4 Jean 5.30 Job 23.12
35 Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno.
Luc 10.2-10.3 Matthieu 9.37-9.38 Jean 4.30
36 Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja.
Romains 1.13 1 Timothée 4.16 Daniel 12.3 2 Timothée 4.7-4.8 Romains 6.22
37 Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine.
Michée 6.15 Job 31.8 Luc 19.21 Juges 6.3
38 Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao.
Jean 1.7 Matthieu 11.8-11.13 Actes 8.14-8.17 Actes 10.42-10.43 2 Chroniques 36.15
39 Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.
Jean 4.29 Jean 4.5 Jean 10.41-10.42 Jean 11.45 Jean 4.42
40 Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili.
Luc 10.39 Jérémie 14.8 Luc 19.5-19.10 Proverbes 4.13 Luc 24.29
41 Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake.
Actes 8.25 Actes 8.12 Actes 15.3 Actes 1.8 Jean 6.63
42 Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu.
1 Jean 4.14 Jean 1.29 2 Corinthiens 5.19 Romains 10.11-10.13 Jean 4.29

Guérison du fils d’un officier

43 Na baada ya siku mbili hizo akaondoka huko, akaenda Galilaya.
Jean 4.40 Marc 7.27-7.28 Jean 1.42 Romains 15.8 Matthieu 4.13
44 Kwa maana Yesu mwenyewe alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.
Matthieu 13.57 Luc 4.24 Marc 6.4
45 Basi alipotoka Galilaya, Wagalilaya walimpokea; kwa kuwa wameyaona mambo yote aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu; maana hao nao waliiendea sikukuu.
Jean 2.23 Jean 3.2 Luc 8.40 Luc 9.53 Deutéronome 16.16
46 Basi alifika tena Kana ya Galilaya, hapo alipoyafanya yale maji kuwa divai. Na palikuwa na diwani mmoja ambaye mwanawe hawezi huko Kapernaumu.
Jean 2.1-2.11 Luc 8.42 Psaumes 78.34 Jean 21.2 Psaumes 50.15
47 Huyo aliposikia ya kwamba Yesu amekuja kutoka Uyahudi mpaka Galilaya, alimwendea, akamsihi ashuke na kumponya mwanawe; kwa maana alikuwa kufani.
Jean 4.3 Jean 4.54 Luc 7.6-7.8 Psaumes 46.1 Jean 11.32
48 Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?
Jean 20.29 1 Corinthiens 1.22 Hébreux 2.4 Daniel 4.2 Actes 2.22
49 Yule diwani akamwambia, Bwana, ushuke asijakufa mtoto wangu.
Marc 5.23 Marc 5.35-5.36 Psaumes 88.10-88.12 Psaumes 40.17
50 Yesu akamwambia, Enenda; mwanao yu hai. Mtu yule akalisadiki lile neno aliloambiwa na Yesu, naye akashika njia.
Matthieu 8.13 Luc 17.14 Jean 11.40 Marc 7.29-7.30 Romains 4.20-4.21
51 Hata alipokuwa akishuka, watumwa wake walimlaki, wakisema ya kwamba mtoto wake yu hai.
Jean 4.50 1 Rois 17.23 Jean 4.53
52 Basi akawauliza habari ya saa alipoanza kuwa hajambo; nao wakamwambia, Jana, saa saba, homa ilimwacha.
53 Basi babaye akafahamu ya kuwa ni saa ile ile aliyoambiwa na Yesu, Mwanao yu hai. Akaamini yeye na wote wa nyumbani mwake.
Actes 16.34 Actes 11.14 Actes 18.8 Actes 2.39 Matthieu 8.13
54 Hiyo ni ishara ya pili aliyoifanya Yesu, alipokuwa ametoka Uyahudi kufika Galilaya.
Jean 4.45 Jean 2.1-2.11

Cette Bible est dans le domaine public.