Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 5.2
Bible en Swahili de l’est


1 Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.
Marc 4.35 Luc 8.26-8.39 Matthieu 8.28-8.34
2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;
Marc 1.23 Esaïe 65.4 Marc 5.8 Luc 8.27 Marc 7.25
3 makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo;
Esaïe 65.4 Daniel 4.32-4.33 Marc 9.18-9.22 Luc 8.29
4 kwa sababu alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, akaikata ile minyororo, na kuzivunja-vunja zile pingu; wala hakuna mtu aliyekuwa na nguvu za kumshinda.
Jacques 3.7-3.8
5 Na sikuzote, usiku na mchana, alikuwako makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikata-kata kwa mawe.
Job 2.7-2.8 1 Rois 18.28 Jean 8.44
6 Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;
Jacques 2.19 Luc 4.41 Psaumes 72.9 Psaumes 66.3 Actes 16.17
7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese.
Matthieu 8.29 Actes 16.17 Matthieu 26.63 Matthieu 4.3 Apocalypse 12.12
8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu.
Marc 1.25 Marc 9.25-9.26 Actes 16.18
9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi.
Matthieu 26.53 Luc 8.30 Matthieu 12.45 Luc 11.21-11.26 Marc 5.15
10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
Marc 5.13 Marc 3.22
11 Na hapo milimani palikuwa na kundi kubwa la nguruwe, wakilisha.
Matthieu 8.30 Luc 8.32 Lévitique 11.7-11.8 Deutéronome 14.8 Esaïe 65.4
12 Pepo wote wakamsihi, wakisema, Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao.
2 Corinthiens 2.11 1 Pierre 5.8 Luc 22.31-22.32 Job 1.10-1.12 Job 2.5
13 Akawapa ruhusa. Wale pepo wachafu wakatoka, wakaingia katika wale nguruwe; nalo kundi lote likatelemka kwa kasi gengeni, wakaingia baharini, wapata elfu mbili; wakafa baharini.
Job 2.6 Job 1.12 Apocalypse 9.11 1 Rois 22.22 Apocalypse 13.5-13.7
14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea.
Luc 8.34 Matthieu 8.33
15 Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mwenye pepo, ameketi, amevaa nguo, ana akili zake, naye ndiye aliyekuwa na lile jeshi; wakaogopa.
Marc 5.9 2 Timothée 1.7 Colossiens 1.13 1 Samuel 16.4 1 Samuel 6.20-6.21
16 Na wale waliokuwa wameona waliwaeleza ni mambo gani yaliyompata yule mwenye pepo, na habari za nguruwe.
17 Wakaanza kumsihi aondoke mipakani mwao.
Matthieu 8.34 Luc 8.37 Actes 16.39 Marc 1.24 Marc 5.7
18 Naye alipokuwa akipanda chomboni, yule aliyekuwa na pepo akamsihi kwamba awe pamoja naye;
Luc 8.38-8.39 Marc 5.17 Psaumes 116.12 Luc 17.15-17.17 Philippiens 1.23-1.24
19 lakini hakumruhusu, bali alimwambia, Enenda zako nyumbani kwako, kwa watu wa kwenu, kawahubiri ni mambo gani makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokurehemu.
Psaumes 66.16 Jean 4.29 Daniel 6.25-6.27 Daniel 4.1-4.3 Daniel 4.37
20 Akaenda zake, akaanza kuhubiri katika Dekapoli, ni mambo gani makuu Yesu aliyomtendea; watu wote wakastaajabu.
Matthieu 4.25 Marc 7.31

Guérison d’une femme et résurrection d’une fillette

21 Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng’ambo katika kile chombo, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari.
Matthieu 9.1 Marc 4.1 Luc 8.40
22 Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake,
Actes 18.8 Actes 13.15 Actes 18.17 Luc 13.14 Marc 5.33
23 akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi.
Luc 13.13 Marc 16.18 Luc 4.40 Actes 28.8 2 Samuel 12.15-12.16
24 Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa.
Marc 5.31 Luc 8.45 Luc 8.42 Marc 3.20 Luc 12.1
25 Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili,
Lévitique 15.25-15.27 Luc 13.11 Luc 8.43-8.44 Matthieu 9.20-9.22 Lévitique 15.19-15.20
26 na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya
Jérémie 30.12-30.13 Jérémie 51.8 Psaumes 108.12 Job 13.4 Jérémie 8.22
27 aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake;
Actes 19.12 Actes 5.15 Matthieu 14.36 Marc 6.56 2 Rois 13.21
28 maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona.
29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule.
Marc 3.10 Marc 5.34 Exode 15.26 Luc 7.21 Job 33.24-33.25
30 Mara Yesu, hali akifahamu nafsini mwake kwamba nguvu zimemtoka, akageuka kati ya mkutano, akasema, Ni nani aliyenigusa mavazi yangu?
Luc 6.19 Luc 5.17 Luc 8.46 1 Pierre 2.9
31 Wanafunzi wake wakamwambia, Je! Wawaona makutano wanavyokusonga-songa, nawe wasema, Ni nani aliyenigusa?
Luc 8.45 Luc 9.12
32 Akatazama pande zote ili amwone yule aliyelitenda neno hilo.
33 Na yule mwanamke akaingiwa na hofu na kutetemeka, akijua lililompata, akaja akamwangukia, akamweleza kweli yote.
Luc 1.29 Luc 1.12 Luc 8.47 Psaumes 103.2-103.5 Psaumes 30.2
34 Akamwambia, Binti, imani yako imekuponya, enenda zako kwa amani, uwe mzima, usiwe na msiba wako tena.
Luc 8.48 Matthieu 9.22 Luc 7.50 Luc 18.42 1 Samuel 1.17
35 Hata alipokuwa katika kunena, wakaja watu kutoka kwa yule mkuu wa sinagogi, wakisema, Binti yako amekwisha kufa; kwani kuzidi kumsumbua mwalimu?
Jean 11.28 Marc 5.22 Luc 7.6-7.7 Jean 11.39 Jean 5.25
36 Lakini Yesu, alipolisikia lile neno likinenwa, akamwambia mkuu wa sinagogi, Usiogope, amini tu.
Luc 8.50 Romains 4.18-4.24 Matthieu 9.28-9.29 Marc 5.34 Marc 9.23
37 Wala hakumruhusu mtu afuatane naye, ila Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye Yakobo.
Marc 9.2 Marc 14.33 Actes 9.40 Luc 8.51 2 Corinthiens 13.1
38 Wakafika nyumbani kwa yule mkuu wa sinagogi, akaona ghasia, na watu wakilia, wakifanya maombolezo makuu.
Matthieu 9.23-9.24 Luc 8.52-8.53 Matthieu 11.17 Marc 5.22 Jérémie 9.17-9.20
39 Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu.
Actes 20.10 Daniel 12.2 1 Thessaloniciens 5.10 Jean 11.11-11.13 1 Corinthiens 11.30
40 Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana.
Luc 8.53-8.54 Actes 17.32 Psaumes 123.3-123.4 Job 12.4 Matthieu 7.6
41 Akamshika mkono kijana, akamwambia, Talitha, kumi; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka.
Jean 5.28-5.29 Marc 1.31 Jean 11.43-11.44 Luc 7.14-7.15 Luc 8.54-8.55
42 Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu.
Marc 6.51 Marc 7.37 Actes 3.10-3.13 Marc 1.27 Marc 4.41
43 Akawaonya sana, mtu asijue habari ile; akaamuru apewe chakula.
Matthieu 8.4 Jean 5.41 Luc 8.56 Marc 3.12 Luc 24.42-24.43

Cette Bible est dans le domaine public.