Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 1.27
Bible en Swahili de l’est


De Jean-Baptiste à Jésus

Ministère de Jean-Baptiste

1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
Matthieu 14.33 1 Jean 5.11-5.12 Romains 8.32 Matthieu 17.5 Matthieu 4.3
2 Kama ilivyoandikwa katika nabii Isaya, Tazama, namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako.
Malachie 3.1 Matthieu 11.10 Luc 1.76 Matthieu 2.5 Luc 3.2-3.16
3 Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.
Esaïe 40.3-40.5 Matthieu 3.3 Luc 3.4-3.6 Jean 3.28-3.36 Jean 1.19-1.34
4 Yohana alitokea, akibatiza nyikani, na kuuhubiri ubatizo wa toba liletalo ondoleo la dhambi.
Luc 1.77 Jean 3.23 Matthieu 3.11 Matthieu 3.6 Actes 22.16
5 Wakamwendea nchi yote ya Uyahudi, nao wa Yerusalemu wote, wakabatizwa katika mto wa Yordani, wakiziungama dhambi zao.
Actes 19.18 Lévitique 26.40-26.42 Actes 2.38 1 Jean 1.8-1.10 Psaumes 32.5
6 Na Yohana alikuwa amevaa singa za ngamia na mshipi wa ngozi kiunoni mwake, akala nzige na asali ya mwitu.
2 Rois 1.8 Lévitique 11.22 Zacharie 13.4 Matthieu 3.4
7 Akahubiri akisema, Yuaja nyuma yangu aliye na nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuinama na kuilegeza gidamu ya viatu vyake.
Actes 13.25 Jean 1.27 Luc 3.16 Jean 3.28-3.31 Luc 7.6-7.7
8 Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.
Actes 1.5 Actes 2.4 Actes 19.4-19.6 Joël 2.28 Matthieu 3.11
9 Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani.
Matthieu 2.23 Matthieu 3.13-3.17 Luc 3.21-3.22
10 Mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu zinapasuka, na Roho, kama hua, akishuka juu yake;
Luc 3.22 Matthieu 3.16 Esaïe 64.1 Esaïe 42.1 Jean 1.31-1.34
11 na sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.
Esaïe 42.1 Marc 9.7 Matthieu 3.17 Psaumes 2.7 Jean 3.16
12 Mara Roho akamtoa aende nyikani.
Matthieu 4.1-4.11 Luc 4.1-4.13
13 Akawako huko jangwani siku arobaini, hali akijaribiwa na Shetani; naye alikuwa pamoja na wanyama wa mwitu, na malaika walikuwa wakimhudumia.
Matthieu 26.53 Hébreux 4.15 Exode 34.28 1 Timothée 3.16 Matthieu 4.10-4.11

Premiers disciples de Jésus

14 Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu,
Matthieu 4.23 Matthieu 4.12 Esaïe 61.1-61.3 Ephésiens 2.17 Matthieu 14.2
15 akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili.
Ephésiens 1.10 Matthieu 3.2 Galates 4.4 Matthieu 4.17 Actes 20.21
16 Naye alipokuwa akipita kando ya bahari ya Galilaya, akamwona Simoni na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.
Matthieu 4.18-4.22 Jean 1.40-1.42 Matthieu 10.2 Luc 5.1-5.11 Marc 1.16-1.20
17 Yesu akawaambia, Njoni mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
Luc 5.10 Matthieu 4.19-4.20 Actes 2.38-2.41 Ezéchiel 47.10
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
Luc 5.11 Marc 10.28-10.31 Philippiens 3.8 Matthieu 19.27-19.30 Luc 14.33
19 Akaendelea mbele kidogo, akamwona Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, nao pia walikuwa chomboni, wakizitengeneza nyavu zao.
Matthieu 4.21 Marc 5.37 Actes 12.2 Marc 9.2 Marc 10.35
20 Mara akawaita, wakamwacha baba yao Zebedayo ndani ya chombo pamoja na watu wa mshahara, wakaenda, wakamfuata.
Matthieu 8.21-8.22 Marc 10.29 1 Rois 19.20 Matthieu 4.21-4.22 Deutéronome 33.9

Ministère de Jésus en Galilée

Miracles à Capernaüm

21 Wakashika njia mpaka Kapernaumu, na mara siku ya sabato akaingia katika sinagogi, akafundisha.
Matthieu 4.23 Marc 6.2 Marc 1.39 Matthieu 4.13 Luc 10.15
22 Wakashangaa mno kwa mafundisho yake; kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi.
Matthieu 7.28-7.29 Jérémie 23.29 Actes 9.21-9.22 Marc 7.3-7.13 Hébreux 4.12-4.13
23 Na mara palikuwapo ndani ya sinagogi lao mtu mwenye pepo mchafu; akapaza sauti,
Marc 5.2 Luc 4.33-4.37 Marc 9.25 Marc 7.25 Marc 1.34
24 akisema, Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je! Umekuja kutuangamiza?
Actes 3.14 Matthieu 8.29 Apocalypse 3.7 Luc 4.34 Jacques 2.19
25 Nakutambua u nani, Mtakatifu wa Mungu. Yesu akamkemea, akisema, Fumba kinywa, umtoke.
Marc 1.34 Marc 9.25 Luc 4.41 Marc 3.11-3.12 Actes 16.17
26 Yule pepo mchafu akamtia kifafa, akalia kwa sauti kuu, akamtoka.
Marc 9.20 Marc 9.26 Luc 9.42 Luc 11.22 Luc 9.39
27 Wakashangaa wote, hata wakaulizana, wakisema, Nini hii? Ni elimu mpya! Maana kwa uweza awaamuru hata pepo wachafu, nao wamtii!
Luc 9.1 Matthieu 12.22-12.23 Marc 10.32 Luc 4.36 Marc 10.24
28 Habari zake zikaenea mara kotekote katika nchi zote kandokando ya Galilaya.
Marc 1.45 Matthieu 4.24 Luc 4.17 Michée 5.4 Matthieu 9.31
29 Na mara walipotoka katika sinagogi, walifika nyumbani kwa Simoni na Andrea, pamoja na Yakobo na Yohana.
Luc 4.38-4.39 Matthieu 8.14-8.15 Marc 1.21 Marc 1.23 Luc 9.58
30 Naye mkwewe Simoni, mamaye mkewe, alikuwa kitandani, hawezi homa; na mara wakamwambia habari zake.
1 Corinthiens 9.5 Jean 11.3 Jacques 5.14-5.15 Marc 5.23
31 Akamkaribia, akamwinua kwa kumshika mkono, homa ikamwacha, akawatumikia.
Actes 9.41 Psaumes 116.12 Marc 5.41 Psaumes 103.1-103.3 Luc 8.2-8.3
32 Hata kulipokuwa jioni, na jua limekwisha kuchwa, walikuwa wakimletea wote waliokuwa hawawezi, na wenye pepo.
Matthieu 8.16 Luc 4.40 Matthieu 4.24 Marc 3.2 Marc 1.21
33 Na mji wote ulikuwa umekusanyika mlangoni.
Marc 1.5 Actes 13.44
34 Akaponya wengi waliokuwa na maradhi mbalimbali, akatoa pepo wengi, wala hakuwaacha pepo kunena, kwa sababu walimjua.
Marc 3.12 Luc 4.41 Matthieu 4.23 Actes 16.16-16.18 Marc 1.25

Guérisons en Galilée

35 Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.
Luc 22.39-22.46 Ephésiens 6.18 Hébreux 5.7 Philippiens 2.5 Luc 5.16
36 Simoni na wenziwe wakamfuata;
37 nao walipomwona wakamwambia, Watu wote wanakutafuta.
Jean 12.19 Jean 3.26 Zacharie 11.11 Jean 11.48 Marc 1.5
38 Akawaambia, Twendeni mahali pengine, mpaka vijiji vilivyo karibu, nipate kuhubiri huko nako; maana kwa hiyo nalitokea.
Luc 4.43 Jean 16.28 Jean 17.4 Luc 2.49 Jean 17.8
39 Akaenda akihubiri katika masinagogi yao, katika nchi yote ya Galilaya, na kutoa pepo.
Matthieu 4.23 Marc 1.21 Marc 7.30 Luc 4.43-4.44 Luc 4.41
40 Akaja kwake mtu mwenye ukoma, akamsihi na kumpigia magoti, na kumwambia, Ukitaka, waweza kunitakasa.
Marc 10.17 Luc 5.12-5.14 Matthieu 8.2-8.4 Marc 9.22-9.23 Matthieu 17.14
41 Naye akamhurumia, akanyosha mkono wake, akamgusa, akamwambia, Nataka, takasika.
Genèse 1.3 Matthieu 9.36 Marc 6.34 Hébreux 1.3 Marc 4.39
42 Na mara ukoma wake ukamtoka, akatakasika.
Marc 1.31 Psaumes 33.9 Jean 4.50-4.53 Matthieu 15.28 Jean 15.3
43 Akamkataza kwa nguvu, akamwondoa mara,
Matthieu 9.30 Marc 7.36 Luc 8.56 Marc 5.43 Marc 3.12
44 akamwambia, Angalia, usimwambie mtu neno lolote, ila enenda zako ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe alivyoamuru Musa kwa kutakasika kwako, iwe ushuhuda kwao.
Matthieu 8.4 Lévitique 14.1-14.32 Luc 17.14 Matthieu 23.2-23.3 Romains 15.4
45 Lakini akatoka, akaanza kuhubiri maneno mengi, na kulitangaza lile neno, hata Yesu asiweze tena kuingia mjini kwa wazi; bali alikuwako nje mahali pasipokuwa na watu, wakamwendea kutoka kila mahali.
Marc 2.13 Matthieu 9.31 Jean 6.2 Marc 3.7 Matthieu 28.15

Cette Bible est dans le domaine public.