Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 71
Bible en Swahili de l’est


Prière confiante d’un vieil homme persécuté

1 Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele.
Psaumes 31.1-31.3 Psaumes 25.2-25.3 Psaumes 125.1 Psaumes 146.5 Psaumes 22.5
2 Kwa haki yako uniponye, uniopoe, Unitegee sikio lako, uniokoe.
Psaumes 17.6 Psaumes 31.1 1 Corinthiens 10.13 Daniel 9.16 Psaumes 17.2
3 Uwe kwangu mwamba wa makazi yangu, Nitakakokwenda sikuzote. Umeamuru niokolewe, Ndiwe genge langu na ngome yangu.
Psaumes 18.2 Psaumes 31.2-31.3 Psaumes 44.4 Apocalypse 7.2-7.3 Psaumes 91.1-91.2
4 Ee Mungu wangu, uniopoe mkononi mwa mkorofi, Katika mkono wake mwovu, mdhalimu,
2 Samuel 17.1-17.2 Psaumes 17.13 Psaumes 59.1-59.2 Psaumes 140.1-140.4 2 Samuel 16.21-16.22
5 Maana ndiwe taraja langu, Ee Bwana MUNGU, Tumaini langu tokea ujana wangu.
Jérémie 17.7 Jérémie 17.13 Psaumes 39.7 1 Samuel 17.45-17.47 Psaumes 71.17
6 Nimekutegemea Wewe tangu kuzaliwa, Ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu, Ninakusifu Wewe daima.
Psaumes 22.9-22.10 Psaumes 139.15-139.16 Psaumes 34.1 Jérémie 1.5 Esaïe 49.5
7 Nimekuwa kitu cha ajabu kwa watu wengi, Na Wewe ndiwe kimbilio langu la nguvu.
1 Corinthiens 4.9 Esaïe 8.18 Psaumes 61.3 Luc 2.34 2 Corinthiens 4.8-4.12
8 Kinywa changu kitajazwa sifa zako, Na heshima yako mchana kutwa.
Psaumes 146.2 Psaumes 35.28 Psaumes 104.1 Psaumes 71.15 Psaumes 51.14-51.15
9 Usinitupe wakati wa uzee, Nguvu zangu zipungukapo usiniache.
Psaumes 71.18 Esaïe 46.4 Psaumes 92.13-92.15 Psaumes 90.10 Ecclésiaste 12.1-12.7
10 Kwa maana adui zangu wananiamba, Nao wanaoniotea roho yangu hushauriana.
Psaumes 56.6 Matthieu 27.1 Psaumes 83.3 2 Samuel 17.1-17.14 Psaumes 10.9
11 Wakisema, Mungu amemwacha, Mfuatieni, mkamateni, hakuna wa kumponya.
Psaumes 7.2 Psaumes 3.2 Psaumes 41.7-41.8 Matthieu 27.42-27.43 Daniel 3.15
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami; Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia.
Psaumes 38.21-38.22 Psaumes 35.22 Psaumes 22.11 Psaumes 22.19 Psaumes 10.1
13 Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya.
Psaumes 109.29 Psaumes 71.24 Psaumes 35.4 Psaumes 35.26 Psaumes 132.18
14 Nami nitatumaini daima, Nitazidi kuongeza sifa zake zote.
Lamentations 3.26 1 Jean 3.3 1 Thessaloniciens 4.10 Philippiens 1.9 Psaumes 43.5
15 Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa; maana sijui hesabu yake.
Psaumes 40.5 Psaumes 35.28 Psaumes 145.2 Psaumes 71.8 Psaumes 89.16
16 Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako.
Psaumes 51.14 Psaumes 29.11 Philippiens 3.9 Esaïe 63.7 2 Thessaloniciens 1.6
17 Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo.
1 Chroniques 16.4-16.36 2 Samuel 4.9 Psaumes 66.16 Psaumes 119.102 1 Samuel 17.36-17.37
18 Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, Na kila atakayekuja uweza wako.
Psaumes 71.9 Esaïe 46.4 Psaumes 78.4 Exode 13.8 Psaumes 78.6
19 Na haki yako, Ee Mungu, Imefika juu sana. Wewe uliyefanya mambo makuu; Ee Mungu, ni nani aliye kama Wewe?
Psaumes 35.10 Psaumes 57.10 Psaumes 36.5-36.6 Esaïe 55.9 Psaumes 89.6-89.8
20 Wewe, uliyetuonyesha mateso mengi, mabaya, Utatuhuisha tena. Utatupandisha juu tena Tokea pande za chini ya nchi.
Psaumes 60.3 Psaumes 80.18 Psaumes 138.7 Osée 6.1-6.2 Psaumes 86.13
21 Laiti ungeniongezea ukuu! Urejee tena na kunifariji moyo.
2 Samuel 3.1 2 Corinthiens 7.6 Apocalypse 11.15 Esaïe 12.1 2 Corinthiens 7.13
22 Nami nitakushukuru kwa kinanda, Na kweli yako, Ee Mungu wangu. Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.
2 Rois 19.22 Psaumes 33.2 Psaumes 89.18 Esaïe 60.9 Psaumes 92.1-92.3
23 Midomo yangu itafurahi sana nikuimbiapo, Na nafsi yangu uliyoikomboa.
Psaumes 103.4 Psaumes 104.33 Luc 1.46-1.47 Psaumes 34.22 2 Samuel 4.9
24 Ulimi wangu nao utasimulia Haki yako mchana kutwa. Kwa maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya.
Psaumes 71.13 Psaumes 35.28 Matthieu 12.35 Psaumes 92.11 1 Corinthiens 15.25

Cette Bible est dans le domaine public.