Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 11.14
Bible en Swahili de l’est


Répartition des nouveaux habitants

1 Basi, wakuu wa watu walikuwa wakikaa Yerusalemu; nao watu waliosalia wakapiga kura, ili katika watu kumi kumleta mmoja akae ndani ya Yerusalemu mji mtakatifu, na wale kenda wakae mijini.
Néhémie 11.18 Esaïe 48.2 Néhémie 10.34 Esaïe 52.1 Matthieu 27.53
2 Na hao watu wakawabariki wote waliojitoa kwa hiari wakae Yerusalemu.
Juges 5.9 2 Corinthiens 8.16-8.17 Job 31.20 Deutéronome 24.13 Job 29.13
3 Basi hawa ndio wakuu wa jimbo waliokaa Yerusalemu; ila mijini mwa Yuda wakakaa kila mtu katika milki yake mijini mwao, yaani, Israeli, makuhani, na Walawi, na Wanethini, na akina watumwa wa Sulemani.
Esdras 2.43 Néhémie 7.73 Esdras 2.1 Néhémie 7.57-7.60 Néhémie 7.6
4 Tena wakakaa Yerusalemu wengine wa wana wa Yuda, na wengine wa wana wa Benyamini. Wa wana wa Yuda; Athaya, mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, wa wana wa Peresi;
Genèse 38.29 Ruth 4.18 Matthieu 1.3 1 Chroniques 9.3-9.9 Luc 3.33
5 na Maaseya, mwana wa Baruki, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, Mshelani.
Nombres 26.20 Genèse 38.5 1 Chroniques 4.21 Néhémie 3.15 1 Chroniques 9.5
6 Wana wa Peresi wote waliokaa Yerusalemu walikuwa watu mia nne sitini na wanane, mashujaa.
7 Na wana wa Benyamini ndio hawa; Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseva, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya.
1 Chroniques 9.7-9.9
8 Na baada yake Gabai, Salai, watu mia kenda ishirini na wanane.
9 Na Yoeli, mwana wa Zikri, alikuwa msimamizi wao; na Yuda, mwana wa Hasenua, alikuwa wa pili juu ya mji.
1 Chroniques 9.7
10 Wa makuhani; Yedaya, Yoyaribu, Yakini,
Esdras 8.16 Néhémie 12.6 1 Chroniques 9.10 Néhémie 7.39 Néhémie 12.19
11 na Seraya, mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi wa nyumba ya Mungu,
Actes 5.24 1 Chroniques 9.1 Nombres 3.32 1 Chroniques 6.7-6.14 1 Chroniques 9.11
12 na ndugu zao waliofanya kazi ya nyumbani, watu mia nane ishirini na wawili; na Adaya, mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amzi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
1 Chroniques 9.12-9.13
13 na ndugu zake, wakuu wa mbari za mababa, watu mia mbili arobaini na wawili; na Maasai, mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
14 na ndugu zao, waume mashujaa, watu mia na ishirini na wanane; na msimamizi wao alikuwa Zabdieli, mmojawapo wa hao wakuu.
15 Na wa Walawi; Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
1 Chroniques 9.19 1 Chroniques 9.14
16 na Shabethai na Yozabadi, wa wakuu wa Walawi, walioisimamia kazi ya nje ya nyumba ya Mungu;
1 Chroniques 26.20 Esdras 8.33 Actes 6.2-6.3 Néhémie 8.7 1 Chroniques 26.29
17 na Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu, mkuu mwenye kuanzisha shukrani katika sala, na Bakbukia, wa pili wake miongoni mwa nduguze; na Obadia, mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
1 Chroniques 9.15 1 Thessaloniciens 5.17-5.18 1 Chroniques 16.4 Néhémie 12.25 1 Chroniques 16.41
18 Walawi wote waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu mia mbili themanini na wanne.
Néhémie 11.1 Apocalypse 21.2 Daniel 9.24 Matthieu 27.53 Apocalypse 11.2
19 Pamoja na hao, mabawabu; Akubu, Talmoni, na ndugu zao waliolinda malangoni, walikuwa watu mia na sabini na wawili.
Psaumes 84.10 1 Chroniques 9.17-9.22 Néhémie 7.45 Néhémie 12.25
20 Na Israeli waliosalia, katika hao makuhani, na Walawi, walikuwamo mijini mwote mwa Yuda, kila mtu katika milki yake.
Néhémie 11.3
21 Lakini Wanethini walikuwa wakikaa Ofeli; na juu ya Wanethini walikuwa Siha na Gishpa.
Néhémie 3.26 Néhémie 3.31 2 Chroniques 27.3
22 Naye msimamizi wa Walawi huko Yerusalemu, ni Uzi, mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, hao waimbaji, alikuwa juu ya kazi ya nyumba ya Mungu.
Néhémie 12.42 Néhémie 11.9 Néhémie 11.14 1 Chroniques 25.1-25.6 Néhémie 11.11
23 Kwa kuwa palikuwa na amri ya mfalme juu yao, na agizo la hakika walilowekewa waimbaji, kama ilivyohusika na kila siku.
Esdras 6.8-6.9 Esdras 7.20-7.24 1 Chroniques 9.33 Néhémie 12.47
24 Na Pethahia, mwana wa Meshezabeli, wa wana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa wakili wa mfalme kwa habari ya mambo yote ya watu.
Genèse 38.30 1 Chroniques 18.17 Nombres 26.20 1 Chroniques 23.28 Néhémie 10.21
25 Na katika habari za vijiji na mashamba yake; wengine wa wana wa Yuda walikuwa wakikaa Kiriath-arba na vijiji vyake, na katika Diboni na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake;
Josué 14.15 Josué 15.21-15.22
26 na katika Yeshua, na Molada, na Beth-peleti;
Josué 19.2 Josué 15.26-15.27
27 na Hazar-shuali, na Beer-sheba na vijiji vyake;
Josué 15.28 Genèse 26.33 Josué 19.3 Juges 20.1 Genèse 21.31
28 na katika Siklagi, na Mekona na vijiji vyake;
1 Samuel 27.6 Josué 15.31
29 na katika Enrimoni, na Sora, na Yarmuthi;
Josué 15.32-15.33 Josué 12.11 Juges 13.25 Josué 19.41 Josué 15.35
30 Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, Lakishi na mashamba yake, Azeka na vijiji vyake. Hivyo wakatua toka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.
Josué 15.8 Josué 10.3 Jérémie 19.6 Esaïe 37.8 Michée 1.15
31 Wana wa Benyamini nao walikuwa wakikaa Geba, na Mikmashi, na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake;
Esaïe 10.28 Josué 18.24 Josué 8.9 Genèse 28.19 Néhémie 7.30-7.32
32 Anathothi, Nobu, Anania;
Josué 21.18 Esaïe 10.30 1 Samuel 21.1 1 Samuel 22.19 Néhémie 7.27
33 Hazori, Rama, Gitaimu;
2 Samuel 4.3 1 Samuel 7.17 Josué 18.25 Matthieu 2.18
34 Hadidi, Seboimu, Nebalati;
1 Samuel 13.18
35 Lodi, na Ono, bonde la Wakarashi.
1 Chroniques 8.12 1 Chroniques 4.14 Néhémie 7.37
36 Na wa Walawi, wengine walikaa katika Yuda na wengine katika Benyamini.
Josué 21.1-21.45 1 Chroniques 6.54-6.81 Genèse 49.7

Cette Bible est dans le domaine public.