Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esdras 2.21
Bible en Swahili de l’est


Liste des Israélites revenus d’exil

1 Basi hawa ndio wana wa wilaya, waliokwea kutoka katika ule uhamisho wa hao waliokuwa wamechukuliwa, ambao Nebukadneza, mfalme wa Babeli, aliwachukua mateka mpaka Babeli, nao wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mtu mjini kwake;
Néhémie 7.6-7.73 2 Rois 24.14-24.16 2 Rois 25.11 2 Chroniques 36.1-36.23 Sophonie 2.7
2 ndio hawa waliokuja pamoja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu, na Baana. Hii ndiyo hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli;
Néhémie 7.7 Aggée 1.12 Aggée 2.4 Aggée 1.14 Esdras 4.3
3 wana wa Paroshi, elfu mbili mia moja sabini na wawili.
Esdras 8.3 Esdras 10.25 Néhémie 7.8
4 Wana wa Shefatia, mia tatu sabini na wawili.
Néhémie 7.9 Esdras 8.8
5 Wana wa Ara, mia saba sabini na watano.
Néhémie 7.10 Néhémie 6.18
6 Wana wa Pahath-Moabu, wa wana wa Yeshua na Yoabu, elfu mbili mia nane na kumi na wawili.
Néhémie 7.11 Esdras 8.4 Esdras 10.30 Esdras 8.9 Esdras 10.14
7 Wana wa Elamu, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
Néhémie 7.12 Esdras 10.26 Esdras 2.31 Esdras 8.7
8 Wana wa Zatu, mia kenda arobaini na watano.
Néhémie 7.13 Esdras 10.27
9 Wana wa Zakai, mia saba na sitini.
Néhémie 7.14
10 Wana wa Binui, mia sita arobaini na wawili.
Néhémie 7.15 Esdras 10.34
11 Wana wa Bebai, mia sita ishirini na watatu.
Esdras 8.11 Néhémie 7.16 Esdras 10.28
12 Wana wa Azgadi, elfu moja mia mbili ishirini na wawili.
Néhémie 7.17 Esdras 8.12
13 Wana wa Adonikamu, mia sita sitini na sita.
Esdras 8.13 Néhémie 7.18
14 Wana wa Bigwai, elfu mbili hamsini na sita.
Esdras 8.14 Néhémie 7.19
15 Wana wa Adini, mia nne hamsini na wanne.
Néhémie 7.20 Esdras 8.6
16 Wana wa Ateri, wa wana wa Hezekia, tisini na wanane.
Néhémie 7.21
17 Wana wa Besai, mia tatu ishirini na watatu.
Néhémie 7.23
18 Wana wa Harifu, mia moja na kumi na wawili.
Néhémie 7.24
19 Wana wa Hashumu, mia mbili ishirini na watatu.
Néhémie 7.22 Esdras 10.33
20 Watu wa Gibeoni, tisini na watano.
Néhémie 7.25
21 Watu wa Bethlehemu, mia ishirini na watatu.
1 Chroniques 2.50-2.52
22 Watu wa Netofa, hamsini na sita.
2 Samuel 23.28 1 Chroniques 2.54 Jérémie 40.8 Néhémie 7.26
23 Watu wa Anathothi, mia ishirini na wanane.
Néhémie 7.27 Jérémie 1.1 Esaïe 10.30 Jérémie 11.21 Josué 21.18
24 Watu wa Beth-Azmawethi, arobaini na wawili.
Néhémie 7.28
25 Watu wa Kiriath-yearimu, na Kefira, na Beerothi, mia saba arobaini na watatu.
Néhémie 7.29 Josué 9.17
26 Watu wa Rama na Geba, mia sita ishirini na mmoja.
Josué 18.24-18.25 Néhémie 7.30
27 Watu wa Mikmashi, mia moja ishirini na wawili.
Néhémie 7.31 Esaïe 10.28 1 Samuel 13.23 1 Samuel 13.5
28 Watu wa Betheli, na Ai, mia mbili ishirini na watatu.
Genèse 12.8 Josué 8.17 Josué 7.2 Néhémie 7.33 Josué 8.9
29 Watu wa Nebo, hamsini na wawili.
Néhémie 7.33 Esaïe 15.2 Nombres 32.3 Deutéronome 32.49 Jérémie 48.1
30 Watu wa Magbishi, mia moja hamsini na sita.
31 Watu wa Elamu wa pili, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
Esdras 2.7 Néhémie 7.34
32 Watu wa Harimu, mia tatu na ishirini.
Néhémie 7.35 Esdras 10.31
33 Watu wa Lodi, na Hadidi, na Ono, mia saba ishirini na watano.
Néhémie 6.2 Néhémie 11.34-11.35 1 Chroniques 8.12 Néhémie 7.37
34 Watu wa Yeriko, mia tatu arobaini na watano.
1 Rois 16.34 Néhémie 7.36 2 Chroniques 28.15
35 Watu wa Senaa, elfu tatu mia sita na thelathini.
Néhémie 7.38
36 Makuhani; wana wa Yedaya, wa mbari ya Yeshua, mia kenda sabini na watatu.
1 Chroniques 24.7-24.18 1 Chroniques 9.10 Néhémie 7.39 Esdras 3.9
37 Wana wa Imeri, elfu moja hamsini na wawili.
1 Chroniques 24.14 Néhémie 7.40 Esdras 10.20
38 Wana wa Pashuri, elfu moja mia mbili arobaini na saba.
1 Chroniques 9.12 Néhémie 7.41 Esdras 10.22
39 Wana wa Harimu, elfu moja na kumi na saba.
1 Chroniques 24.8 Néhémie 7.42 Esdras 10.21
40 Walawi; wana wa Yeshua, na wana wa Kadmieli wa wana wa Hodavia, sabini na wanne.
Esdras 3.9 Néhémie 7.43
41 Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane.
1 Chroniques 6.39 1 Chroniques 25.1-25.2 Néhémie 11.17 1 Chroniques 15.17 Néhémie 7.44
42 Akina bawabu; wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu, wana wa Hatita, wana wa Shobai; jumla yao ni mia moja thelathini na kenda.
Néhémie 7.45 1 Chroniques 9.17 1 Chroniques 26.1-26.19
43 Wanethini; wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi;
1 Chroniques 9.2 Esdras 2.58 Néhémie 10.28 Néhémie 7.46-7.56
44 wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni;
Néhémie 7.47
45 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Akubu;
Néhémie 7.48
46 wana wa Hagabu, wana wa Salmai, wana wa Hanani;
47 wana wa Gideli, wana wa Gahari, wana wa Reaya;
48 wana wa Resini, wana wa Nekoda, wana wa Gazamu;
49 wana wa Uza, wana wa Pasea, wana wa Besai;
Néhémie 7.51
50 wana wa Asna, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu;
Néhémie 7.52
51 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri;
52 wana wa Basluthi, wana wa Mehida, wana wa Harsha;
Néhémie 7.54
53 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema;
Néhémie 7.55
54 wana wa Nesia, wana wa Hatifa.
55 Wa watumwa wa Sulemani; wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Peruda;
1 Rois 9.21 Néhémie 7.57
56 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli;
Néhémie 7.58
57 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-Sebaimu, wana wa Amoni.
Néhémie 7.59
58 Wanethini wote, pamoja na watumwa wa Sulemani, walikuwa mia tatu tisini na wawili.
1 Chroniques 9.2 1 Rois 9.21 Josué 9.23 Josué 9.27 Néhémie 7.60
59 Na hawa ndio watu waliokwea kutoka Tel-mela, na Tel-harsha, na Kerubu, na Adani, na Imeri; walakini hawakuweza kuonyesha mbari za baba zao, wala kizazi chao, kwamba walikuwa wa Israeli;
Néhémie 7.61
60 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, mia sita hamsini na wawili.
Néhémie 7.62
61 Tena wa makuhani; wana wa Habaya, wana wa Hakosi, wana wa Barzilai, yule aliyeoa mmojawapo wa binti Barzilai, Mgileadi, akaitwa kwa jina lao.
2 Samuel 17.27 1 Rois 2.7 2 Samuel 19.31-19.39 Néhémie 7.63-7.64
62 Hao waliitafuta orodha yao miongoni mwa wale waliohesabiwa kwa nasaba, wasionekane; kwa hiyo walihesabiwa kuwa na unajisi.
Nombres 3.10 Lévitique 21.21-21.23 Nombres 16.39-16.40 Nombres 18.7 Ezéchiel 44.10-44.14
63 Na huyo Tirshatha akawaambia wasile katika vitu vitakatifu sana ,hata atakaposimama kuhani mwenye urimu na Thumimu.
Exode 28.30 Lévitique 2.3 Nombres 27.21 Lévitique 2.10 Lévitique 22.10
64 Basi hilo kusanyiko lote zima, jumla yake ilikuwa watu arobaini na mbili elfu na mia tatu na sitini,
Esaïe 10.20-10.22 Esdras 9.8 Néhémie 7.66-7.69 Jérémie 23.3
65 tena, zaidi ya hao, kulikuwa na watumishi wao waume kwa wake, ambao walikuwa saba elfu, na mia tatu na thelathini na saba; nao walikuwa na waimbaji waume kwa wake mia mbili.
2 Samuel 19.35 Ecclésiaste 2.8 Psaumes 68.25 Esaïe 14.1-14.2 2 Chroniques 35.25
66 Farasi zao walikuwa mia saba thelathini na sita; nyumbu zao, mia mbili arobaini na watano;
67 ngamia zao, mia nne thelathini na watano; punda zao elfu sita, na mia saba na ishirini.
68 Na baadhi ya wakuu wa mbari za baba zao, hapo walipoifikilia nyumba ya Bwana, iliyoko Yerusalemu, walitoa mali kwa ukarimu kwa ajili ya nyumba ya Mungu, ili kuisimamisha mahali pake;
1 Chroniques 22.1 2 Corinthiens 8.3 Luc 21.1-21.4 1 Chroniques 21.18 2 Chroniques 3.1
69 wakatoa kadiri walivyoweza, na kutia katika hazina ya kazi hiyo, darkoni za dhahabu sitini na moja elfu ,na nane za fedha elfu tano,na mavazi mia ya makuhani.
Esdras 8.25-8.34 1 Chroniques 22.14 1 Rois 7.51 Néhémie 7.71-7.72 1 Chroniques 26.20-26.28
70 Hivyo makuhani, na Walawi, na baadhi ya watu, na waimbaji, na mabawabu, na Wanethini, wakakaa mijini mwao, naam, Israeli wote wakakaa mijini mwao.
Néhémie 7.73 Néhémie 11.3-11.36 1 Chroniques 11.2 1 Chroniques 9.2 Esdras 6.16-6.17

Cette Bible est dans le domaine public.