Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 5.23
Bible en Swahili de l’est


Règne de David sur Israël

Sacre de David

1 Ndipo kabila zote za Israeli wakamwendea Daudi huko Hebroni, wakasema naye, wakinena, Tazama, sisi tu mfupa wako na nyama yako.
1 Chroniques 11.1-11.3 2 Samuel 19.13 Deutéronome 17.15 Hébreux 2.14 Juges 9.2
2 Zamani za kale, hapo Sauli alipokuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyewaongoza Israeli watoke nje, na kuingia ndani. Naye Bwana akakuambia, Wewe utawalisha watu wangu Israeli, nawe utakuwa mkuu juu ya Israeli.
Matthieu 2.6 2 Samuel 7.7 1 Samuel 18.13 Esaïe 55.4 1 Samuel 25.30
3 Basi wazee wote wa Israeli wakamwendea mfalme huko Hebroni, naye mfalme Daudi akapatana nao huko Hebroni mbele za Bwana; wakamtia Daudi mafuta awe mfalme juu ya Israeli.
2 Samuel 2.4 Juges 11.11 2 Rois 11.17 2 Samuel 3.21 1 Samuel 23.18
4 Daudi alikuwa amepata miaka thelathini alipoanza kutawala, akatawala miaka arobaini.
1 Chroniques 26.31 1 Chroniques 29.27 Luc 3.23 1 Rois 2.11 1 Chroniques 3.4
5 Huko Hebroni alitawala miaka saba na miezi sita; na katika Yerusalemu alitawala miaka thelathini na tatu juu ya Israeli wote na Yuda.
2 Samuel 2.11 1 Chroniques 3.4 1 Rois 2.11
6 Kisha mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu ili kupigana na Wayebusi, wenyeji wa nchi ile; hao ndio waliomwambia Daudi, wakisema, Usipowaondoa vipofu, na viwete, hutaingia humu kamwe; huku wakidhania ya kuwa Daudi hawezi kuingia humo.
Juges 1.8 Josué 15.63 Juges 1.21 Josué 18.28 Jérémie 37.10
7 Lakini Daudi aliipiga ngome ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi.
1 Rois 2.10 2 Samuel 6.12 2 Samuel 6.16 1 Chroniques 11.7 Esaïe 12.6
8 Naye Daudi alisema siku hiyo, Yeye atakayewapiga Wayebusi, na apande kwenye mfereji wa maji, na kuwapiga viwete, na hao vipofu, ambao roho yake Daudi inawachukia. Kwa sababu hii watu husema, Wako vipofu na viwete hawawezi kuingia nyumbani.
Josué 15.16-15.17 1 Samuel 17.25 1 Chroniques 11.6-11.9
9 Basi Daudi akakaa ndani ya ngome hiyo, akaiita mji wa Daudi. Kisha Daudi akajenga toka Milo na pande za ndani.
1 Rois 9.15 1 Rois 9.24 1 Rois 11.27 2 Samuel 5.7 2 Chroniques 32.5
10 Naye Daudi akazidi kuwa mkuu; kwa maana Bwana, Mungu wa majeshi, alikuwa pamoja naye.
2 Samuel 3.1 Job 17.9 Proverbes 4.18 Psaumes 46.7 Daniel 2.44-2.45
11 Kisha Hiramu, mfalme wa Tiro, akatuma wajumbe kwa Daudi, akampelekea na mierezi, na maseremala, na waashi; nao wakamjengea Daudi nyumba.
1 Chroniques 14.1 1 Rois 5.1-5.2 1 Rois 5.18 Ecclésiaste 2.4-2.11 2 Samuel 7.2
12 Akajua Daudi ya kwamba Bwana amemweka imara awe mfalme juu ya Israeli, na ufalme wake ameutukuza kwa ajili ya watu wake, Israeli.
Esther 4.14 2 Chroniques 2.11 1 Rois 10.9 Esaïe 1.25-1.27 Daniel 2.30
13 Naye Daudi akazidi kujitwalia masuria na wake huko Yerusalemu baada ya kutoka Hebroni; wakazaliwa zaidi kwa Daudi wana na binti.
1 Chroniques 3.9 Deutéronome 17.17 1 Chroniques 14.3-14.7 2 Chroniques 13.21 2 Chroniques 11.18-11.21
14 Na haya ndiyo majina ya hao waliozaliwa kwake huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani,
Luc 2.31 2 Samuel 12.24-12.25 Matthieu 1.6 2 Samuel 12.1-12.7 1 Chroniques 14.4
15 na Ibhari, na Elishua; na Nefegi, na Yafia;
1 Chroniques 3.6 1 Chroniques 14.5
16 na Elishama, na Eliada, na Elifeleti.
1 Chroniques 14.7 1 Chroniques 3.8

Victoires de David sur les Philistins

17 Na hao Wafilisti waliposikia kwamba wamemtia Daudi mafuta ili awe mfalme juu ya Israeli, Wafilisti wote wakapanda kumtafuta Daudi; naye Daudi akapata habari, akashuka akaenda ngomeni.
2 Samuel 23.14 1 Chroniques 11.16 1 Chroniques 14.8-14.9 Psaumes 2.1-2.5 Apocalypse 11.15-11.18
18 Basi Wafilisti walikuwa wamekuja na kujitawanya bondeni mwa Warefai.
Josué 15.8 2 Samuel 23.13 Josué 17.15 Genèse 14.5 Josué 18.16
19 Basi Daudi akauliza kwa Bwana, akisema, Je! Nipande juu ya Wafilisti? Utawatia mkononi mwangu? Naye Bwana akamwambia Daudi, Panda; kwa kuwa hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.
2 Samuel 2.1 1 Samuel 23.2 1 Samuel 28.6 2 Samuel 5.23 1 Rois 22.6
20 Basi Daudi akaja Baal-perasimu, naye Daudi akawapiga huko; akasema, Bwana amewafurikia adui zangu mbele yangu, kama mafuriko ya maji. Basi akapaita mahali pale Baal-perasimu.
Esaïe 28.21
21 Nao wakaziacha sanamu zao huko, na Daudi na watu wake wakaziondolea mbali.
Deutéronome 7.5 1 Chroniques 14.11-14.12 Esaïe 37.19 Deutéronome 7.25 1 Samuel 5.2-5.6
22 Lakini wakapanda hao Wafilisti tena mara ya pili, wakajitawanya bondeni mwa Warefai.
1 Rois 20.22 1 Chroniques 14.13 2 Samuel 5.18
23 Naye Daudi alipouliza kwa Bwana, alisema, Usipande; zunguka nyuma yao, ukawajie huko mbele ya miforsadi.
Josué 8.7 Matthieu 9.29-9.30 Matthieu 8.23-8.25 1 Chroniques 14.14 Josué 8.2
24 Kisha itakuwa, hapo utakapoisikia sauti ya kwenda katika vilele vya miforsadi, ndipo nawe ujitahidi; kwa maana ndipo Bwana ametoka mbele yako awapige jeshi la Wafilisti.
2 Rois 7.6 Juges 4.14 Philippiens 2.11-2.12 Juges 7.15 1 Chroniques 14.15
25 Ndivyo alivyotenda Daudi, vile vile kama Bwana alivyomwagiza; naye akawapiga Wafilisti toka Geba hata ujapo Gezeri.
1 Chroniques 14.16 Esaïe 28.21 Josué 16.10

Cette Bible est dans le domaine public.