Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 14.11
Bible en Swahili de l’est


Abram vainqueur de plusieurs rois

1 Ikawa siku za Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, na Kedorlaoma mfalme wa Elamu na Tidali mfalme wa Goimu,
Genèse 10.10 Genèse 11.2 Genèse 10.22 Esaïe 11.11 Jérémie 49.34-49.39
2 walifanya vita na Bera mfalme wa Sodoma na Birsha mfalme wa Gomora, na Shinabu mfalme wa Adma, na Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela, ndio Soari.
Genèse 13.10 Genèse 10.19 Deutéronome 29.23 Esaïe 15.5 1 Samuel 13.18
3 Hawa wote wakakutana panapo bonde la Sidimu, kwenye Bahari ya Chumvi.
Nombres 34.12 Deutéronome 3.17 Josué 3.16 Genèse 19.24 Psaumes 107.34
4 Miaka kumi na miwili walimtumikia Kedorlaoma, hata mwaka wa kumi na tatu wakaasi.
Genèse 9.25-9.26 Ezéchiel 17.15
5 Na mwaka wa kumi na nne akaja Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja naye, wakawapiga Warefai katika Ashteroth-karnaimu, na Wazuzi katika Hamu, na Waemi katika Shawe-kiryathaimu,
Deutéronome 1.4 Deutéronome 2.10-2.11 Deutéronome 3.11 Genèse 15.20 Psaumes 105.27
6 na Wahori katika mlima wao Seiri, mpaka Elparani iliyo karibu na jangwa.
Deutéronome 2.22 Genèse 21.21 Deutéronome 2.12 Nombres 13.3 Nombres 12.16
7 Kisha wakarudi wakaja mpaka Enmisfati, ndio Kadeshi, wakapiga nchi yote ya Waamaleki, na Waamori waliokaa Hasason-tamari.
2 Chroniques 20.2 Genèse 16.14 Genèse 20.1 1 Samuel 27.1-27.12 Deutéronome 1.19
8 Mfalme wa Sodoma, na mfalme wa Gomora, na mfalme wa Adma, na mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela, ndio Soari, wakatoka wakapanga vita panapo bonde la Sidimu;
Genèse 19.20 Genèse 13.10 Genèse 19.22 Genèse 14.10 Genèse 14.2-14.3
9 wapigane na Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu, na Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, wafalme wanne juu ya wale watano.
10 Na bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami. Nao wafalme wa Sodoma na Gomora wakakimbia, wakaanguka huko, nao waliosalia wakakimbia milimani.
Genèse 19.17 Genèse 19.30 Genèse 11.3 Esaïe 24.18 Jérémie 48.44
11 Wakachukua mali zote za Sodoma na Gomora na vyakula vyao vyote, wakaenda zao.
Genèse 14.21 Genèse 14.16 Deutéronome 28.35 Deutéronome 28.31 Genèse 12.5
12 Wakamtwaa Lutu, mwana wa nduguye Abramu, aliyekaa huko Sodoma, na mali yake, wakaenda zao.
Genèse 11.27 Genèse 12.5 Apocalypse 3.19 1 Timothée 6.9-6.11 Job 9.23
13 Mtu mmoja aliyeponyoka akaenda, akampasha habari Abramu Mwebrania; naye amekaa panapo mialoni ya Mamre, yule Mwamori, ndugu ya Eshkoli, na ndugu ya Aneri, na hao walikuwa wamepatana na Abramu.
Genèse 13.18 Genèse 14.24 Genèse 40.15 Exode 2.6 Exode 2.11
14 Abramu aliposikia ya kwamba nduguye ametekwa mateka, akawapa silaha vijana wake, waliozaliwa katika nyumba yake, watu mia tatu na kumi na wanane, akawafuata mpaka Dani.
Juges 18.29 Genèse 15.3 Ecclésiaste 2.7 Deutéronome 34.1 Genèse 17.27
15 Akajipanga apigane nao usiku, yeye na watumwa wake, akawapiga, akawafukuza mpaka Hoba, ulioko upande wa kushoto wa Dameski.
Actes 9.2 Deutéronome 15.2 1 Rois 15.18 Psaumes 112.5 Esaïe 41.2-41.3
16 Naye akarudisha mali zote, akamrudisha na Lutu nduguye na mali zake, na wanawake pia, na watu.
1 Samuel 30.18-30.19 1 Samuel 30.8 Genèse 14.11-14.12 Esaïe 41.2 Genèse 12.2

Abram béni par Melchisédek

17 Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme.
2 Samuel 18.18 Proverbes 19.4 Hébreux 7.1 1 Samuel 18.6 Proverbes 14.20
18 Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
Psaumes 110.4 Hébreux 5.6 Hébreux 5.10 Matthieu 26.26-26.29 Actes 16.17
19 Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.
Genèse 14.22 Hébreux 7.6-7.7 Matthieu 11.25 2 Samuel 2.5 Actes 16.17
20 Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.
Genèse 28.22 Luc 18.12 Genèse 24.27 Malachie 3.10 2 Chroniques 31.12
21 Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, Nipe mimi hao watu, na hizo mali uchukue wewe.
22 Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi,
Exode 6.8 Daniel 12.7 Apocalypse 10.5-10.6 Psaumes 24.1 Deutéronome 32.40
23 ya kuwa sitatwaa uzi wala gidamu ya kiatu wala cho chote kilicho chako, usije ukasema, Nimemtajirisha Abramu;
2 Rois 5.16 Esther 9.15-9.16 2 Corinthiens 11.9-11.12 1 Rois 13.8 Hébreux 13.5
24 isipokuwa hivyo walivyokula vijana, na sehemu za watu waliokwenda nami, yaani, Aneri, na Eshkoli, na Mamre; na watwae wao sehemu zao.
Romains 13.7-13.8 Matthieu 7.12 1 Corinthiens 9.14-9.15 1 Timothée 5.18 Genèse 14.13

Cette Bible est dans le domaine public.