Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 19.9
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha Sauli akasema na mwanawe Yonathani, tena na watumishi wake wote, kwamba wamwue Daudi.
1 Samuel 18.1 1 Samuel 18.9
2 Lakini huyo Yonathani, mwana wake Sauli, alikuwa akipendezwa sana na Daudi. Basi Yonathani akamwambia Daudi, akasema, Sauli, baba yangu, anatafuta kukuua; basi, nakusihi, ujiangalie sana asubuhi, ukae mahali pa siri na kujificha;
Proverbes 17.17 1 Samuel 18.1-18.3 1 Samuel 20.2 Psaumes 16.3 1 Jean 3.12-3.14
3 na mimi nitatoka nje na kusimama kando ya babangu huko shambani ulipo wewe, nami nitazungumza na babangu habari zako; nami nikiona neno lo lote nitakuambia.
1 Samuel 20.9 1 Samuel 20.13
4 Naye Yonathani akamsifu Daudi kwa Sauli, babaye akamwambia, Mfalme asikose juu ya mtumishi wake, yaani, juu ya Daudi kwa maana yeye hakukosa juu yako, tena matendo yake kwako yamekuwa mema sana.
Jérémie 18.20 Genèse 42.22 Proverbes 31.8-31.9 Proverbes 17.13 1 Samuel 20.32
5 Kwa kuwa alitia uhai wake mkononi mwake, na kumpiga yule Mfilisti, naye Bwana akawatendea Israeli wote wokovu mkuu. Wewe mwenyewe uliona jambo hilo, ukafurahi; basi kwa nini kukosa juu ya damu isiyo na hatia, umwue huyo Daudi bure?
Matthieu 27.4 1 Samuel 11.13 1 Chroniques 11.14 1 Samuel 28.21 1 Samuel 20.32
6 Sauli akaisikiliza sauti ya Yonathani; naye Sauli akaapa, Aishivyo Bwana, yeye hatauawa.
1 Samuel 19.10-19.11 1 Samuel 28.10 Psaumes 15.4 Jérémie 5.2 Proverbes 26.24-26.25
7 Basi Yonathani akamwita Daudi, naye Yonathani akamjulisha mambo hayo yote. Kisha Yonathani akamleta Daudi kwa Sauli, naye alikuwa akihudhuria mbele yake, kama kwanza.
1 Samuel 18.13 1 Samuel 16.21 1 Samuel 18.2 1 Samuel 18.10 Esaïe 30.33
8 Baada ya hayo kulikuwa na vita tena; naye Daudi akatoka, naye akapigana na Wafilisti, naye akawaua kwa uuaji mkuu; nao wakakimbia mbele yake.
Psaumes 27.3 Psaumes 18.32-18.50
9 Tena ikawa, roho mbaya kutoka kwa Bwana ilimjilia Sauli, hapo alipoketi ndani ya nyumba yake, akiwa na mkuki wake mkononi mwake; naye Daudi alikuwa akipiga kinubi kwa mkono wake.
1 Samuel 16.14 1 Samuel 18.10-18.11 1 Samuel 16.16
10 Sauli akajaribu kumpiga Daudi hata ukutani kwa mkuki wake, ila yeye akaponyoka kutoka mbele ya Sauli, nao huo mkuki akaupiga ukutani; naye Daudi akakimbia, akaokoka usiku ule.
1 Samuel 20.33 1 Samuel 18.11 Psaumes 34.19 Proverbes 21.30 2 Pierre 2.20-2.22
11 Kisha Sauli akatuma wajumbe mpaka nyumbani kwa Daudi, ili wamvizie na kumwua asubuhi; naye Mikali, mkewe Daudi, akamwambia, akasema, Wewe usipojiponya nafsi yako usiku huu, kesho utauawa.
Psaumes 59.1-59.17 Juges 16.2
12 Basi Mikali akamtelemsha Daudi dirishani; naye akaenda akakimbia na kuokoka.
Josué 2.15 Actes 9.24-9.25 2 Corinthiens 11.32-11.33 Psaumes 34.19
13 Ndipo Mikali akakitwaa kinyago, na kukilaza kitandani, akatia na mto wa singa za mbuzi kichwani pake, na kukifunika kwa nguo.
Genèse 31.19 Juges 18.17 Juges 18.14 Juges 17.5 Osée 3.4
14 Naye Sauli alipotuma wajumbe ili kumkamata Daudi, yeye alisema, Hawezi.
Josué 2.5 2 Samuel 17.20 2 Samuel 16.17-16.19
15 Basi Sauli akawatuma hao wajumbe ili wamtazame Daudi, akisema, Mleteni kwangu juu ya kitanda chake, nipate kumwua.
Psaumes 37.12 Job 31.31 Proverbes 27.3-27.4 1 Samuel 19.6 Romains 3.15
16 Nao wajumbe walipoingia, kumbe! Kuna kinyago kitandani, na mto wa singa za mbuzi kichwani pake!
17 Sauli akamwambia Mikali, Mbona wewe umenidanganya hivi, na kumwacha adui yangu aende, hata ameniponyoka? Naye Mikali akamjibu Sauli, Yeye aliniambia, Niache niende zangu; kwa nini nikuue?
2 Samuel 2.22 Galates 4.16 1 Rois 21.20 1 Samuel 22.17 1 Samuel 28.12
18 Hivyo Daudi akakimbia, akajiponya, akamwendea Samweli huko Rama, akamwambia hayo yote Sauli aliyomtenda. Kisha yeye na Samweli wakaenda na kukaa katika Nayothi.
1 Samuel 7.17 1 Samuel 15.34 Psaumes 116.11 1 Samuel 28.3 Jacques 5.16
19 Naye Sauli akaambiwa, kusema, Angalia, yule Daudi yuko katika Nayothi, huko Rama.
1 Samuel 23.19 1 Samuel 22.9-22.10 Proverbes 29.12 1 Samuel 26.1
20 Basi Sauli akatuma wajumbe ili kumkamata Daudi; nao hapo walipowaona jamaa ya manabii wakitabiri, na Samweli amesimama kama mkuu wao, roho ya Mungu ikawajilia wajumbe wa Sauli, nao pia wakatabiri.
Jean 7.32 1 Samuel 10.10 Joël 2.28 1 Samuel 19.14 1 Samuel 10.5-10.6
21 Naye Sauli alipoambiwa, alituma wajumbe wengine, wao nao wakatabiri. Naye Sauli akatuma wajumbe tena mara ya tatu, na wao pia wakatabiri.
Proverbes 27.22 Joël 2.28 Jérémie 13.23 2 Rois 1.9-1.13
22 Kisha yeye mwenyewe akaenda Rama, akafika kunako kile kisima kikubwa kilicho huko Seku; akauliza, akasema, Je! Wako wapi Samweli na Daudi? Na mtu mmoja akajibu, Tazama, wako Nayothi, huko Rama.
23 Basi akaenda Nayothi huko Rama, na roho ya Mungu ikamjilia yeye naye, akaendelea mbele, huku anatabiri, mpaka kufika Nayothi huko Rama.
1 Samuel 10.10 1 Samuel 19.20 Nombres 23.5 1 Corinthiens 13.2 Nombres 24.2
24 Naye akavua nguo zake, akatabiri mbele ya Samweli, akalala uchi mchana kutwa na usiku kucha siku ile. Kwa hiyo watu husema, Je! Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?
Michée 1.8 2 Samuel 6.20 Esaïe 20.2 1 Samuel 10.10-10.12 Actes 9.21

Cette Bible est dans le domaine public.