Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 16.19
Bible en Swahili de l’est


Onction de David comme roi d’Israël

1 Bwana akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.
1 Samuel 15.23 1 Samuel 15.35 1 Samuel 9.16 2 Rois 9.1 1 Samuel 10.1
2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi Bwana akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea Bwana dhabihu.
1 Samuel 9.12 1 Samuel 20.29 Jérémie 38.26-38.27 Exode 3.11 Matthieu 10.16
3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako.
1 Samuel 9.16 Exode 4.15 Actes 9.6 1 Samuel 16.12-16.13 2 Samuel 15.11
4 Samweli akafanya hayo aliyosema Bwana, akaenda Bethlehemu. Wakaja wazee wa mji kumlaki, wakitetemeka, nao wakasema, Je! Umekuja kwa amani?
1 Rois 2.13 2 Rois 9.22 1 Samuel 21.1 1 Chroniques 12.17-12.18 Luc 8.37
5 Naye akasema, Naam, kwa amani; nimekuja kumtolea Bwana dhabihu; jitakaseni; njoni pamoja nami kwenye dhabihu. Akawatakasa Yese na wanawe, akawaita kwenye dhabihu.
Exode 19.10 Josué 3.5 Lévitique 20.7-20.8 1 Corinthiens 11.28 Nombres 11.8
6 Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake.
1 Samuel 17.13 1 Chroniques 2.13 1 Samuel 17.22 Juges 8.18 1 Chroniques 27.18
7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo.
Jean 7.24 Jérémie 17.10 Luc 16.15 1 Chroniques 28.9 Esaïe 55.8-55.9
8 Ndipo Yese akamwita Abinadabu, akampitisha mbele ya Samweli. Naye akasema, Bwana hakumchagua huyu.
1 Samuel 17.13 1 Chroniques 2.13
9 Ndipo Yese akampitisha Shama. Naye akasema, wala Bwana hakumchagua huyu.
1 Samuel 17.13 2 Samuel 13.3 1 Chroniques 2.13
10 Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa.
1 Chroniques 2.13-2.15
11 Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, Amesalia mdogo wao, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku.
Psaumes 78.70-78.71 1 Chroniques 17.7 2 Samuel 7.8 2 Samuel 13.3 1 Samuel 17.12-17.15
12 Basi akatuma mtu, naye akamleta kwao. Naye alikuwa mwekundu, mwenye macho mazuri, na umbo lake lilikuwa la kupendeza. Bwana akasema, Ondoka, umtie mafuta; maana huyu ndiye.
1 Samuel 17.42 1 Samuel 9.17 Actes 7.20 Genèse 39.6 Psaumes 2.2
13 Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama.
1 Samuel 10.6 1 Samuel 10.1 1 Samuel 10.9-10.10 Nombres 27.18 Juges 11.29
14 Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.
1 Samuel 18.10 1 Samuel 28.15 1 Samuel 18.12 Juges 9.23 Psaumes 51.11
15 Nao watumishi wa Sauli wakamwambia, Angalia, sasa roho mbaya kutoka kwa Mungu inakusumbua.
16 Basi bwana wetu na atuamuru sisi watumishi wake waliopo hapa mbele yako watafute mtu aliye stadi wa kupiga kinubi; basi itakuwa, roho ile mbaya kutoka kwa Mungu itakapokujilia, yeye atapiga kinubi kwa mkono wake, nawe utapona.
2 Rois 3.15 1 Samuel 16.21-16.23 1 Rois 10.8 1 Samuel 19.9 1 Samuel 18.10
17 Basi Sauli akawaambia, Vema, nitafutieni mtu aliye stadi wa kupiga kinubi, mkaniletee.
18 Ndipo akajibu mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama, nimemwona mwana mmoja wa Yese, Mbethlehemi, aliye stadi wa kupiga kinubi, tena ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye Bwana yu pamoja naye.
1 Samuel 3.19 1 Samuel 17.32-17.36 2 Samuel 17.10 Genèse 39.23 Genèse 39.2
19 Basi Sauli akampelekea Yese wajumbe, akasema, Nipelekee Daudi mwanao, aliye pamoja na kondoo.
1 Samuel 16.11 1 Samuel 17.15 Psaumes 78.70-78.72 Matthieu 4.18-4.22 Amos 7.14-7.15
20 Yese akatwaa punda, wa kuchukua mikate, na kiriba cha divai, na mwana-mbuzi, akampelekea Sauli kwa mkono wa Daudi mwanawe.
1 Samuel 10.27 Proverbes 18.16 1 Samuel 17.18 Genèse 43.11 1 Samuel 25.18
21 Basi Daudi akamwendea Sauli, akasimama mbele yake, naye akampenda sana; naye akapata kuwa mtu wa kumchukulia silaha zake.
Proverbes 22.29 Genèse 41.46 Psaumes 146.3 Psaumes 62.9 Psaumes 118.9
22 Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, mwache Daudi asimame mbele yangu; maana ameona kibali machoni pangu.
23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha.

Cette Bible est dans le domaine public.