Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jacques 3.17
Bible en Swahili de l’est


L’usage de la parole

1 Ndugu zangu, msiwe waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi.
Matthieu 23.13 2 Timothée 1.11 1 Pierre 5.3 2 Corinthiens 5.10 1 Timothée 1.7
2 Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu.
Jacques 1.26 Matthieu 12.37 1 Pierre 3.10 Proverbes 13.3 Jacques 3.5-3.6
3 Angalieni, twatia lijamu katika vinywa vya farasi, ili wamtii, hivi twageuza mwili wao wote.
Psaumes 32.9 Psaumes 39.1 Jacques 1.26 Esaïe 37.29 2 Rois 19.28
4 Tena angalieni merikebu; ingawa ni kubwa kama nini, na kuchukuliwa na pepo kali, zageuzwa na usukani mdogo sana, ko kote anakoazimia kwenda nahodha.
Actes 27.14-27.38 Psaumes 107.25-107.27 Jonas 1.4 Matthieu 8.24
5 Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.
Jérémie 9.3-9.8 Psaumes 17.10 Psaumes 52.1-52.2 Psaumes 73.8-73.9 Psaumes 12.2-12.4
6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.
Proverbes 16.27 Marc 7.20-7.22 Marc 7.15 Matthieu 15.11-15.20 Colossiens 3.8-3.9
7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.
8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
Romains 3.13 Psaumes 140.3 Jacques 3.6 Psaumes 55.21 Ecclésiaste 10.11
9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
1 Corinthiens 11.7 Genèse 1.26-1.27 Matthieu 26.74 Ecclésiaste 7.22 Psaumes 145.21
10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.
1 Pierre 3.9 1 Corinthiens 3.3 Psaumes 50.16-50.20 Genèse 20.9 Romains 12.14
11 Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?
12 Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu.
Luc 6.43-6.44 Matthieu 7.16-7.20 Jérémie 2.21 Matthieu 12.33 Romains 11.16-11.18

Sagesse et mauvais désirs

13 N’nani aliye na hekima na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole wa hekima.
Jacques 2.18 1 Pierre 2.12 Psaumes 107.43 Jacques 1.21 Ecclésiaste 8.5
14 Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli.
Jacques 3.16 Philippiens 2.3 2 Corinthiens 12.20 Philippiens 1.15 1 Corinthiens 3.3
15 Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani.
Jacques 1.17 Jude 1.19 Philippiens 3.19 2 Corinthiens 1.12 1 Timothée 4.1
16 Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya.
1 Corinthiens 3.3 Jacques 3.14 Galates 5.20 1 Jean 3.12 Actes 19.29
17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki.
Jacques 1.17 Romains 12.9 1 Corinthiens 2.6-2.7 Jacques 1.5 1 Corinthiens 13.4-13.7
18 Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.
Matthieu 5.9 Philippiens 1.11 Esaïe 32.16-32.17 Galates 6.8 Hébreux 12.11

Cette Bible est dans le domaine public.