Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Timothée 5
Bible en Swahili de l’est


Conseils à propos des membres de l’Église

1 Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;
1 Pierre 5.5-5.6 Lévitique 19.32 Tite 2.6 Tite 2.2 1 Timothée 5.19-5.20
2 wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote.
1 Timothée 4.12 Matthieu 12.50 Philippiens 4.8 Jean 19.26-19.27 2 Timothée 2.22
3 Uwaheshimu wajane walio wajane kweli kweli.
Actes 6.1 Exode 20.12 Deutéronome 16.11 Actes 9.39 Deutéronome 27.19
4 Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.
Matthieu 15.4-15.6 Jean 19.26-19.27 Genèse 45.10-45.11 Ruth 2.2 Ruth 2.18
5 Basi yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake, huyo amemwekea Mungu tumaini lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na usiku.
1 Timothée 5.3 Luc 2.37 1 Pierre 3.5 1 Corinthiens 7.32 Luc 18.1
6 Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai.
Jacques 5.5 Apocalypse 3.1 Luc 15.24 Ephésiens 5.14 1 Samuel 25.6
7 Mambo hayo pia uyaagize, ili wasiwe na lawama.
1 Timothée 4.11 Tite 2.15 1 Timothée 6.17 2 Timothée 4.1 1 Timothée 1.3
8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.
Tite 1.16 2 Corinthiens 12.14 Esaïe 58.7 Galates 6.10 Luc 11.11-11.13
9 Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja;
1 Timothée 3.2 1 Timothée 3.12 Luc 2.36-2.37 1 Corinthiens 7.39-7.40 1 Timothée 5.14
10 naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema.
Tite 3.8 1 Timothée 6.18 1 Pierre 2.12 Luc 7.44 Actes 9.36
11 Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;
1 Timothée 5.14 Osée 13.6 Deutéronome 32.15 Jacques 5.5 1 Timothée 5.9
12 nao wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza.
Galates 1.6 Apocalypse 2.4-2.5 1 Pierre 4.17 Jacques 3.1 1 Corinthiens 11.34
13 Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.
Proverbes 20.19 Tite 1.11 1 Pierre 4.15 Proverbes 31.27 Jacques 3.10
14 Basi napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, wawe na madaraka ya nyumbani; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu.
Tite 2.5 1 Timothée 6.1 Tite 2.8 1 Timothée 4.3 2 Corinthiens 11.12
15 Kwa maana wengine wamekwisha kugeuka na kumfuata Shetani.
2 Pierre 2.2 Jude 1.4-1.5 Apocalypse 12.9 Matthieu 4.10 1 Timothée 1.20
16 Mwanamke aaminiye, akiwa ana wajane, na awasaidie mwenyewe, Kanisa lisilemewe; ili liwasaidie wale walio wajane kweli kweli.
1 Timothée 5.3-5.5 1 Timothée 5.8
17 Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.
Romains 12.8 Luc 10.7 Philippiens 2.29 Hébreux 13.17 Galates 6.6
18 Kwa maana andiko lasema, Usimfunge kinywa ng’ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira wake.
Deutéronome 25.4 Luc 10.7 Matthieu 10.10 Lévitique 19.13 Deutéronome 24.14-24.15
19 Usikubali mashitaka juu ya mzee, ila kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.
Matthieu 18.16 Deutéronome 19.15 Deutéronome 17.6 Jean 18.29 Tite 1.6
20 Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope.
Deutéronome 13.11 2 Timothée 4.2 Tite 1.13 1 Timothée 1.20 Actes 19.17
21 Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, na mbele za malaika wateule, uyatende hayo pasipo kuhukumu kwa haraka; usifanye neno lo lote kwa upendeleo.
2 Timothée 4.1 1 Timothée 6.13 2 Timothée 2.14 2 Pierre 2.4 Jude 1.6
22 Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi.
1 Timothée 3.10 Ephésiens 5.11 Actes 6.6 2 Jean 1.11 1 Timothée 3.6
23 Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara.
Psaumes 104.15 1 Timothée 3.8 Tite 2.3 Tite 1.7 Proverbes 31.4-31.7
24 Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata.
Actes 8.18 2 Timothée 4.10 Actes 1.16-1.20 Actes 5.1-5.11 2 Pierre 2.20-2.21
25 Vivyo hivyo matendo yaliyo mazuri ya dhahiri; wala yale yasiyo dhahiri hayawezi kusitirika.
Luc 11.33 Proverbes 10.9 Actes 10.22 Actes 9.36 Psaumes 37.5-37.6

Cette Bible est dans le domaine public.